Hi Guys,
Kwa wale wapenda movie za animation bas lazima utakuwa umeshaangalia movie inayoitwa COCO iliyotoka mwaka 2017.
Hapa Tanzania kuna kijiji kinachoitwa GAMBOSHI nimewahi kusikia story ya kijiji hiki inasemekana watu wanaokufa kimazingara ya kichawi huwa wanapelekwa huko. Huko kuna maisha yanaendelea kama sisi huku duniani. Kwa maana ya kwamba kuna Michezo, burudani, Siasa na biashara zinaendelea kila siku kama huku kwetu duniani..
Katika kuiangalia hii movie maudhui yake na nilichokisikia kuhusu Gamboshi kinanipa mawazo.
INAWEZEKANA KUWA UKIFA HAPA DUNIANI BAS HATA HUKO UENDAKO KUNA MAISHA KAMA UNAYOYAACHA HAPA DUNIANI...
Mpaka sasa najiuliza aliyetengeneza story ya movie ya COCO aliwaza nini au idea aliipata wapi..
View attachment 1370820
Sent using
Jamii Forums mobile app