Funga za Sunnah kwa Waislamu

Funga za Sunnah kwa Waislamu

_*KESHO NI FUNGA YA ALHAMISI KATIKA MIEZI MITUKUFU*

قال ﷺ | من صام يومًا في سبيلِ اللهِ ، باعدَ اللهُ وجهَهُ عن النَّارِ سبعينَ خريفا.

Mtume ﷺ amesema: "Anayefunga siku moja kwa ajili ya Allah, Allah atamuepusha(atauweka mbali) uso wake na Moto wa Jahannam kwa umbali wa miaka sabini."
﴿ متفق عليه

Nasaha:
Hata kama hufungi, basi wakumbushe wengine... kwani kuna wengi watakao funga kwa sababu ya ukumbusho wako, nawe utapata thawabu zao Biidhni llaah.
قال رسول الله ﷺ:
«مَن دلَّ على خيرٍ، فله مثلُ أجرِ فاعِلِه»

Amesema Mtume ﷺ:
"Aliyeongoza kwenye kheri atapata thawabu sawa na yule atakayefanya kheir hiyo-(bila kupunguza chochote katika ujira wao)."
رواه مسلم_

Kwa faida mbali mbali ungana nasi YOUTHS SALAFIYYAH_TZ 🇹🇿kupitia link 👇🏼

 
WAISLAMU TUMEFIWA NA SHEIKH WETU KIPENZI
وصية الشيخ الإمام ربيع لأبنائه أن لا يقام له مجلس عزاء
وهذه رسالة لأحد أبناء الشيخ ربيع رحمه الله :

"السلام عليكم
الأخوة الأحبة
العزاء عن طريق الواتس يكفي
او الاتصال
وصية الوالد رحمه الله لا يقام له مجلس عزاء
لاتنسوه من صالح الدعاء"
Wosia wa Sheikh Imam Rabi’ kwa watoto wake ni kwamba asifanyiwe kikao cha maombolezo.

Na huu ni ujumbe kutoka kwa mmoja wa watoto wa Sheikh Rabi’ (rahimahullah):

**"Assalaamu alaykum
Ndugu wapendwa,
Kutoa pole kupitia WhatsApp inatosha,
au kwa kupiga simu.
Wosia wa baba (rahimahullah) ni kwamba asifanyiwe kikao cha maombolezo.
Msimusahau katika dua njema."**
 
Hakika ya kuondoka kwa Wanazuoni ni pigo kubwa sana kwa Ummah wa Kiislamu
 

Attachments

  • Screenshot_20250710-044052_WhatsApp.jpg
    Screenshot_20250710-044052_WhatsApp.jpg
    189.4 KB · Views: 14
  • Screenshot_20250710-044059_WhatsApp.jpg
    Screenshot_20250710-044059_WhatsApp.jpg
    393.8 KB · Views: 16
  • Screenshot_20250710-044106_WhatsApp.jpg
    Screenshot_20250710-044106_WhatsApp.jpg
    343.3 KB · Views: 15
  • Screenshot_20250710-044114_WhatsApp.jpg
    Screenshot_20250710-044114_WhatsApp.jpg
    364 KB · Views: 12
Ukumbusho msimu wa dhulhijja umeingia tuwe tayari kufunga masiku 9 haya na kufanya ibada kwa wingi katika jumla yake masiku haya 10
 
Waislamu tumeingia mwezi 9 dhul hijja ni siku iliyotiliwa mkazo sana kufunga kwa aliekua hajaenda hijja

Funga ya kesho ukiifunga na kukubaliwa basi Mja husamehewa madhambi ya mwaka ulopita na ujao unakosaje fursa hii ewe muislamu?

Ndugu zangu wapendwa, kesho ni siku tukufu ya Arafa siku yenye rehema, maghfira na kujibiwa dua. Tusiiache ipite kama siku ya kawaida.tuzidisheni
kumtaja Allah (dhikr), kuomba msamaha (istighfar), kumswalia Mtume ﷺ,
na kuomba dua kwa ajili yetuu, familia zetu na Ummah mzima.

Siku ya Arafa ni miongoni mwa siku bora zaidi za dua. Tumnyenyekee Mola wetu, kwani huenda dua ya siku hiyo ikawa sababu ya kufunguliwa kheri zetu kuondolewa huzuni zetu, au kusamehewa madhambi yetu.

Usiseme sina la kuomba… mwombe Allah kila kilichomo moyoni mwako.
Hakuna dua ndogo mbele ya Allah, na hakuna jambo gumu kwake.
 
Inapoingia Alfajiri ya Siku ya ‘Arafah, inapasa kutamka kwa wingi maneno yafuatayo ambayo ni maneno bora kabisa aliyoyatamka Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pamoja na Manabii kabla yake kama alivyosema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

((خَيْرُ الدُّعَاءِ دُعَاءُ يَوْمِ عَرَفَةَ، وخَيْرُ مَا قُلْتُ أنَا وَالنَّبيُّونَ مِنْ قَبْـلِي: لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيْكَ لَهُ، لَهُ الـمُلْكُ، ولَهُ الـحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيءٍ قَدِير)) روى الترمذي
“Du’aa bora kabisa ni du’aa katika siku ya 'Arafah, na (maneno) yaliyo bora kabisa niliyosema mimi na Manabii kabla yangu ni:
لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيْكَ لَهُ، لَهُ الـمُلْكُ، ولَهُ الـحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيءٍ قَدِير
Laa Ilaaha illa Allaah Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku Walahul-Hamdu wa Huwa 'alaa kulli shay-in Qadiyr.

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, Pekee, Hana mshirika, Ufalme ni Wake, na Himdi zote ni Zake Naye juu ya kila kitu ni Muweza. [At-Tirmidhiy]
 
Ewe Muislamu usiiache fursa hii kwani hujui kama mwakani utaipata tena


Nb: Walosema watabadilika kesho leo wapo makaburini
 
Waislamu tupo katika masiku bora haya tujitahidi tufunge

Hakika ya swaumu iliyo bora baada ya Ramadhani ni swaumu katika mwezi huu wa muharram yani mfunguo 4
 

Attachments

  • Screenshot_20260623-194724_WhatsApp.jpg
    Screenshot_20260623-194724_WhatsApp.jpg
    153.5 KB · Views: 1
Back
Top Bottom