Freeman Mbowe atimiza siku 90 mahabusu

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
141,436
Reaction score
283,720
Leo ni miezi mitatu kamili tangu kukamatwa kwenye masuala ya kongamano la Katiba Mpya na kurundikwa rumande kwa mwamba Mbowe, na baadaye kutengenezewa mashitaka ya kutunga ya ugaidi.

Miezi mitatu kwa kesi ya uongo ya ugaidi ya kutengenezwa na kingai si jambo jepesi, bali ukweli uko wazi kwamba katika dunia hii hakuna mahali popote pale ambapo shetani amewahi kumshinda mungu, ikumbukwe pia kwamba kila ubaya utalipwa.

 
View attachment 1978393

KATIKA DUNIA HII HAKUNA MAHALI POPOTE PALE AMBAPO SHETANI AMEWAHI KUMSHINDA MUNGU , Ikumbukwe pia kwamba KILA UBAYA UTALIPWA .
Sasa Erythrocyte ikitokea Mbowe akahukumiwa kwa kesi hizo.. Ni nani atakaekuwa kamshinda mwenzake kati ya Mungu na shetani? Maana katika uchaguzi mkuu tuliaminishwa hivi hivi matokea yake mshindi akapatikana upande ule ulioonekana kuwa sio wa Mungu. Sasa swali lingine ni Mungu gani anaeshindwa na kiumbe alichokiumba mwenyewe (shetani)? Au huyu Mungu mnaesemaga kuwa hashindwi na shetani na baadae anashindwa sio yule Mungu halisi tunaemjua kupitia utukufu wake?
 
Hawakushinda bali walijitangaza
 
To highlight this matter is a good move. You must highlight it repeatedly.
Mkuu pole kwa kifungo cha sabaya , ndio basi tena , zile bia mlizopora zitawatokea puani , tumeanza kusaka mmoja mmoja , kwenye orodha umo
 
Si alikuwa analilia maridhiano na chamatawala.
Hayo ndiyo majibu ya maridhiano yenyewe.
Aendelee kuomba maridhiano huko aliko.
Malipo ni hapahapa.
 


Pole kwa Lilian na watoto wake
 
Kesi ni kesi tu hakuna ya uwongo Wala ya ukweli mpaka Mahakama itakapotoa hukumu.

Huyo muache tu akae huko, nchi iko salama bila kelele zake. Na akitoka atakuwa kajifunza kitu
 
Mungu amjalie moyo wa uvumilivu na uhimilivu. Amina
 
Kesi ni kesi tu hakuna ya uwongo Wala ya ukweli mpaka Mahakama itakapotoa hukumu.

Huyo muache tu akae huko, nchi iko salama bila kelele zake. Na akitoka atakuwa kajifunza kitu
Kama alivyojifunza Jiwe na Sabaya🤣🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…