Abel Ndundulu
JF-Expert Member
- Sep 17, 2015
- 847
- 389
Naomba kuwafahamisha yafuatayo wana mabadiliko wenzangu wa vyama vya UKAWA!!!! na Wafuasi wa Comrade LOWASSA!!!
Yumkini katika siku zilizobaki tukaendelea kupata misukosuko mingi ndani ya umoja wa vyama vyetu UKAWA na ndani ya vyama vyetu vya NCCR,CHADEMA,NLD na CUF na katika majimbo yetu na sisi wafuasi mmoja mmoja. Ninashauri yafuatayo:
1. Kutokukatishwa tamaa na kauli,matamko,matangazo,vipande vya hotuba za Nyerere ama maneno yeyote ya kutuvunja nguvu sisi wana "mabadiliko" yaliyoratibiwa vyema na yatakayotolewa na watu wa kada mbalimbali ndani ya Chama na Serikali kama Mwinyi,Mkapa,Mama Maria Nyerere,n.k,
2. Katika kipindi hiki Matamko,Matamasha,Maandamano feki na message nyingi za kizushi katika simu zetu zitaibuka kukipa kiki Chama Cha Magufuli,naomba tuendeleze msimamo wetu,wala tusiyumbe.Lowassa Chaguo letu.
3. Vitatolewa vitisho mbalimbali kwa watu binafsi,familia,makundi na Taasisi zinazounga mkono UKAWA na MABADILIKO kwa ujumla,TUSIOGOPE,USHINDI UNAKUJA!
4. Wapo baadhi ya Viongozi wa vyama vyetu watakaonunuliwa ili kudhoofisha upinzani na Mabadiliko..USIRUDI NYUMA.USHINDI NI LAZIMA!!
5. Vyombo mbalimbali vya habari kama magazeti,luninga na blogs zitaelekeza nguvu kwa Chama Cha Magufuli kwa sababu ya nguvu ya fedha zinazotokana na uuzwaji wa hisa za TBL,NMB na fedha zingine zetu wavuja jasho..MSIKONDE SISI TUNA NGUVU YA UMMA.
6. Mipango mbalimbali endelevu ya kuvunja nguvu yaMabadiliko itawekwa kwetu kwa kuwa wao wana fedha za kodi zetu sisi Wapumbavu,malofa,mbumbumbu na Kunguni ambao tuna nguvu ya Umma TUSIJALI!!
7. Usiku wa kuamkia siku ya kupiga kura pamoja na siku yenyewe ya kupiga kura kutakuwa na hujuma za nishati,mitandao ya simu na internet,vyombo mbalimbali vya habari pamoja na mambo lukuki,USIJALI NA WALA USIRUDI NYUMA!!
MUHIMU: Mshike mwenzako Mkono, usimwache atutoke,vumilia yote hayo kwa kuwa;
Giza likizidi ujue nuru imekaribia
Huwezi kula mua bila kukuta fundo
Ugumu ukizidi,unafuu umekaribia
"Hata dhahabu ili iitwe dhahabu ni lazima ipitekatika moto
CHAGUA RAIS WA CHADEMA (LOWASSA),..CHAGUA VYAMA VYA UKAWA (CHADEMA,CUF,NCCR NA NLD KWA MABADILIKO YA MAISHA YAKO NA WANAO)
Yumkini katika siku zilizobaki tukaendelea kupata misukosuko mingi ndani ya umoja wa vyama vyetu UKAWA na ndani ya vyama vyetu vya NCCR,CHADEMA,NLD na CUF na katika majimbo yetu na sisi wafuasi mmoja mmoja. Ninashauri yafuatayo:
1. Kutokukatishwa tamaa na kauli,matamko,matangazo,vipande vya hotuba za Nyerere ama maneno yeyote ya kutuvunja nguvu sisi wana "mabadiliko" yaliyoratibiwa vyema na yatakayotolewa na watu wa kada mbalimbali ndani ya Chama na Serikali kama Mwinyi,Mkapa,Mama Maria Nyerere,n.k,
2. Katika kipindi hiki Matamko,Matamasha,Maandamano feki na message nyingi za kizushi katika simu zetu zitaibuka kukipa kiki Chama Cha Magufuli,naomba tuendeleze msimamo wetu,wala tusiyumbe.Lowassa Chaguo letu.
3. Vitatolewa vitisho mbalimbali kwa watu binafsi,familia,makundi na Taasisi zinazounga mkono UKAWA na MABADILIKO kwa ujumla,TUSIOGOPE,USHINDI UNAKUJA!
4. Wapo baadhi ya Viongozi wa vyama vyetu watakaonunuliwa ili kudhoofisha upinzani na Mabadiliko..USIRUDI NYUMA.USHINDI NI LAZIMA!!
5. Vyombo mbalimbali vya habari kama magazeti,luninga na blogs zitaelekeza nguvu kwa Chama Cha Magufuli kwa sababu ya nguvu ya fedha zinazotokana na uuzwaji wa hisa za TBL,NMB na fedha zingine zetu wavuja jasho..MSIKONDE SISI TUNA NGUVU YA UMMA.
6. Mipango mbalimbali endelevu ya kuvunja nguvu yaMabadiliko itawekwa kwetu kwa kuwa wao wana fedha za kodi zetu sisi Wapumbavu,malofa,mbumbumbu na Kunguni ambao tuna nguvu ya Umma TUSIJALI!!
7. Usiku wa kuamkia siku ya kupiga kura pamoja na siku yenyewe ya kupiga kura kutakuwa na hujuma za nishati,mitandao ya simu na internet,vyombo mbalimbali vya habari pamoja na mambo lukuki,USIJALI NA WALA USIRUDI NYUMA!!
MUHIMU: Mshike mwenzako Mkono, usimwache atutoke,vumilia yote hayo kwa kuwa;
Giza likizidi ujue nuru imekaribia
Huwezi kula mua bila kukuta fundo
Ugumu ukizidi,unafuu umekaribia
"Hata dhahabu ili iitwe dhahabu ni lazima ipitekatika moto
CHAGUA RAIS WA CHADEMA (LOWASSA),..CHAGUA VYAMA VYA UKAWA (CHADEMA,CUF,NCCR NA NLD KWA MABADILIKO YA MAISHA YAKO NA WANAO)