Filamu: Mwili wa mwanamke aliyekufa kwa sumu, umepotea Mochwari

SteveMollel

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
8,660
24,676
Utafanya nini kama umefiwa, umeupeleka mwili wa mpendwa wako kuhifadhiwa alafu unapigiwa simu kwamba mwili hauonekani? Umepotea? Haujulikani ulipo?

Tafuta popcorn, ambaa na kisa hiki..

Baada ya kutokea ajali, mlinzi wa hospitali akigongwa na gari mita kadhaa kutoka eneo lake la kazi, inspekta wa polisi aitwaye Jaime anaitikia wito wa kuja kufanya upelelezi wa kesi hii yenye utata.

Anapofika hospitali anabaini mambo mawili, moja - mlinzi alidakwa na kamera akiwa anakimbia kwa papara kutoka eneo lake la kazi, mochwari, huku kinachomkimbiza hakionekani.

Na kukimbia huko ndo' kukampelekea aingie barabarani alipogongwa vibaya kiasi cha kulazwa akiwa hana fahamu mpaka sasa.

Pili - mochwari alipotokea mlinzi huyo kuna mwili wa mwanamke hauonekani, haijulikani mwili huo umeelekea wapi na ni nani aliyeuchukua!


Inspekta anakuna kichwa.

Kuna mahusiano gani kwenye matukio haya mawili? - Kupotea kwa maiti ya mwanamke na ajali mbaya ya mlinzi?

Anataka kujua vema, mwanamke huyu ambaye mwili wake umepotea ni nani.


Anapewa taarifa jina lake ni Mayka, mwanamke wa makamo, mfanyabiashara tajiri ambaye kifo chake kilisababishwa na mshtuko wa moyo.

Mwanamke huyu aliolewa na kijana mdogo kiumri jina lake Alex Ulloa, bwana mmoja anayefundisha huko chuoni, na mwili wake hapa mochwari ulikuwa unangojea kufanyiwa uchunguzi wa kisayansi kubaini ukweli juu ya kifo chake (Autopsy).

Kupata maelezo hayo, inspekta akawa amempata mtuhumiwa wake kwanza kichwani, si mwingine bali Alex Ulloa.


Bwana huyo alipewa taarifa ya kupotea kwa mwili wa mkewe, akafika hospitalini upesi akiwa na bumbuwazi. Ni yeye ndo' aliuleta mwili huu hapa, tena baada ya kuhakikisha kwamba Mayka kafariki, sasa kimetokea nini?

Alex anatoa maelezo na inspekta anamshuku huenda bwana huyu alimuua mkewe kwa sumu kisha akautorosha mwili wake kuepusha uchunguzi.

Lakini huu ndo' ukweli?

HAPANA.

Ni kweli enzi za uhai wake, Mayka alikuwa anampenda sana Alex kiasi cha kufunga naye ndoa pasipo kujali umri wake mkubwa lakini kiuhalisia, kwa Alex hali ilikua tofauti.


Yeye alimpenda huyu 'mshangazi' kwasababu ya pesa tu, na si vinginevyo.

Siku moja Alex akiwa kazini, anakutana na mwanamke anayetokea kumpenda sana, mwanamke kijana kama yeye, aitwaye Carla.

Wanatengeneza mahusiano mazito kiasi kwamba Alex anaanza kupwaya kwa 'mshangazi' wake. Si unajua tena ya mshika mawili?

Na hivi michepuko walivyo na sifa sasa, anazikamua zote, Alex akifika kwa mshangazi hana hata tone. Dhoofu bin taaban!

Mayka akaanza kuhisi kuna mtu anampokonya tonge lake.

Upande wa pili, mchepuko nao ukaanza kutingisha kiberiti - hautaki tena kushea, anaitaka hii tamu iwe yake peke yake.

Sasa Alex anakuwa njia panda.

Bado pesa za mshangazi anazitaka, na raha za mchepuko ndo' usiseme.

Ili apate vyote, anaamua kummaliza 'le mshangaz' kwa kumwekea sumu ya kumuua taratibu ili afe abakiwe na mali na huku pia aendelee na penzi la Carla.

Anafanikiwa vema.

Mayka anakunywa wine yenye sumu na kufariki dunia baada ya siku kadhaa kama vile ilivyopangwa.

Alex anampa taarifa Carla kwamba zoezi limekamilika. Mwili wa Mayka upo mochwari, hauna pumzi tena, na sasa wapo free kula mema ya nchi.


Kwahiyo ni kweli isiyo na shaka, Alex kamuua Mayka. Lakini si kweli kwamba Alex amehusika na kuuchukua mwili wa Mayka mochwari!

Sasa mwili uko wapi?

Mhusika ni nani?

Mara kidogo, mlinzi anapata unafuu wa angalau kuweza kuongea.

Swali la kwanza, ni aliona nini siku ile mpaka akakimbia?

Katazame 'El Cuerpo' (The Body).
 

Attachments

  • e343bb2882b0c1245f9660fd12c3f12f.png
    148.2 KB · Views: 12
UNAAMKA KABURINI, UMEZUNGUKWA NA MAITI NA HAUKUMBUKI KITU. UNAFANYA NINI?


Mwanaume mmoja anaamka katikati ya giza. Hajui yuko wapi. Mwili wake una maumivu na huku kichwani hamna anachokumbuka.

Anajipekua mfukoni mwake na kubaini kuna funguo na kiberiti cha gesi. Anawasha kiberiti aangaze mazingira. Anagundua yuko ndani ya shimo kubwa na amezingirwa na maiti lukuki!


Anashtuka.

Anatazama juu, anamwona mwanamke mmoja akiwa amesimama kando ya shimo. Anaomba msaada na mwanamke huyo anamtupia kamba.


Mwanaume huyo anatoka kaburini na kwenda moja kwa moja kwenye nyumba fulani ambamo humo ndani anakuta watu watano; mwanamke mchina alomsaidia pamoja na watu wengine wanne.

Kati yao wanaume ni watatu na mwanamke ni mmoja. Wote hawa hamna anayekumbuka kitu isipokuwa mwanamke yule mchina, na mwanamke huyo ni bubu, hawezi kuongea.

Sasa watu hawa wanashukiana maana haijulikani nani ni rafiki na nani ni adui, achilia mbali hawajui wamefikaje hapa.

Lakini mashaka makubwa yapo kwa bwana huyu alotoka kaburini, kwanini yeye amezindukia huko na ingali wenzake wameamkia ndani?

Je, huyu sio muuaji?


Muda kidogo watu wale wengine wanapata vitambulisho vyao vya leseni na kufahamu majina yao; Luka, Michael, Nathan na Sharon, ila huyu alotoka kaburini yeye bado hajulikani.

Pia yule mwanamke mchina, hamna anayemfahamu ingali wote hawa wameamka na kumkuta hapa.

Wanakagua humu ndani na bwana yule alotoka kaburini anabaini kuna kalenda iliyozungushiwa tarehe 8, yani siku mbili zijazo, lakini haijulikani siku hiyo kuna kitu gani haswa.

Wanapata mashaka.

Anaulizwa mwanamke mchina lakini atasema nini na yeye kuongea hawezi?

Baadae kidogo, mwanamke huyo mchina akiwa amebebelea taa, anakimbilia msituni pasipo kuaga.

Upesi wanamfuatilia anapoelekea na huko porini wanaona miili ya watu waliokufa ikiwa imefungiwa kwenye miti.

Hawaelewi watu hao ni kina nani na kwanini wamefungiwa hapo.

Wanamkuta mchina kwenye kijumba fulani akiwa anamlisha chakula mwanamke mmoja aliyefungwa mikono.

Mwanamke huyo anapomwona mwanaume yule alotoka kaburini, anapandwa na hasira kali akitaka kumshambulia.

Hali inakuwa tete.

Mwanamke huyo anatulizwa na kitako cha bunduki, anazirai. Lakini hii inazidi kuongeza maswali juu ya bwana huyu wa kaburini.

Ni nani haswa?

Panapokucha, wanatoka kwenda kuangaza huko nje kutafuta magari kwa maana funguo wameamka nazo mifukoni. Nyumbani anabaki Michael na mwanamke mchina tu.

Huko porini, wanapata kuyaona magari kadhaa yakiwa yamefunikwa. Ndani ya gari moja, wanaipata picha waliyopiga wote kwa pamoja lakini haina sura ya bwana yule wa kaburini.

Yeye bado ni kitendawili..


Wanacheki magari hayo na kubaini hayana mafuta ya kutosha. Kidogo wanakumbana na mwanamke mchina akiwa anakimbia kwa hofu. Wanamfuata mwanamke huyo na kufika eneo wanalomkuta Michael akiwa anajifia, ameshambuliwa na bwana mmoja alokuwa anajaribu kumsaidia.

Bwana huyo ni kama zombi mwenye kiu ya damu.

Wanammaliza kwa risasi kisha yule bwana alotoka kaburini akiwa pamoja na Sharon wanarudi kwenye yale magari kuchukua mojawapo ili watafute sehemu ya mafuta au magari yenye mafuta ya kutosha waondoke eneo hili.

Wanafika eneo fulani lenye jengo kubwa, wanatazama ndani na kumwona mtoto wa kiume. Wanamwomba afungue geti lakini ajabu mtoto anashikwa na woga mkubwa anapomwona mwanaume yule alotoka kaburini!

Anamwita mwanaume huyo kwa jina la Jonah lakini hataki kabisa kumfungulia.

Sasa Jonah ni nani?


Walau mwanaume huyu amejua jina lake, lakini kwanini watu wanaokutana naye wanamwogopa kiasi hiki?

Anataka kujua zaidi yeye ni nani na mtoto huyu anaonekana kujua. Analazimisha kuingia ndani kwa kutumia bunduki, Sharon anamsihi asitumie nguvu kubwa na bahati mbaya mtoto anatoroka asijulikane ameelekea wapi.

Wanasonga mbele kidogo, wanakutana na watu wanaokata miti kwa shoka. Jonah anajaribu kuwapazia sauti ili wapate msaada lakini watu hao kumwona Jonah, wote wanacharuka na kuanza kuwakimbiza kama wendawazimu!


Wanafanikiwa kutoroka lakini wanapofika nyumbani wanamkuta Luka akiwa ameshikilia bunduki anawangojea.

Luka sasa anajua huyu Jonah ni nani kwani alikumbana na kamera yenye video ya zamani, humo akaona yale ambayo Jonah alipata kuyafanya.

Kwahiyo Jonah anaposhuka tu kwenye gari anamnyooshea mdomo wa bunduki kisha anamwambia Sharon akae mbali na bwana huyo kwani ni hatari.

Kafanya nini?

Nini haswa kinaendelea hapa?

Kesho yake ni ile tarehe nane ya kwenye kalenda, kuna tukio gani?

Tazama "OPEN GRAVE"
 
Ipo netnaija..?
 
Nimeenda NetNaija sijaona hii the body hata sijui naipakua kwenye site ipi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…