Bata batani
JF-Expert Member
- Nov 11, 2011
- 3,182
- 3,547
KUACHWA NA MTU ULIYEMPENDA ZAIDI SIO MCHEZO ZIFUATAZO NI DALILI ZA MTU ALIYEACHWA
~ Muhanga wa tatizo hili hukosa utulivu wa akili katika kufanya na kukumbuka mambo yake binafsi na hata ya kijamii. Hushindwa kufanya maamuzi katika masuala mbalimbali yanayomtaka yeye kuamua.
~Mtu hujihisi mkosaji, asiye na faida wala msaada katika familia na jamii kwa ujumla. mara nyingi mtu wa namna hii hujiengua na kujiweka mbali na watu wengine na mara nyingine hufikiria na kujihisi hana hadhi.
~Mtu mwenye tatizo hili, hukosa tumaini la maisha, huona kila kitu kwake ni kibaya au kila jambo haliendi sawa, hujihisi kua na mkosi katika kila jambo analofanya. hujihisi kila mmoja ni adui yake anamuonea na kumg'ong'a.
~Wagonjwa wengi wenye dalili za tatizo hili, hukosa usingizi na huwahi kuamka asubuhi . Mwili hukosa nguvu pia na afya ya mwili kudhoofika.
~Mgonjwa hukosa hamu ya kufanya mambo muhimu tena ya furaha ,vitu kama vile kushiriki kufanyq kazi za kumuingizia kipato, kushiriki sherehe au hata michezo na shughuli mbalimbali za kijamii.
~Mtu hukosa hamu ya kula,kila chakula hutoa ladha mbaya mdomoni mwake na huona hakuna faida ya kukila chakula hicho.hii nayo huchangia mgonjwa kudhohofika kwa mwili.
~Wakati mwingine mtu mwenye tatizo hili,hujihisi maumivu ya kichwa na mwili mzima,hii ni kutoka na kufikiria sana kwa muda mrefu.
~Mtu mwenye tatizo hili asipopatiwa matibabu kwa muda mrefu hufikia hatua ya kufikiria kujitoa uhai. Mara nyingi utamuona akizungumzia kupotea hapa duniani, kutoa uhai wake mwenyewe. Mtu huyu asipopata uangalizi wa kutosha huweza kujitoa uhai wake mwenyewe.
HAYA ENDELEA KAMA ZINGINE UNAZIFAHAMU
~ Muhanga wa tatizo hili hukosa utulivu wa akili katika kufanya na kukumbuka mambo yake binafsi na hata ya kijamii. Hushindwa kufanya maamuzi katika masuala mbalimbali yanayomtaka yeye kuamua.
~Mtu hujihisi mkosaji, asiye na faida wala msaada katika familia na jamii kwa ujumla. mara nyingi mtu wa namna hii hujiengua na kujiweka mbali na watu wengine na mara nyingine hufikiria na kujihisi hana hadhi.
~Mtu mwenye tatizo hili, hukosa tumaini la maisha, huona kila kitu kwake ni kibaya au kila jambo haliendi sawa, hujihisi kua na mkosi katika kila jambo analofanya. hujihisi kila mmoja ni adui yake anamuonea na kumg'ong'a.
~Wagonjwa wengi wenye dalili za tatizo hili, hukosa usingizi na huwahi kuamka asubuhi . Mwili hukosa nguvu pia na afya ya mwili kudhoofika.
~Mgonjwa hukosa hamu ya kufanya mambo muhimu tena ya furaha ,vitu kama vile kushiriki kufanyq kazi za kumuingizia kipato, kushiriki sherehe au hata michezo na shughuli mbalimbali za kijamii.
~Mtu hukosa hamu ya kula,kila chakula hutoa ladha mbaya mdomoni mwake na huona hakuna faida ya kukila chakula hicho.hii nayo huchangia mgonjwa kudhohofika kwa mwili.
~Wakati mwingine mtu mwenye tatizo hili,hujihisi maumivu ya kichwa na mwili mzima,hii ni kutoka na kufikiria sana kwa muda mrefu.
~Mtu mwenye tatizo hili asipopatiwa matibabu kwa muda mrefu hufikia hatua ya kufikiria kujitoa uhai. Mara nyingi utamuona akizungumzia kupotea hapa duniani, kutoa uhai wake mwenyewe. Mtu huyu asipopata uangalizi wa kutosha huweza kujitoa uhai wake mwenyewe.
HAYA ENDELEA KAMA ZINGINE UNAZIFAHAMU