Idd Ninga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 5,539
- 4,854
1>upo mwingi usafiri,ila huu ni hatari.
Hatari si kama gari,lipasukapo tairi.
Nawaza naufikiri,sitopanda kwa hiyari.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
2>na ulimi ulikiri,kiri imani hariri.
Ninamuomba ghafari,ya ilahi ya qahari.
Afanye yangu safari,vyema mimi nisafiri.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
3>mwendo wake ni wa kasi,farasi huyu ajabu.
Wote wafanya maasi,watampanda kwa tabu.
Wakitokwa na kamasi,bora mapema kutubu.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
4>farasi hana kelele,ni mkimya wa sauti.
Hutompanda milele,hutompanda kwa suti.
Hata wako ukelele,utazimwa kwa manati.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
5>farasi siyo mzuri,japokuwa apendeza.
Atanukishwa uzuri,hakuna ataecheza.
Na tandiko lilo zuri,litafunikwa jeneza.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
Shairi=FARASI.
MTUNZI=Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0755519736 Au 0655519736.
Hatari si kama gari,lipasukapo tairi.
Nawaza naufikiri,sitopanda kwa hiyari.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
2>na ulimi ulikiri,kiri imani hariri.
Ninamuomba ghafari,ya ilahi ya qahari.
Afanye yangu safari,vyema mimi nisafiri.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
3>mwendo wake ni wa kasi,farasi huyu ajabu.
Wote wafanya maasi,watampanda kwa tabu.
Wakitokwa na kamasi,bora mapema kutubu.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
4>farasi hana kelele,ni mkimya wa sauti.
Hutompanda milele,hutompanda kwa suti.
Hata wako ukelele,utazimwa kwa manati.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
5>farasi siyo mzuri,japokuwa apendeza.
Atanukishwa uzuri,hakuna ataecheza.
Na tandiko lilo zuri,litafunikwa jeneza.
Namwaza huyu farasi,siku nikija mpanda.
Shairi=FARASI.
MTUNZI=Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0755519736 Au 0655519736.