GenZ wamekataa kutawaliwa na mkoloni mweusi

GenZ wamekataa kutawaliwa na mkoloni mweusi

Bagamoyo

Platinum Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
29,869
Reaction score
34,025
VIEWS 52,000
29 November 2025
Sumbawanga, Tanzania

M/KITI WA CHADEMA SUMBAWANGA ADOLF MKONO AFUNGUKA MAZITO KWENYE KONGAMANO LA VIJANA | TUNA MAUMIVU


View: https://m.youtube.com/watch?v=12pTD54NCT8

DC, DAS na Samia wapewa ukweli

GenZ siyo wa kwanza kukataa ukoloni, wakati wa vuguvugu la vita ya Majimaji waTanganyika 300,000 walipoteza maisha kupinga ukoloni

Hizi stori za kuwa waTanzania hawajawahi kupoteza maisha wakikataa ukoloni. Hivyo GenZ ni watanzania wanaorudia historia ya vuguvugu la Majimaji na wapo tayari kumpinga mkoloni mweusi anakumbushia mwenyekiti wa CHADEMA Sumbawanga..

Anaongeza kuwa watawala wakoloni weusi waliopo Dodoma ni makaburu pia, kwa kuwabagua watanzania wenzao wasiokuwepo ktk CCM anakumbushia mwenyekiti wa CHADEMA huku DC wa Sumbawanga na kamati yake ya ulinzi na usakama wakitoa macho kushangaa ukumbi ukiofurika mjini Sumbawanga wakishangilia nondo za kada huyo wa chama kikuu mbadala cha nchini Tanzania ..

Kada huyo akumbushia kiburi cha watawala 2019 TAMISEMI, 2020, 2024 na juzi Oktoba 29, 2025 ambapo watanzania GenZ wakakataa kuendelea kuona kiburi cha serikali ya CCM

Mwaka 1884 kurudi nyuma watu wa Sumbawanga na maeneo mengine walikuwa wanachagua viongozi wao. Mwaka 1885 wakoloni wakakaa kule Berlin na kutuchagulia viongozi. Leo hii CCM nayo inafanya mambo yaleyale ya Bismarck wa Ujerumani, Samia na CCM wanakaa Dodoma kutulazimisha kukubali viongozi ambao hawaja chaguliwa kuja kuwatawala CCM wanana kiburi cha mkoloni mweusi...

Watawala wa Dodoma ni lazima wakubali wakati ni ukuta, mabadiliko ni lazima ili haki na amani iwepo..
 
Back
Top Bottom