Nilipotaka kuchimba kisima changu na kuona haya makampuni yanavyochimba mikwara ya utafiti tu nilichoka na kuishiwa nguvu. Nikakumbuka jana yake jirani yangu aliponiambia kuna kikundi cha vijana wajasiri mali wanachimba kisima kwa gharama nafuu na wana uzoefu wa kujua kama maji yanapatikana au laa katika eneo hilo. Nikaamua kurudi niwatafute hao vijana, na kweli walipofika eneo hilo wakafanya utafiti kutokana na visima vilivyochimwa awali na wakasema 90% maji yapo chini ya ardhi Ft 80 - 100.
Ingwawa ilikuwa risk nilijilazimisha kuwaamini kutokana na majirani wa hapo kuwa na visima vingi tu vya maji. Bila ajizi vijana wali-drill kisima cha maji kwa zana zao za kimachinga na walipofikia Ft 55 dalili za maji zilianza na wakanihakikishia wanataka wafikishi ft 80 ili kupata maji baridi bila chumvi.
Nikuhakikishie hadi leo napata maji safi baridiii toka Ft 80 chini ya ardhi kwa gharama nafuu sana, kwani gharama zote za kuchimba kisima na kukamilika kuweka pump ilinigharibu
Tz Shs 1,200,000. Gharama hii ni tofauti na ile waliyoniambia wataalamu maana wao utafiti tu zaidi ya laki tatu zingenitoka.
- Mambo ya msingi yanayotakiwa uyaandae ni kujaribu kuangalia waliokutangulia maeneo hayo kama wana maji ya visima na pia kujirishisha kwamba eneo lako haliko kwenye mwinuko zaidi ya wenzako walio na visima eneo lako.
- Ukubwa wa kisima chako ni diameter ngapi kulingana na mabomba mengi yanayopatikana ambyo kwa kawaida ni mabomba magumu ya Plastic yatakayozamisha ili kuhifadhi maji ndani ya kisima chako.
- Kuna mchanga wa pekee wa kutiwa kwenye basement ya kisima chako na kando ya bomba ili kuchuja maji yawe maangavu zaidi, wachimbaji wa visima wanajua wapi kwa kupata mchanga huo hasa kandokando ya vijito vya maji, na kuna wauzaji mitaani wa mchanga huo ila hakikisha umehakikiwa na wazoefu wa visima vya maji usijechukua mchanga unaotoa vumbi k uchafua tena maji yako zaidi.
- Mabomba yatakayounganishwa hadi chini ambayo ni ya plastic ya kuhifadhi maji tokana na chemchemi.
- Kifuniko cha juu kwenye kisima chako ili kulinda na kuhifahdi kisima kisiharibiwe na maji machafu yasiingie tena.
- Pump ya maji na tank la maji.
Maelezo hayo ni kwa kisima ambacho ni drilled ambacho pia ni salama kwa familia yako tofauti na kisima chenye shimo kubwa la kuchimbwa ambalo pia si salama kwa famili na huweza sababisha mmommonyoko wa ardhi.
Kama nafasi inakuruhusu kuwatumia wataalamu zaidi ni bora tu ila ujue gharama nazo zinaendana na kiwango cha ukubwa na elimu ya mtu.