FAO: Bei ya Chakula Ilifikia Kiwango Cha Juu Kabisa 2022

FAO: Bei ya Chakula Ilifikia Kiwango Cha Juu Kabisa 2022

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,768
Reaction score
49,940
Nyumbani Tanzania, malalamiko yamekuwa mengi kuhusiana na kupanda sana kwa bei ya chakula. Wengine wakiilaumu Serikali kuwa haikuchukua jitihada za kutosha ili kuzuia mfumko wa bei ya chakula.

Mimi si mtetezi wa Serikali, sijawahi kuwa na sitakuwa. Nafurahia uhuru wangu unaozingatia ukweli kuliko kumfurahisha mtu au kikundi cha watu.

Ukweli ni kwamba, mchanganyiko wa mambo, kuanzia Covid 19, vita vya Ukraine, bei kubwa ya mafuta, matatizo ya hali ya hewa na ongezeko kubwa la watu hasa kwa mataifa masikini na yanayoendelea, vyote kwa pamoja, vimechangia sana kupanda kwa bei ya chakula na bidhaa nyingine.

Mfumko huu wa bei ni janga lakini lenye fursa kubwa ndani yake. Ni janga kubwa kwa nchi ambazo hazina ardhi nzuri ya kilimo, hazina maji ya kutosha, hazina maeneo makubwa yenye ardhi nzuri, hazina utulivu wala amani (nchi kama Ukraine), lakini ni fursa nzuri sana kwa nchi kama Tanzania. Nchi ambayo ina eneo kubwa, ardhi nzuri ya kilimo, hali ya hewa nzuri inayoruhusu ustawi wa mazao, maji mengi kila kona, watu wengi wanaozurula na vinguo vichache mabegani, mazingira rahisi ya usafirishaji.

Serikali iwekeze kwa kiwango kikubwa kwenye kilimo. Wanannchi wa kawaida na wawekezaji, twende tukawekeze kwenye kilimo. Tatizo la upungufu wa chakula haliishi leo wala kesho. Leo nipo Njombe kwenye uwekezaji, angalao kwa kuanzia nilime ekari 200, lakini ikiwezekana nilime ekari 600 zote za shamba nililolipata.

Serikali iendelee kuachia uhuru kwa wakulima kuuza mazao mahali popote ili kujenga mazingira ya wengi kwenda kuwekeza kwenye kilimo. Bei nzuri ya mazao itavutia wengi kuwekeza kwenye kilimo. Serikali, ihamasishe sana uuzaji wa mazao yetu nje ya Taifa letu ili pesa ya mataifa hayo ije nchini mwetu, iongeze mzunguko wa fedha, iongeze akiba ya pesa ya kigeni, iinue hali za wananchi wa vijijini ambao kimsingi ndio wakulima.

World food prices hit record high in 2022

World food prices dropped for a ninth month in December, but hit their highest level on record for the full year in 2022, United Nations data found.

Food prices rose to a monthly record high in March after Russia invaded Ukraine, a significant worldwide wheat and cooking oil supplier.

A grain deal brokered by Turkey and the UN in July lifted a Russian naval blockade on Ukrainian exports.

The Food and Agriculture Organisation said its price index, tracking the monthly change in international food commodities, saw a 1.9 percent drop from November.

It was also 1 percent lower than in December 2021.

But the index was 14.3 percent higher overall in 2022 compared with the previous year as it reached an all-time high of 143.7 points.
 
Kuna watu wanasema Magufuli angekuwepo vyakula visingepanda bei..
Wengine wanasema angekuwepo mafuta ya petroli yasingepanda bei

Ndio maana nasema hii nchi haitakaa ipate maendeleo kwa akili kama hizi
 
Vijana wapewe maeneno ya kulima, trekta za kutosha mbegu bora na uhakika wa masoko baada.... sasa huo mchakato wa kuvipata hivi vitu, hata mwaka waeza isha usiambulie chochote
 
Nyumbani Tanzania, malalamiko yamekuwa mengi kuhusiana na kupanda sana kwa bei ya chakula. Wengine wakiilaumu Serikali kuwa haikuchukua jitihada za kutosha ili kuzuia mfumko wa bei ya chakula...
Pamoja na ukweli huu Sisi mtu aliechangia kupanda bei ya vyakula ni Waziri Bashe....alipokataa kuzuia chakula kwenda nje...matokeo yake walanguzi wanapeleka vyakula Kenya na Commoro wauze Kwa faida zaidi...

Kila mwaka kipindi hiki tunazuia vyakula kutoka nje ...mwaka huu Bashe kawakingia kifua walanguzi
 
Selikali hii imefeli sana kwenye suala la chakula!

Tulisema humu kwamba zuieni chakula kutoka nje maana soko la ndani bado halijajitosheleza, wapumbavu wakawa wanapiga mayowe eti ni muda wa mkulima kufaidi!

Ni mkulima yupi anafaidika na huu mfumuko wa bei za vyakula?
 
Pamoja na ukweli huu Sisi mtu aliechangia kupanda bei ya vyakula ni Waziri Bashe....alipokataa kuzuia chakula kwenda nje...matokeo yake walanguzi wanapeleka vyakula Kenya na Commoro wauze Kwa faida zaidi...

Kila mwaka kipindi hiki tunazuia vyakula kutoka nje ...mwaka huu Bashe kawakingia kifua walanguzi
Ni kweli, umakini walionao kudhibiti Foreign currency deposit hasa $ wangeweka pia kwenye chakula tusingefika hapa.

Nchi yetu haikusimama kipindi cha Covid hasa kwenye kilimo na hatukupata shida kubwa ya mvua. Tatizo huko walikojifungia kuwa na demand kubwa huku sisi wenyewe hatuna udhibiti mzuri.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Magufuli alipoambiwa nchi ina njaa mwaka 2017 alisemaje? Alisema Serikali haina shamba, asiyefanya kazi na asile , asipokula afe.

Alikuwa tayari kuona watu wanakufa kuliko kugawa chakula cha msaada
 
Back
Top Bottom