fomu ya kuomba kazi

Viol

JF-Expert Member
Dec 15, 2009
25,426
18,231
Jina: Ousofia

Jinsia: ya kiume halafu namtafuta mrembo atayenifaa

Cheo unayotaka: Rais au makamu wa kampuni,ila sipendekezi sana hizo nafasi mpaka mtakaponiajiri kwanza.

Kiasi cha mshahara unaotaka:isipungue 185,000000/= kwa mwezi ila mnisaidie pia

Elimu:ndiyo

Ujuzi wako wa ziada:Nakumbuka nilipokuwa shule ya msingi niliibiwa kalamu ila nilimkamata mwizi wangu.pia ujuzi wangu unabadilika kutokana na mazingira.

Ulishawahi kuajiriwa kwingine?: ndiyo

kwanini ukaacha hiyo ajira:ah uzinguzi

Muda utakaofanya kazi: wowote

Andika mawasiano ya mwajiri wako wa kwanza:kama yupo kwanini niombe kazi

Je kuna matatizo ya kiafya ambayo yangekuzuia usibebe kilogram isiyopumgua 5?:Kilogram za nini?

Una gari: nadhani swali la msingi hapa ingekuwa naendesha gari kwa speed gani

Unavuta sigara:kazini hapana nyumbani kama kawaida

Kwa hiyo miaka 5 ya ajira hapa Dar es salaam ungependa uishi wapi:napenda kuishi arusha na mwanza

Umehakikisha hayo yote uliyoyasema hapo juu ni kweli?: sijadanganya
 
mh kweli kwa hapa ndo nimeamini OUSOFIA kilaza km thread zake.....hahahahaaa natania
 
Nimependa hiyo sehemu ya kuishi Mwanza kufanya kazi Dar. Ningekuwa mimi ningeomba niishi Mbeya.
 
Back
Top Bottom