Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,198
- 7,536
Wadau,
Wapo ndugu zetu ambao wanadhani kwamba siasa bora, au siasa wanazoziweza ni siasa za chuki na fitna na hivyo wamewekeza sana kwenye eneo hilo.Ni vyema tukawekana sawa juu ya faida ya siasa hizo ili waliowekeza humo wawe wanafanya wakiwa na 'Informed Mind '
1. Siasa za chuki humfanya muhusika awe anapambana na watu badala ya kupambana na hoja (Concepts& arguments) kwa mtu yeyote anayefanya siasa kwa kusukumwa na chuki, hata ije hoja nzuri kiasi gani, haangalii hoja bali huangalia nani kaileta na kuanza kupambana naye.
2. Mfanya siasa za chuki huwa hana amani moyoni na wala hana uso wa tabasamu.Hii ni kutokana na roho ya visasi na nia mbaya ambavyo vinakuwa vinamsuta ndani yake. Hali hii humsababisha awe anaishi katika msongo wa mawazo wakati wote na kuwa na sura ama ya kuchukiza au ya kutisha.
3. Wanaowekeza katika siasa za chuki, hujikuta wakiwajibika kutumia mbinu yetote iwe halali au haramu kuwashinda wale wanaowachukia kitu ambacho wakati mwingine huleta madhara kwao wenyenye au kwa jamii nzima.
4. Wenye kufanya siasa za chuki, inapotokea wakashindwa katika uchaguzi, hu- panic kwa kuogopa uwezekano wa kulipiziwa visasi kwa kuwa huogopa kuwa huenda wakafanyiwa yale waliowafanyia wengine. Wakati mwingine huishia kukata tamaa na kuamua kujiua kama balozi wa Libya.
Kuna faida nyingi za siasa za aina hii nawe unaweza kuongezea.
Kwa ujumla tushauri tu kuwa, ni vyema tukafanya siasa tukiwa free minded na tukisukumwa na hoja pamoja na dhamira safi badala ya chuki. Hii itatuwezesha kuwa flexible pamoja na kuwa na amani (peace of mind) Ikionekana inafaa ni bora tukaziepuka siasa hizi.
Wapo ndugu zetu ambao wanadhani kwamba siasa bora, au siasa wanazoziweza ni siasa za chuki na fitna na hivyo wamewekeza sana kwenye eneo hilo.Ni vyema tukawekana sawa juu ya faida ya siasa hizo ili waliowekeza humo wawe wanafanya wakiwa na 'Informed Mind '
1. Siasa za chuki humfanya muhusika awe anapambana na watu badala ya kupambana na hoja (Concepts& arguments) kwa mtu yeyote anayefanya siasa kwa kusukumwa na chuki, hata ije hoja nzuri kiasi gani, haangalii hoja bali huangalia nani kaileta na kuanza kupambana naye.
2. Mfanya siasa za chuki huwa hana amani moyoni na wala hana uso wa tabasamu.Hii ni kutokana na roho ya visasi na nia mbaya ambavyo vinakuwa vinamsuta ndani yake. Hali hii humsababisha awe anaishi katika msongo wa mawazo wakati wote na kuwa na sura ama ya kuchukiza au ya kutisha.
3. Wanaowekeza katika siasa za chuki, hujikuta wakiwajibika kutumia mbinu yetote iwe halali au haramu kuwashinda wale wanaowachukia kitu ambacho wakati mwingine huleta madhara kwao wenyenye au kwa jamii nzima.
4. Wenye kufanya siasa za chuki, inapotokea wakashindwa katika uchaguzi, hu- panic kwa kuogopa uwezekano wa kulipiziwa visasi kwa kuwa huogopa kuwa huenda wakafanyiwa yale waliowafanyia wengine. Wakati mwingine huishia kukata tamaa na kuamua kujiua kama balozi wa Libya.
Kuna faida nyingi za siasa za aina hii nawe unaweza kuongezea.
Kwa ujumla tushauri tu kuwa, ni vyema tukafanya siasa tukiwa free minded na tukisukumwa na hoja pamoja na dhamira safi badala ya chuki. Hii itatuwezesha kuwa flexible pamoja na kuwa na amani (peace of mind) Ikionekana inafaa ni bora tukaziepuka siasa hizi.