Kama unapoanza mahusiano na mwanamke kwa mara kwanza unakuwa na tabia ya kumuuliza "mimi ni mpenzi wako wa ngapi?" basi lazima ukumbane na maswahiba kama hayo! Yaani kuna wanaume wa ajabu sana...unamuuliza mwanamke mimi ni wako wa ngapi unatarajia atakuambia wewe ni wa kumi hata kama alivuka idadi hiyo tangu kidato cha pili?! Atakuambia wewe ni pili, amekuheshimu sana atakuambia wewe wa tatu na ukikutana na ngurubembe kabisa lazima akuambie wewe ni wa kwanza na kukupa bikira ya ndimu!