Forbes yachafua hali ya hewa Lumumba!

Forbes yachafua hali ya hewa Lumumba!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Suala la Forbes limewatofautisha viongozi waandamizi wa CCM na kupelekea mkutano na waandishi wa habari kuahirishwa. Mkutano huo na waandishi wa habari ulilenga kutoa uchambuzi wa kiindi cha waka mmoja wa Serikali ya Awamu ya tano iliyo chini ya Rais Dr. John P. Magufuli. Ilipangwa kusifu kila idara na kuwaomba wananchi wamuunge mkono Rais Magufuli.

Nyaraka za mkutano huo na waandishi wa habari zinaonesha kuwa CCM imeuchambua mwaka huo na kwa ujumla, kumemiminwa sifa za kutosha na kutisha. Pia, CCM ilipanga kugusia mwenendo wa chama kwa ujumla kwa kudurusu kesi mbalimbali za uchaguzi zilizopo mahakamani kwa sasa na hata Uchaguzi wa Meya wa Kinondoni na Ubungo.

CCM pia ililenga kuzungumzia 'kuongoza' kwa Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dr. Magufuli kwenye shindano la 'Mtu Mahiri Afrika wa mwaka 2016' linalosemekana kuendeshwa na Forbes. Suala hilo limewagawa viongozi waandamizi chamani hapa Ofisi Ndogo za Lumumba na kupelekea kuchafuka kwa hali ya hewa kwa muda. Suluhisho lilikuwa ni kuahirisha Mkutano na waandishi wa habari.

Eti mambo ya mitandao inaahirisha Press Conference! PC ni kesho saa tano asubuhi hapa hapa Lumumba!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam!
 
Mtu mashuhuri Rais wa nchi anashindanishwa na watu wasio na nyadhifa wala majina makubwa.Ilikuwa njia ya kutuondoa kwenye mjadala mkubwa wa Mheshimiwa anaetumia majina ya wizi.
 
186a3a64953593c76cf0fa675dd51205.jpg
 
Ndiyo uzuri wako tupa tupa coz you usually hit to the point and you know to sort out the cue words
 
Hao watu bado tuu wanajipendekeza kwa Magu ili wapete hata cheo chochote.....!!
 
Suala la Forbes limewatofautisha viongozi waandamizi wa CCM na kupelekea mkutano na waandishi wa habari kuahirishwa. Mkutano huo na waandishi wa habari ulilenga kutoa uchambuzi wa kiindi cha waka mmoja wa Serikali ya Awamu ya tano iliyo chini ya Rais Dr. John P. Magufuli. Ilipangwa kusifu kila idara na kuwaomba wananchi wamuunge mkono Rais Magufuli.

Nyaraka za mkutano huo na waandishi wa habari zinaonesha kuwa CCM imeuchambua mwaka huo na kwa ujumla, kumemiminwa sifa za kutosha na kutisha. Pia, CCM ilipanga kugusia mwenendo wa chama kwa ujumla kwa kudurusu kesi mbalimbali za uchaguzi zilizopo mahakamani kwa sasa na hata Uchaguzi wa Meya wa Kinondoni na Ubungo.

CCM pia ililenga kuzungumzia 'kuongoza' kwa Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dr. Magufuli kwenye shindano la 'Mtu Mahiri Afrika wa mwaka 2016' linalosemekana kuendeshwa na Forbes. Suala hilo limewagawa viongozi waandamizi chamani hapa Ofisi Ndogo za Lumumba na kupelekea kuchafuka kwa hali ya hewa kwa muda. Suluhisho lilikuwa ni kuahirisha Mkutano na waandishi wa habari.

Eti mambo ya mitandao inaahirisha Press Conference! PC ni kesho saa tano asubuhi hapa hapa Lumumba!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam!
Mzee Tupatupa wa Ufipa katika ubora wako.
 
VUTA-NKUVUTE
ina maana nyie hapo lumumba ni kusifu tu hamna hata kushauri serikali ni wap ielekeze nguvu kama livyokuwa wakati wa mwalimu chama kushauri serikali na sio kila kitu kusifu tu?
 
Hehehe... Tungejua tungewaacha waropoke kwanza
 
Back
Top Bottom