DOKEZO Familia ya Rais Kikwete yahusika ufisadi wa ESCROW

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mkuu Juve2012,

Ina maana na huu mradi ya yale yale madudu kuwa wataweka mkataba mkubwa na kuchota hela za Mkopo?



Mkuu unaniongezea hasira tu kwa kunikumbusha huu uchafu mwingine wa juzi juzi.

Kuna wakati najiuliza,hivi hawa viongozi wetu ni watz kwa asili kweli?au wamejivika huu utanzania?
 
Last edited by a moderator:

Weka ushahidi wa nyaraka, haya maneno matupu hata mie ningeweza kuyatunga na kuyaandika humu JF

Mkuu Hishma yako!

Huyo kijana Yeriko Msambila aka "Yericko Nyerere", basi hata kama akiweka hizo "nyaraka" zake kama ulivyomtaka/ulivyomwomba...bado pia ni mashaka na mughali kuaminika!

Kwa kifupi, huyu kijana ni muharibifu/mchafuzi tu wa mazingira...yaani anaishi tu mjini kwa kutumiwa kuwachafua watu mitandaoni kisiasa na pia kuratibu malumbano yaso tija baina ya Wana-Forum...kitu ambacho si faida kwa Taifa letu changa au khasa kwa Wananchi wa kawaida kama sisi tulioko huku vijijini! Daah!

Ubarikiwe Mkuu!

Ahsanta sana.
 
1743447_734633933296467_2738211866964166138_n.jpg
 
Hapo kwenye rangi inasababishwa na haya manyang'au yenye ulafi wa mafisi na mapanya. Kila kitu yanataka kifanywe kupitia makampuni ya nje ili yaweze kupokea rushwa kubwa kutoka haya makampuni ya nje.

Okey sawa lakini mbona mahakama zetu hazija amua in favor ya tanesco?
Au nazo zimekatiwa ?
Hii ishu pia inatokana ujinga jinga.
Zamani serikali ilijenga Mtera Kihansi Pangani Kidatu na nk . Hizi zote zikimilikiwa na serikali 100% .
Leo tumetiwa ujinga na wazungu tunawapa watu kuzalisha umeme.
Hii si biashara hii ni national service na jambo muhimu la uchumi na usalama wa nchi.
Leo watu tunakubali ushauri za kijinga kabisa kama hatuna akili.
Leo wangewezeshwa tanesco kununua majenereta wakazalisha umeme bila shaka bei ingekuwa chini
Sasa kuna maporomoko huko rufiji na singida badala ya kuwawezesha tanesco wakazalisha umeme tutawapa watu binafsi.mambo ya ajabu kabisa..
 
Tuziweke records sawasawa..........
Yerricko hajawahi kuleta ubaoni kitu cha maana zaidi ya majungu na umbea. Hata hili ni ujinga uleule wa BAVICHA.
Hahahaaaaaaaaaa ni MENDE TUU HAWA.
“Ignorance is a lot like alcohol: the more you have of it, the less you are able to see its effect on you.” (Jay M. Bylsma)
 
Hawa mafisadi wanakula bila hata kunawa mikono. Sijui Wadanganyika watajifunza lini kuwa majasiri kama Burkina Faso?
 
Naona umeamua ku-copy na ku-paste ile taarifa ya Yericko

Hata hivyo, sio mbaya cha msingi ujumbe ufike.
 
Naona yericko ameamua kutumia ile id yake nyingine kuweka tena uzi huu mods tuondoleeni taka hii au iunganishwe kwenue andiko la jana naona hakuna kipya.
 
anayetuhumu haleti ushahidi lakini anayetuhumiwa akikanusha anaambiwa kakanusha kikawaida, hii sio sawa. Hivi ingeandikwa katika thread hapo kuwa mmojawapo wa wamiliki wa simba trust ni wewe ungekanusha kivipi zaidi ya hivyo alivyokanusha miraji?
Ni equation ya power relation, huwezi elewa kama huwezi hoji sababu ya wewe kuwa hapo wakati anayekanusha ni wa "first family"!!!!
Wewe ukitembea kwa miguu huwezi weka headline lakini mtoto wa Rais akipanda daladala atakaa front page ya gazeti zoote!!!

Jikomboe kifikra!!!
 
Na hiyo PAP ni ya nani,?hayo majina ya viongozi wa upinzani hayakutajwa?mbna wengne umetaja wazi?
 
Naona yericko ameamua kutumia ile id yake nyingine kuweka tena uzi huu mods tuondoleeni taka hii au iunganishwe kwenue andiko la jana naona hakuna kipya.

Kama mlimbana kwenye mijadala sio mbaya akatumia id nyingine mpya ili kufikisha meseji kwa umma wa watanzania
 
Hawa mafisadi wanakula bila hata kunawa mikono. Sijui Wadanganyika watajifunza lini kuwa majasiri kama Burkina Faso?
Wanakula nini mkuu kwani kwenye hili andiko kunakitu cha maana hata kimoja kilichoandikwa zaidi ya vitu vya kutunga na porojo zisizokuwa na maana.
 
Kama mlimbana kwenye mijadala sio mbaya akatumia id nyingine mpya ili kufikisha meseji kwa umma wa watanzania
Kweli mkuu jamaa naona leo kaja na nyingine jana niliona kwa mbali katumia ile id yake ya yenye jina la kudandia toka ukoo wa nyerere.
 
Back
Top Bottom