Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania NBC Premier League imeendelea tena leo kwa mchezo mmoja ambapo Mbeya City walikuwa wakiwakaribisha Azam FC kwenye Uwanja wa Sokoine.
Mchezo umekwisha kwa Mbeya City kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya Azam FC, ambapo wenyeji ndo walikuwa wa kwanza kutikisa nyavu za Azam FC kunako dakika ya 51' kupitia kwa Juma Shemvuni baada ya kutokea piga nikupige lango la Azam.
Mbeya City waliendelea kuliandama lango la Azam FC kwa mashambulizi zaidi, ambapo kwenye dakika ya 83' Azam FC walijifunga bao kwa mlinzi wake wa kati Daniel Amoah kumpoteza maboya golikipa wake Ahmed Salula, akimuacha akichumpa bila mafaniko.
Kuelekea kumalizika kwa mchezo huo, Azam FC walipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Ayoub Lyanga kwenye dakika ya 88' baada ya beki kufinywa na kuachia shuti kali lililogonga mwamba wa juu na kujaa wavuni.
Hadi mwisho wa mchezo Mbeya City mbili na Azam FC moja | FT: Mbeya City 2-1 Azam FC
Azam wanapoteza mchezo wa sita msimu huu kwenye Ligi Kuu Tanzania.
Je una maoni gani kuhusu mwenendo wa Azam FC msimu huu..?
Mchezo umekwisha kwa Mbeya City kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya Azam FC, ambapo wenyeji ndo walikuwa wa kwanza kutikisa nyavu za Azam FC kunako dakika ya 51' kupitia kwa Juma Shemvuni baada ya kutokea piga nikupige lango la Azam.
Mbeya City waliendelea kuliandama lango la Azam FC kwa mashambulizi zaidi, ambapo kwenye dakika ya 83' Azam FC walijifunga bao kwa mlinzi wake wa kati Daniel Amoah kumpoteza maboya golikipa wake Ahmed Salula, akimuacha akichumpa bila mafaniko.
Kuelekea kumalizika kwa mchezo huo, Azam FC walipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Ayoub Lyanga kwenye dakika ya 88' baada ya beki kufinywa na kuachia shuti kali lililogonga mwamba wa juu na kujaa wavuni.
Hadi mwisho wa mchezo Mbeya City mbili na Azam FC moja | FT: Mbeya City 2-1 Azam FC
Azam wanapoteza mchezo wa sita msimu huu kwenye Ligi Kuu Tanzania.
Je una maoni gani kuhusu mwenendo wa Azam FC msimu huu..?