Greenwhich
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 1,337
- 968
Gazeti la HOJA linalomilikiwa na anayedaiwa kuwa ni kada mashuhuri wa CCM limeendelea kutoa taarifa mbalimbali za kukichafua chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA.
Gazeti hilo linalotoka kila Ijumaa limekuwa likiandika taarifa na makala mbalimbali zinaonekana wazi ni za kisiasa zenye lengo la kuichafua CHADEMA mbele ya Jamii.
Gazeti hilo hivi karibuni lilitoa kile linachodai ni njama za viongozi wa chama hicho kutaka kumfukuza uanachama mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe.Pia wiki nyingine iliyofuata lilishambulia operesheni M4C kwa madai kwamba ni feki na ina lengo la kuvuruga amani ya nchi.
Pia siku chache zilizopita gazeti hilo lilishambulia wabunge wa CHADEMA kwamba ni wabunge wa hovyo na wasiojua kanuni wala sheria na kuwaomba watanzania wasichague tena wabunge wa chama hicho.
Wiki iliyopita gazeti hilo la HOJA lilidai makao makuu ya CHADEMA yanamwandaa Josephine Slaa kugombea ubunge jimbo la Kawe.Lengo kubwa la habari hiyo ni kuleta vurugu kati ya Josephine na Halima Mdee na kuwachanganya wanachama.
Katika toleo lake la Jana gazeti hilo lilidai CHADEMA kinajiandaa kumfukuza uanachama mbunge wake John Shibuda kwa kile walichodai waliona ripoti ya Marando kwenda Kamati kuu inayodai Shibuda ni mamluki wa CCM na anapaswa kufukuzwa mara moja.Pia kwa unafiki mkubwa gazeti hilo lililaani viongozi wa CHADEMA wenye kadi za CCM kwa madai wanahujumu demokrasia ndani ya vyama vingi.
Kwa mifano hii niliyotoa hapo juu ni wazi gazeti hili linaonekana wazi lipo kwa malengo maalum.
Gazeti hilo linalotoka kila Ijumaa limekuwa likiandika taarifa na makala mbalimbali zinaonekana wazi ni za kisiasa zenye lengo la kuichafua CHADEMA mbele ya Jamii.
Gazeti hilo hivi karibuni lilitoa kile linachodai ni njama za viongozi wa chama hicho kutaka kumfukuza uanachama mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe.Pia wiki nyingine iliyofuata lilishambulia operesheni M4C kwa madai kwamba ni feki na ina lengo la kuvuruga amani ya nchi.
Pia siku chache zilizopita gazeti hilo lilishambulia wabunge wa CHADEMA kwamba ni wabunge wa hovyo na wasiojua kanuni wala sheria na kuwaomba watanzania wasichague tena wabunge wa chama hicho.
Wiki iliyopita gazeti hilo la HOJA lilidai makao makuu ya CHADEMA yanamwandaa Josephine Slaa kugombea ubunge jimbo la Kawe.Lengo kubwa la habari hiyo ni kuleta vurugu kati ya Josephine na Halima Mdee na kuwachanganya wanachama.
Katika toleo lake la Jana gazeti hilo lilidai CHADEMA kinajiandaa kumfukuza uanachama mbunge wake John Shibuda kwa kile walichodai waliona ripoti ya Marando kwenda Kamati kuu inayodai Shibuda ni mamluki wa CCM na anapaswa kufukuzwa mara moja.Pia kwa unafiki mkubwa gazeti hilo lililaani viongozi wa CHADEMA wenye kadi za CCM kwa madai wanahujumu demokrasia ndani ya vyama vingi.
Kwa mifano hii niliyotoa hapo juu ni wazi gazeti hili linaonekana wazi lipo kwa malengo maalum.