Fikiri kuhusu vijana wa leo

Fikiri kuhusu vijana wa leo

o_2

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2017
Posts
431
Reaction score
388
Shwari?

Wakati tunazaliwa miaka ya 90s kulikuwa na wale mabro ambao wapo na harakati zao za kupiga mishe mishe wapate hela familia zao zipate kula. Mabro wa ukoo, mabroo wa familia kila mtoto alikuwa anatamani kuwa kama kaka yake.

Mabro walikuwa wanafanya juu chini, chochote wakiwezacho ili ile riziki basi waweze kuipata. Hakujalisha kama ilikuwa ni halali ama la. Na Mama zao, familia zao zilikuwa zinawaombea ili basi hustle zao ziwe na mafanikio.

Mabro waliokuwa wanasoma, waliokuwa wanafanya vizuri darasani basi wadogo zao ndio tulikuwa tunawaangalia.

Natamani niwe kama blaza. Bro kaenda shule ya kipaji sekondari. Kijiji kizima anafahamika. Na wewe unatamani kuwa kama bro. Bro kaenda UDSM kasoma education bumu asilimia zote, kamaliza chuo kazi inamsubiria kapata, maisha yanaendelea.

Zama zimebadilika. Role models wengi tumewapoteza kwenye bangi na unga. Vyuoni wamejaa tele na ajira hakuna. Bahati nzuri wazazi wetu hawataki tuwe wabunifu kufanya yale tunayoyataka. Wazazi wanataka tusome lakini tufanikiwe kama mabro miaka hiyo.

Siku hizi vijana tulio wengi tumewekeza maisha yetu kwenye mitandao. Hatuna kazi za maana tupo tupo na mambo ya betting na kupiga story za mipira vijiweni. Dira ya vijana inapotea.

Tumepotea vibaya. Tumesoma tunashindwa kujiajiri. Tumekuwa tegemezi. Sio marole models tena miaka 30 bado haujaanza chochote. Hauna chochote cha kujishughulisha nacho na bado una matumaini ya kuwa na maisha mazuri. Miaka 60 ijayo nchi hii itakuwa nchi ya hovyo kuwatokea.

Vijana wa leo tumejaa stress na hamu za kujiua kila mahali. Tusipoweza kujikomboa sisi wenyewe hakuna atakayeweza.

Vijana wa leo majanga, hao vijana wa kesho sijui itakuaje.

Tuishi.
 
Enzi zinaenda mbio sana.
1670805864482.jpg
 
Kwahiyo unatakaje yan!?
Wewe unadhan nini kifanyike kama kusoma mmesoma ila kijiajiri hamuwezi!!.

Na hatuwezi au hatutaki?? Full kuchagua cha gua shughul za kufanya...Aibuu zimetujaaaaa tunaona soo hata kwe ye mambo yanabeba mustakabali wetu wenyewe eti kisa tuuu watu watatuochukuliaje!.
Vijana tuache upumbavu..tunataka kuwa smart muda wooote kaz kufanya tunaona aibu
 
Tatizo watu wanazaliana tunajazana alafu cha kutulisha hakuna... Tunabaki kuishi kwa majungu.
 
Ila betting hazikuwepo na enzi hiyo ukifika form 4 una maisha kuanzia ukarani kwenye vyama vya ushirika na kwenye ualimu..yaani ukifika chuo tu hata kama umesoma Bachelor of Arts in music wewe ni bosi mkubwa..
 
Kinachofuata ni kutokuwa na uzalendo ,Hao wazee waliopo wanawanyima fursa vijana soon wanazeeka na kupotea na kutuachia nchi sisi vijana wa hovyo ambao uzalendo umeshakwisha .....

Ni mwendo wa kuiba mali za umma pindi unapopata nafasi ,chota mihela tembea ,chota mihela sepaaaahakuna sijui nchi yangu kudadekiii
 
  • Thanks
Reactions: o_2
Role model wenu siku hizi ni machawa,wakata mauno,wadangaji
Enzi zetu role model wetu walikuwa mabaharia,wapiganaji nk

Ova
 
  • Thanks
Reactions: o_2
Sababu inayofanya vijana wengi waangukie kwenye anasa, ni kuyaishi maisha ya kufikirika.

Kupenda kazi za aina moja, unakuta Kila mmoja anataka kazi ya kutumia computer, yaani hawataki kabisa kukimbilia shambani, utakuta vijistudio vingi mitaani, music production uchwara, kuuza CD, sijui kuingiza nyimbo kwa flash, akijitahidi sana kafungua kijisaloon mtaani, Hadi unashangaa hili frem analipaje, Kodi alikopanga je? vipi kuhusu mahitaji mengine.


Pia unaweza kukuta vijana wapo vijiweni wanapiga stori za magari makali, Mara BMW mara sijui Alphard, yaani mtu anazungumza vitu vya million hamsini huko ikiwa laki tano hajawahi kushika.mara sijui nani ana hela kumzidi nani, yaani dah

Viwanja vya bata, unakuta kijana analeta maisha ya maigizo kuingia kumbi kubwa za starehe wakati Hana uwezo huo, kinachofuata ni kujiingiza kwenye utapeli na wizi ili aendane na maisha anayolazimisha.

Kutamani warembo wakali
Hapa napo Kuna tatizo kubwa sana, hasa ukizingatia mambo ya mitandao,kijana anajukuta anatamani mwanamke ambaye si saizi yake kabisa kuanzia muonekano, Elimu, ushawishi na hata umri, mwisho wa siku badala ya kutongoza , anatongozwa yeye na jimama, huku akipewa vizawadi vidogovidogo kama simu, cheni na vijinguo vya kubana, na akimakizwa kabisa atapewa Subaru, IST sijui Brevis
Hivyo kijana kama huyu huwezi kumfanyisha kazi za kufyatua matofali, saidia fundi, na vinginevyo.

Shida inakuja akiachwa ndiyo anaangukia kwenye ulevi, unga na vingine vya hovyo.

Ndoto za kuzamia ughaibuni,
Kijana anashindwa kutumia Elimu yake aliyoipata shuleni au chuoni mwisho wa siku, anakata tamaa maana maisha nayo hayataki mikato ya hivyo.
 
Role model wenu siku hizi ni machawa,wakata mauno,wadangaji
Enzi zetu role model wetu walikuwa mabaharia,wapiganaji nk

Ova
sasa mkuu huoni kwamba hao ma-rollmodel ninyi ndo mmewazaa?
 
Tanzania tupo 60m wenye uwezo wa kufanya kazi wanaweza kuwa 15m ila NI KAZI YA SERIKALI KUHAKIKISHA AJIRA KWA WATU WAKE.

HAWATAKI KABISA HILI LITOKEE WAPO WANAHAKIKISHA WATU KUWA MASKINI ILI WAWATAWALE

Nchi za ulaya wanachagu kazi hadi leo hii, UK ni visiwa ila kazi zipo za kumwaga

WEUSI tuna matatizo
 
Kwahiyo unatakaje yan!?
Wewe unadhan nini kifanyike kama kusoma mmesoma ila kijiajiri hamuwezi!!.

Na hatuwezi au hatutaki?? Full kuchagua cha gua shughul za kufanya...Aibuu zimetujaaaaa tunaona soo hata kwe ye mambo yanabeba mustakabali wetu wenyewe eti kisa tuuu watu watatuochukuliaje!.
Vijana tuache upumbavu..tunataka kuwa smart muda wooote kaz kufanya tunaona aibu
Tukiweza kuicrack hiyo code, tumefanikiwa. Tunataka maisha mazuri lakini kufanya kazi hatutaki.
 
Ila betting hazikuwepo na enzi hiyo ukifika form 4 una maisha kuanzia ukarani kwenye vyama vya ushirika na kwenye ualimu..yaani ukifika chuo tu hata kama umesoma Bachelor of Arts in music wewe ni bosi mkubwa..
Nyakati zimebadilika. Mambo ya Trab na trat yameingia hapo. Itakuwaje sasa baada ya miaka 10 ijayo??
 
Kinachofuata ni kutokuwa na uzalendo ,Hao wazee waliopo wanawanyima fursa vijana soon wanazeeka na kupotea na kutuachia nchi sisi vijana wa hovyo ambao uzalendo umeshakwisha .....

Ni mwendo wa kuiba mali za umma pindi unapopata nafasi ,chota mihela tembea ,chota mihela sepaaaahakuna sijui nchi yangu kudadekiii
Well said. Sasa hivi kila anayetaka kuingia serikalini basi ni kupiga tu. Watu ulafi wa madaraka na ufujaji wa mali. Kama waliopo ndicho wanachokifanya tunawaangalia tutafanyaje?? Uzalendo hakuna.

Watu wanaenda jkt ili wawe wazalendo lakini ukweli wengi wanafikiria ajira za polisi na jwtz. Ni aibu.
 
Back
Top Bottom