Falsafa ya Dkt. John Pombe Magufuli

Falsafa ya Dkt. John Pombe Magufuli

Tangia mwaka 1776, Taifa la Marekani limepitia vipindi tofauti tofauti ambavyo ndani yake vilitofautishwa na falsafa mbali mbali za uongozi katika kutekeleza sera ya nchi chini ya maraisi wao.

Lakini falsafa za maraisi mbali mbali katika taifa hili la marekani kuna zilizo kumbana na ukinzani dhidi ya azimio la mfumo fulani(x) ambao ulikuwa unatekelezwa na MaJesuit dhidi ya Mataifa ya Amerika ikiwemo Marekani
Amri ya Wajesuiti ilitimiza kiapo chao tena kwamba watatia sumu, wataua, au watafanya chochote kinachohitajika ili kuwaondoa wale wanaopinga mipango yao.

Kuanzia 1841 hadi 1857, Marais watatu wa Marekani walishambuliwa na Wajesuiti kama ilivyoainishwa katika Bunge la Vienna, Verona, na Chieri. Wawili walifariki na mmoja kutoroka (RAIS HARRISON, TAYLOR, NA BUCHANANI) akiwemo pia Rais Lincoln

Hu ulikuwa ni mpango wa Majesuit kuakikisha kuwa Hawaruhusu chochote kusimama katika njia yao ya utawala kamili wa Amerika, na uharibifu wa Katiba. Pia waliazimia kuimiliki United kwa usiri mkubwa kwa kutumia mawakala wao walio jofanya masikini na waaminifu wa kutoka kila kona ya ulimwengu, na kuwakusanya katika mioyo ya miji ya Washington, New York, Boston, Chicago, Buffalo, Albany, Troy, Cincinnati. Chini ya vivuli vya miji hiyo mikuu, Wamarekani .

Waliwatazama mawakala kama watu maskini na kwa dharau kubwa, kama wanaofaa tu kuchimba mifereji yao, kufagia mitaa yao na kufanya kazi katika jikoni zao. Hi ilikuwa ni moja ya mbinu zilizo tumiwa na hao Majesuit mda si mlefu Majesuit walipenya hadi kwenye idara nyeti za nchi hapo ndio ikawa mwanzo wa kuimiliki United.

Lakini falsafa za kizalendo za hao Marais (Lincoln, HARRISON, TAYLOR NA BUCHANANI) ziliendana ambazo zilijikita zaidi kuijenga United isiyo mpigia magoti mtu yeyote au taifa lolote ulimwenguni na kuifanya kuwa taifa huru lisiro na mfungamano wa Dini yoyote.
Ni falisafa ambazo zilikinzana na matakwa ya Majesuit na kwakuwa walipenya ndani ya serikali na idara nyeti ndio sababu walitekereza adhima yao ya kumfuta yeyote aliye ingilia njia zao na ndio maana hawa Marais waliuwawa.

Kwa mfanano huo wa Taifa la Marekani leo hii tunalitazama Taifa la TANZANIA chini ya Rais JOHN POMBE MAGUFULI
Falsafa yake ya uongozi imejikita zaidi katika uzalendo wa utaifa kwanza kulijenga taifa katika nyanja ya kiuchumi na kuziba mianya ya unyonyaji katika wizi wa rasilimali za taifa.

Kama ilivyo kuwa kwa taifa la Marekani leo hii africa tunafanywa hivyo hivyo ambapo tunashindwa kuwa na maamzi ya aina ipi ya demokrasia tunapaswa tuwenayo, tunashindwa kuwa na maamzi kwenye uchumi, Elimu na Siasa kwani hivyo vyote tumeingiliwa na mataifa ya nje(mabeberu)

Lakini falsafa ya Dkt. MAGUFULI ni kupambana na Diplomasia ya uchumi katika kulijenga Taifa ambapo katika nyanja hii ya uchumi ndipo kuna mizizi ya wanyonyaji ambao mpango wao ni kuliangamiza Taifa kuendelea kuwa masikini hivyo ni vita ambayo ni kari sana ambapo kama watanzania inatupasa kusimama pamoja na Rais wetu pasipo kujali tofauti zetu za kisiasa na kidini tuwe mstari wa mbele katika kumwombea Rais wetu na Taifa letu kwa ujumla (Yanayo endelea huko duniani ni makubwa sana kwa kuwa yanaendelea kwa siri kubwa ila matokeo yake ni kunyongwa kwa uchumi na kutaabika katika umasikini sana sana zawadi ambayo tunaweza pewa ni vita kuuwana sisi kwa sisi)

Watanzania tubadilike tuwaelewe viongozi wetu leo hii mifumo mingi ya nchi inashikiliwa na watu wachache ambao adhima yao ni kuitawala Dunia tuna tengenezewa majanga mbali mbali vita, magonjwa na njaa lengo lao ni nchi ziyumbe kiuchumi na tutumbukie kwenye mikopo ambayo tutaendelea kuwa wategemezi na hatuta weza kujikwamua KIUCHUMI mfano mwaka jana na mwaka huu wametengeneza janga la CORONA lakini wazuia nchi zingine kutengeneza chanjo lakini chaajabu wametengeneza wao chanjo na leo inapigwa promo ili mataifa yanunue au wapewe kama msaada kwa njia ya mkopo kupitia WB na IMF.

Sasa pale tunapo pata Rais ambaye kila njia za hawa watu anapambana kuzikwepa huyo ndie SHUJAA na MZALENDO wa kweli wa Taifa letu. Huyu ndie Raisi aliye weza kuonyesha falsafa ya uongozi wa kizalendo na ujasiri mkubwa katika kulijenga Taifa.
Mmeiba matrilioni sasa mnazungumzia falsafa.Ama kweli uhuru ni kitu kizuri na kibaya.Wakati wa huyo Hayati ungethubutu kuandika falsafa ya mtangulizi wake?Ungeozea Keko.Nyie sukuma gang mjue hii ni awamu ya sita.
 
Kama mtu ajawahi hata soma somo la uchumi au Development Study, knows nothing about economic atakuwa vipi na falsafa ya uchumi sasa. Uchumi unataka reasoning capacity sayansi inataka claiming capacity na sio reasoning. Hapa ni kuchanga viungo vya pilau.

Tuhesabu tu ni loss tujipange tu kwa ajae. Kama biashara zinapata hasara tuamini wakati mwingine nchi inapata hasara pia.
Huyo jamaa aliyeandika post hii ni mbumbubu tumdharau tu.Kaandikiwa na wale waliokula matrilioni kama ripoti ya CAG inavyoarifu.Hawa wapo wengi.Bado wanaota kuchota mabilioni.Nasikia wanajiita Sukuma Gang.Isitoshe huyu bado haamini kuwa sasa tupo kwenye awamu ya sita.#Kazi iendelee. Salaam za Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania.
 
Magufuli is a country bumpkin.

Hana falsafa yoyote, anaendesha nchi kwa mabavu.

Case in point.

Hakufanya homework yake kabla ya kuingilia biashara ya korosho.

Kwa mujibu wa ripoti ya Benki Kuu ya Tanzania ya Septemba 2019, mapato ya bidhaa za kilimo zilizouzwa nje mwaka ulioishia Agosti 2019 yalishuka kwa asilimia 55 ukilinganisha na mwaka ulioutangulia.

Hili ni anguko kubwa sana. Na sehemu kubwa ilichangiwa na Magufuli kuingilia kwa papara biashara ya korosho, zao la kilimo la pili kwa kuingiza fedha za kigeni wakati huo.

Sasa huyu mtu anayeangusha mapato ya mazao ya kilimo kwa asilimia 55 katika mwaka mmoja, kwa papara zake zisizo na mkakati, unaweza kusema ana falsafa ya uchumi?

Huyu anaelewa hata mambo ya msingi tu ya uchumi?
Huyo jamaa hakuamini kwenye kujenga taifa bali alitaka kila mwenye hela awe masikini na kila masikini aendelee kuwa masikini zaidi. Ni mjinga sana kwakweli. Hakuna falsafa aliyoweka alikuwa kama alfu Lela Ulela tu. Amebahatisha huo mradi wa umeme tu Ila mengine ya kawaida tu. Barabara hakuna serikali ambayo haikujenga.
 
Back
Top Bottom