IST/Vitz/Swift/Honda Fit
Ninamiliki moja kati ya hizo babywoka.
Nachotaka kujua ni je: Gari yangu itakua na matatizo sehemu ama ndio kawaida ya hizi babywoka.
Siku za weekend demu wangu huwa anakuja kunitembelea getto (mitaa ya Ubungo Riverside).
Jioni namrudisha kwao, anaishi Bunju na dada yake. Nikifika kule tena tunakaa weeee, wanapika chakula kitamu, nakula kisha usiku ukiwa mwingi naaga narudi zangu Ubungo.
Sasa kwa kuwa muda huo wa usiku traffic jams Bagamoyo Road zinakua zimepungua, gari chache, fujo za daladala zimefifia basi huwa natembea speed sana.
Naomba niseme tu huwa naamua kuanzisha ligi ndogondogo za magari mengine. Nayapita shaaaa nafurahi kinoma.
Tatizo nikifika speed kuanzia 80 mpaka 100 naona gari inakua nyepesi kinoma, inakua kama inataka kutoka barabarani. Yaani hata kutulia kwenye lane yangu inakua kazi.
Jana kuna Nissan Murano ilinipita pale Kibo Complex. Namie nikaamua kukimbizana nayo. Fyaaaaa fyaaaa fyuuuu... Gari ikawa inataka sijui kupaaa... Aaah mwisho nikaamua nirudi tu kwenye 60 kph. Jamaa huyooo nikaenda kumkuta mataa ya mwenge.
Sasa wakuu, hii tabia ya babywoka yangu kuwa nyepesi kama karatasi, kupoteza stability na kushindwa kutulia on the road during high speed ni kwamba gari ina tatizo ama ndio wekaness ya hizi gari ndogo.
Kama ndio zilivo niambieni nijue kabisaaa kuwa natakiwa kukaza my 'a$$' nivute Subaru Forester at the helm of next year.