Foolmoon in Taurus. Leo usikose kufanya ibada hii

Foolmoon in Taurus. Leo usikose kufanya ibada hii

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
2,144
Reaction score
3,459
FOOLMOON IN TAURUS
Leo usikose kufanya ibada hii,
IMG-20251006-WA0823.jpg


Mwezi Mkubwa (Supermoon) unakaribia.

Jiandaeni.

kuanzia leo tarehe 5/11, Mwezi Mkubwa utawasili utakuwa mwezi wa duara mkubwa na wenye mwanga zaidi wa mwaka kwa sababu utakuwa karibu zaidi na dunia, ukiwa mkubwa kwa hadi asilimia 14% na mkali kwa hadi asilimia 30% zaidi ya mwezi wa kawaida. Tayari tunaanza kuhisi nguvu zake zikijikusanya. Baadhi watauita “Beaver Moon.”

Mwezi huu utaleta mvutano kati ya kutaka kushikilia usalama na kukubali mabadiliko, hasa kwa kuwa utakuwa na uhusiano wa mvutano na sayari za Jupiter na Pluto hali itakayowasukuma watu katika matamanio ya kupitiliza, kutaka kujumuika na kufurahia maisha, lakini pia inaweza kusababisha mabadiliko makubwa katika mahusiano mengine ya muda mfupi, na mengine yakibadilisha kabisa uhusiano hadi yasirekebishike tena.

Siku chache zijazo zitakuwa na mchanganyiko wa utulivu na msisimko. Wakati nguvu ya “faraja” inapogongana na nguvu ya “mabadiliko,” kunazuka mvutano nyumbani, kazini, au hata kwenye makundi ya kijamii. Watu wanaweza kujikuta wakijitumbukiza katika matendo ya kupitiliza ili kujifariji kama kutumia pesa hovyo, kula au kunywa kupita kiasi, au kutafuta starehe za haraka kisha baadaye kujikuta wakiwa wamechoka au wamevurugwa kihisia.

Hivyo basi, huu ni wakati wa kujizuia na kujitawala kihisia.
Usifanye jambo lolote wiki hii ambalo utalijutia kesho.
Kaa mtulivu au ondoka kwa amani.

Nguvu za mamlaka na udhibiti zitaanzag kuonekana wazi iwe ni kwa ushindani kati ya marafiki, migongano ya nguvu katika uhusiano, au malalamiko yaliyofichwa ambayo sasa yako tayari kulipuka kwa kisingizio kidogo tu. Kile kinachoanza kama mazungumzo ya kirafiki kinaweza haraka kubadilika kuwa jaribio la mipaka, hasa wakati vivuli vilivyofichwa vya kihisia vinapoibuka ghafla.

Kwa hiyo, kuwa mwangalifu usiahidi kupita uwezo wako, usitumie pesa hovyo, wala usilazimishe watu wakidhi mahitaji yako ya kihisia.
Epuka jaribu la kutaka kudhibiti matokeo au kutumia mvuto wako kuficha ukweli mgumu.

Kihisia na kisaikolojia, miezi mikubwa kama hii huamsha hisia kwa kiwango kikubwa wengi watasumbuliwa na kukosa usingizi na ndoto zenye nguvu.

Lakini upande chanya ni kwamba mwanga huu wa mwezi unaweza kufungua ubunifu wa ajabu, nguvu za kiroho, na uwezo wa kiintuisho (intuition). Hata hivyo, ni ukweli kwamba kwa wengi, hii itakuwa wiki yenye nguvu nzito sana.

Kumbuka, ulimwengu mzima kwa sasa unapitia mabadiliko makubwa, hata katika miili ya watu kimwili.

Kwa wale wanaopitia changamoto za kiakili au kihisia, tafuta msaada usiwe peke yako. Na kwa wote wanaohisi nishati ni nzito sana wiki hii kumbuka, kuna mwanga mwishoni mwa handaki.
Hii ni kipindi kifupi tu.
Kivumilie. Kwa upendo.

Aliyeonywa mapema, amejiandaa.


Dr DOGOLI ✍🏻
 
Waisrael wa kweli (African) walichukuliwa utumwani sana wakasambazwa karibu dunia nzima kwa sababu Mungu wao aliwaacha, Mungu aliwaacha kwa sababu walianza kuabudu masanamu

Mwezi na nyota ni masanamu ya waarabu, elimu ya unajimu pia

Wazungu waliabudu Jua, utashangaa kuona waisrael wa kweli (waafrika) nao leo hii wanahangaika kupiga picha za sunset ilihali hawajui wanachokifanya ni kufuru

Acha kufundisha watu kuabudu masanamu
 
Waisrael wa kweli (African) walichukuliwa utumwani sana wakasambazwa karibu dunia nzima kwa sababu Mungu wao aliwaacha, Mungu aliwaacha kwa sababu walianza kuabudu masanamu

Mwezi na nyota ni masanamu ya waarabu, elimu ya unajimu pia

Wazungu waliabudu Jua, utashangaa kuona waisrael wa kweli (waafrika) nao leo hii wanahangaika kupiga picha za sunset ilihali hawajui wanachokifanya ni kufuru

Acha kufundisha watu kuabudu masanamu
Umeandika ufira ngoto tupu mkuu kama uwez kuijua universe power na spiritual zake n heri ufunge ilo kombe lako na maziwa ya mgando
 
Kaka mchawi kumbe hawakupita na wewe ,nafurahia kujua hivyo bwana maana sisi huku kiliwaka mpaka waliofukuzwa walirudishwa kambini
Nipo jombi,nilikuja na usafir wangu maalum nikaona hali ya hewa nzito Moshi mwingi Sion vizuri mbele nikala Kona chombo ikalud kwa hewa nikalud zangu uchawin so nipo shwali kabisa 😂😂
 
Back
Top Bottom