Faini za trafiki ziwe mtandaoni

Faini za trafiki ziwe mtandaoni

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
23,251
Reaction score
28,406
Napenda kuishauri serikali iweke utaratibu wa kuziweka mtandaoni faini za madereva wa magari.

Idadi kubwa ya magari yanayoendeshwa na madereva waajiriwa, kutokana na hali hii baadhi ya madereva wanapopigwa faini wao hunyamaza wakijua baadaye hawatakuwa na magari husika, na bahati mbaya magari yenyewe ni ya kupokezana, jambo linalosababisha gari kukamatwa na dereva mwingine na mmiliki kujikuta akilipa faini na riba ya malimbikizo.

Muda umefika sasa kwa serikali kuweka mamba za magari na majina ya madereva mtandaoni ili wenye magari waweze kufuatilia mwenendo wa magari yao na kuondokana na riba za faini.
 
Ipo link unaweza kucheck ama gari inadaiwa kabla hujafanya handover
 
Lakini si kuna utaratibu wa kuangalia iwapo gari inadaiwa au haidaiwi? Dereva anapopokea gari ni wajibu wake kujiridhisha kama gari lina deni au halina. Mmiliki anawaandalia tu kitabu cha makabidhiano.
 
Issue hapa ni kwamba hakuna tofauti katika faini (mlipaji) kwa makosa ya dereva na makosa ya hali ya gari (uchakavu). Kwa mfano dereva anaweza kupata ajali kutokana na ulevi ambapo mwenye gari atalipa faini kwa kosa la kinidhamu la dereva. Ni muda muafaka kwa serikali kuja na mfumo ambapo faini zinapoandikwa ziambatanishwe kwenye Tin number kama kosa ni la gari (ubovu) au ziambatanishwe kwenye number ya leseni kama kosa ni la dereva. Natambua kwamba kwa mfumo wa sasa kuna changamoto ya kumtambua dereva anaedaiwa awapo barabarani LAKINI wakati wa kurenew Leseni dereva atalipa bila kupenda.Nawakilisha
 
si madereva tu, hata wakati umemkabidhi fundi kwa marekebisho, na yeye anaweza kulitumia na kufanya makosa, anakukabidhi gari bila kukutaarifu....ni bora kuwa unakagua, hii itaindoa usumbufu sana, asante kwa uliweka link.......@mahole
 
Napenda kuishauri serikali iweke utaratibu wa kuziweka mtandaoni faini za madereva wa magari.

Idadi kubwa ya magari yanayoendeshwa na madereva waajiriwa, kutokana na hali hii baadhi ya madereva wanapopigwa faini wao hunyamaza wakijua baadaye hawatakuwa na magari husika, na bahati mbaya magari yenyewe ni ya kupokezana, jambo linalosababisha gari kukamatwa na dereva mwingine na mmiliki kujikuta akilipa faini na riba ya malimbikizo.

Muda umefika sasa kwa serikali kuweka mamba za magari na majina ya madereva mtandaoni ili wenye magari waweze kufuatilia mwenendo wa magari yao na kuondokana na riba za faini.
Pia waweke na leseni ya dereva aliefanya kosa.

Mm shapigwaga fain kwa kosa ambalo sikufanya nawauliza wanionyeshe namba na jina ya leseni ya aliefanya makosa wanasema haijawekwa yan ata jina la askar aliepiga hyo fain halipo.

Trafik anapokushika lazima achukue namba ya leseni,namba ya gari

Pia karatasi lazima hionyeshe location ya kosa lilipo fanyikia na jina la hyo trafik.

Finginevyo bdo tunaibiwa.
 
si madereva tu, hata wakati umemkabidhi fundi kwa marekebisho, na yeye anaweza kulitumia na kufanya makosa, anakukabidhi gari bila kukutaarifu....ni bora kuwa unakagua, hii itaindoa usumbufu sana, asante kwa uliweka link.......@mahole

Iwapo fundi atakamatwa amefanya makosa na ana leseni inakuwa tu ni kama kosa la dereva mwingine ILA kama hana leseni basi yeye fundi na gari wanawekwa chini ya ulinzi hadi mwenye gari aje kuchukua gari yake.
 
Pia waweke na leseni ya dereva aliefanya kosa.

Mm shapigwaga fain kwa kosa ambalo sikufanya nawauliza wanionyeshe namba na jina ya leseni ya aliefanya makosa wanasema haijawekwa yan ata jina la askar aliepiga hyo fain halipo.

Trafik anapokushika lazima achukue namba ya leseni,namba ya gari

Pia karatasi lazima hionyeshe location ya kosa lilipo fanyikia na jina la hyo trafik.

Finginevyo bdo tunaibiwa.
Hizo taarifa zote zipo kuanzia kosa alilofanya, muda, sehemu, askari aliemwandikia, mpaka namba ya leseni ya aliyefanya kosa ipo tatzo wengi hatujapata elimu ya namna ya kuhakiki maana kuna weng sana wanabambikiwa makosa kutokana na makosa ya uandishi wa kati ya plate namba ama namba ya leseni
 
Iwapo fundi atakamatwa amefanya makosa na ana leseni inakuwa tu ni kama kosa la dereva mwingine ILA kama hana leseni basi yeye fundi na gari wanawekwa chini ya ulinzi hadi mwenye gari aje kuchukua gari yake.
wengi wana leseni bro, tatizo keshakukabidhi gari, hajakwambia....mara paap umekaguliwa, gari ina makosa, namaba na jina ni fundi wako......gari haiondoki bila kulipwa + penalty
 
Ni vizuri link hiyo kama ipo iwe wazi ijulikane, kutokujulikana kutokana na trafiki kutowajulisha madereva na wamiliki ndilo kunasababisha malalamiko. Link hiyo iwe kwenye stika za usalama barabarani.
Wanaojua hali halisi ya ajira za madereva hawezi kuzungumzia makabidhiano na daftari.
 
Hizo taarifa zote zipo kuanzia kosa alilofanya, muda, sehemu, askari aliemwandikia, mpaka namba ya leseni ya aliyefanya kosa ipo tatzo wengi hatujapata elimu ya namna ya kuhakiki maana kuna weng sana wanabambikiwa makosa kutokana na makosa ya uandishi wa kati ya plate namba ama namba ya leseni
Wewe pia hauijui hiyo link! Kama unaijua kwanini iwe siri yako!
 
Back
Top Bottom