Falsafa za wanawake wasioolewa

Kuna sehemu moja nimekuelewa mkuu! Kwamba angalau umri akifika wa 25 iwe kwa mwanaume au mwanamke,basi awe kwenye uhusiano unaoeleweka,na sio chain ya mabwana au mabibi.
 
Ni bora kutokuolewa kuliko kuolewa na kuishi katika karaha. Ndoa yenye furaha na amani ya kweli ni neema, ni tunu
 
Hivi nyie mnaopenda kuwasakama wanawake ambo hawajaolewa kwani hamjui kuwa wanawake tuko wengi kuliko wanaume? Mbona kila kitu kiko wazi? Au mnajisikia tu kusemasema wanawake. Huwa sipendi pale mtu anapouliza swali wakati jibu lake analijua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Haaaaaaa! eti incomplited certificate.
 
Naona wanazidi kumimina falsafa bila kujijua....haha
 
Kwasababu yule wa kula kwa jasho bado anajipanga. Sasa ulitaka aolewe na nani ikiwa wewe mwanaume bado haujawa tayari kuoa?
 
1.Idadi ya wanawake ni kubwa kuliko wanaume
2.Idadi ya wanaume(shoga) si riziki inaongezeka kwa kasi
3.Idai ya wanaume wanaopenda (iresponsible men)maisha mteremko inazidi kuongezeka
4.Idadi ya wanaume wote toa hao wanaume jina almost nusu inatoweka na kubakia nusu ambayo ndo waoaji
5.Wanawake wajioe au mwanaume mmoja aoe wanwake kumi? is it applicable?

Let women be guys sio wote watakaoolewa waolewe na nani wakati waoaji wapo wachache?
 
hivi kwanimi mwanamke asipoolewa mapema akavuka miaka thelathini...huwa anasimangwa sana na watu hadi jamii anayoishi
lakini
mwanaume akicheleqa kuoa wala hasimangwi..
Asili (nature) inataka mwanamke azae mapema kisha amalize kuzaa kabla ya miaka 40. Akichelewa kuolewa itabidi azae kwa matatizo na mateso kwake. Na akuchelewa zaidi hazai tena. Mwanaume hadi miaka 85 -95 anaweza kumpa mimba mwanamke. Pia huyo Me anaweza kuwa mzee zaidi ya miaka 60 akaowa binti wa miaka 18 lakini KE wa miaka 60 hawezi kuolewa na mvulana wa miaka 18 na wakapata watoto. Mwanamke anachukua umbo la kuzeeka na kupoteza mvuto mapema hivyo kumsababishia Me asiamshe dude na kupiga match.
 
hivi kwanimi mwanamke asipoolewa mapema akavuka miaka thelathini...huwa anasimangwa sana na watu hadi jamii anayoishi
lakini
mwanaume akicheleqa kuoa wala hasimangwi..
Anasimangwa kichinichini..oooh haamshi dude..mara anaogopa kutongoza..mara ooh hanisi..labda ndo ukute anavimwagia vitumbua mchanga sana ndo atakuwa safe mtaani.
Ila akiwa dormant..kazi anayo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao walio tayari ni wangapi na wanaoa wangapi? Ndio anakusubiri wewe unayejipanga.
Mimi wa kwanza nipo tayari! Nilishajipanga kitambo sana,tatizo hao waolewaji wanasema hawahitaji kuolewa kwa sasa kama mtoa sired alivyosema.
 
Miaka 30 na kuendelea, bado hajaolewa!! Huyo atakuwa amejitakia mateso ya moyo. Mara nyingi hawa ni wale ambao wametumia ujana wao vibaya, kwa kuchagua aina ya bwana atakaye muoa!

Umri ukifa 30 na kuendelea, anajikuta hana tena bwana wa kumchumbia. Mateso ya moyo yanaanza. Wanawake wa umri huu, utawakuta sana kwenye makanisa yanayoahidi miujiza, kwa waganga kusafisha nyota ili wapate mabwana wa kuwaoa.

Walio na nafasi ya kazi na pesa, ndo hao wao hujifanya kuwa hawana haraka ya kuolewa, lakini hiyo ni kujionyesha kwa juujuu tu, ndani ya nafsi zao wanaugulia na wanauchungu mkubwa kukosa wa kuwaoa.

Wanapozidiwa zaidi, hawa wanawake wa 30 na kuendelea huishia kupora mabwana wa wengine kwa kutumia nafasi yao ya kiuchumi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…