Faure Gnassingbé ashinda urais Togo

dubu

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2011
Posts
3,502
Reaction score
3,486

Rais wa Togo Faure Gnassingbe


Tume ya uchaguzi nchini Togo, imetangaza kuwa Rais, Faure Gnassingbé, ameshinda tena kiti cha urais kwa muhula wa tatu.

Matokeo ya awali yanaonyesha kuwa Rais huyo aliyeingia uongozini mnamo mwaka 2005 amepata zaidi ya asilimia 58 ya kura.

Idadi iliyojitokeza kupiga kura siku ya Jumamosi ilifikia asilimia 60.

Bwana Gnassingbé amekuwa uongozini tangu kifo cha babake, Gnassingbé Eyadema, aliyechukua uongozi wa Togo kwa njia ya mapinduzi mwaka 1967.

Mwaka jana, kulikuwa na maandamano makubwa nchini Togo, huku waandamanaji wakiitaka serikali kubuni sheria ya mihula miwili ya Urais.

Chanzo: BBC Swahili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…