Meja Jenerali Isamuhyo
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 3,129
- 9,678
Nchi ya Ethiopia imepiga marufuku na kuondoa makampuni ya kubet nchini mwao.
Hii ni katika harakati za kuwaondoa wananchi na utegemezi na uraibu wa kamari badala ya kufanya kazi za ujenzi wa Taifa.
Unaonaje uamuzi wa serikali ya Ethiopia? Tuwaige au tupotezee?.
======
Ethiopia imesitisha rasmi shughuli zote za kubashiri (betting) nchini humo baada ya Mamlaka ya Bahati Nasibu (Ethiopian Lottery Service – ELS) kuagiza benki, waendeshaji wa mifumo ya malipo na taasisi za kifedha kusitisha mara moja kushughulikia miamala yote inayohusiana na betting.
Agizo hilo linaanza kutekelezwa mara moja na linahusu kampuni zote zinazofanya kazi kwa sasa pamoja na kampuni 22 ambazo leseni zao zilisitishwa wiki mbili zilizopita.
ELS imesema uamuzi huo umetokana na uchunguzi unaoendelea pamoja na matokeo ya tathmini ya kitaifa ya sekta ya betting na fedha, ambayo yamebaini ukiukwaji mkubwa wa masharti ya leseni na uhamishaji haramu wa fedha unaohatarisha usalama wa taifa.
Mamlaka hiyo imeonya kuwa shughuli zote za betting, iwe mtandaoni au ana kwa ana, lazima zisitishe mara moja, huku mifumo yote ya kupokea amana na njia za malipo zikilazimika kusitisha huduma zake.
ELS imeeleza kuwa yeyote atakayeharibu, kubadilisha au kuficha ushahidi atachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria za Ethiopia.
“Waendeshaji wa betting wanapaswa kuhifadhi kwa usalama taarifa za seva, kumbukumbu za kifedha na taarifa za watumiaji,” ilisema ELS.
Taasisi za kifedha, watoa huduma za malipo na waendeshaji wa mifumo ya malipo wamejulishwa kuwa leseni za kampuni zote za betting zitafutwa rasmi ndani ya wiki mbili zijazo.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani, hatua hiyo imefuatia operesheni kubwa ya utekelezaji wa sheria iliyohusisha idara ya ujasusi wa taifa, huduma za usalama wa kifedha na polisi wa shirikisho.
Operesheni hiyo ilisababisha kukamatwa kwa wamiliki kadhaa wa kampuni za betting za michezo pamoja na washirika wao, wakituhumiwa kuficha zaidi ya Birr milioni 100 (sawa na Shilingi milioni 83) za mapato na kodi ambazo hazikuripotiwa.
Ripoti ya Birr Metrics imesema msako huo unaashiria mabadiliko makubwa katika mkabala wa udhibiti wa ELS, kufuatia hatua za awali zilizochukuliwa mapema mwaka huu kuimarisha usimamizi wa shughuli za michezo ya kubahatisha na bahati nasibu. Mnamo Aprili 2025, ELS ilizindua mfumo wa kwanza wa bahati nasibu wa kidijitali nchini Ethiopia kama sehemu ya mpango wa kisasa wa kupanua upatikanaji na kuongeza uwazi katika huduma za michezo ya kubahatisha zinazosimamiwa na serikali.
======
Ethiopia has shut down its entire betting industry after the Lottery Service (ELS) ordered banks, payment operators, and financial intermediaries to stop processing all betting transactions.The directive takes effect immediately and applies to both currently operating firms and 22 companies whose betting licenses were suspended two weeks earlier.
ELS said the move stems from ongoing investigations and findings from a nationwide review of the betting and finance sector, which flagged widespread breaches of licence agreements and illicit financial transfers that pose a threat to national security.It warned that all betting activity, whether digital or otherwise, must stop immediately, and that deposit gateways and payment channels must cease services.ELS emphasised that destroying, altering or concealing evidence will attract criminal prosecution under Ethiopian law.
"Operators are obliged to securely retain server data, financial records and user information," said ELS.Financial institutions, payment instrument issuers and payment system operators have been notified that the licences of all betting companies will be formally revoked within the next two weeks.
According to local media, the revocations follow a sweeping enforcement operation involving the national intelligence, the financial security service and the federal police.The operation led to the arrest of several sports betting company owners and associates over the suspected concealment of more than 100 million Birr (Sh83 million) in unreported revenue and tax proceeds."The crackdown marks a dramatic shift in ELS’s regulatory approach following broader measures earlier in the year to tighten oversight of gaming and lottery operations. In April 2025, ELS launched Ethiopia’s first digital lottery platform as part of its modernisation drive, aimed at expanding access and enhancing transparency in state‑regulated gaming services," Birr Metrics reported.
Hii ni katika harakati za kuwaondoa wananchi na utegemezi na uraibu wa kamari badala ya kufanya kazi za ujenzi wa Taifa.
Unaonaje uamuzi wa serikali ya Ethiopia? Tuwaige au tupotezee?.
======
Ethiopia imesitisha rasmi shughuli zote za kubashiri (betting) nchini humo baada ya Mamlaka ya Bahati Nasibu (Ethiopian Lottery Service – ELS) kuagiza benki, waendeshaji wa mifumo ya malipo na taasisi za kifedha kusitisha mara moja kushughulikia miamala yote inayohusiana na betting.
Agizo hilo linaanza kutekelezwa mara moja na linahusu kampuni zote zinazofanya kazi kwa sasa pamoja na kampuni 22 ambazo leseni zao zilisitishwa wiki mbili zilizopita.
ELS imesema uamuzi huo umetokana na uchunguzi unaoendelea pamoja na matokeo ya tathmini ya kitaifa ya sekta ya betting na fedha, ambayo yamebaini ukiukwaji mkubwa wa masharti ya leseni na uhamishaji haramu wa fedha unaohatarisha usalama wa taifa.
Mamlaka hiyo imeonya kuwa shughuli zote za betting, iwe mtandaoni au ana kwa ana, lazima zisitishe mara moja, huku mifumo yote ya kupokea amana na njia za malipo zikilazimika kusitisha huduma zake.
ELS imeeleza kuwa yeyote atakayeharibu, kubadilisha au kuficha ushahidi atachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria za Ethiopia.
“Waendeshaji wa betting wanapaswa kuhifadhi kwa usalama taarifa za seva, kumbukumbu za kifedha na taarifa za watumiaji,” ilisema ELS.
Taasisi za kifedha, watoa huduma za malipo na waendeshaji wa mifumo ya malipo wamejulishwa kuwa leseni za kampuni zote za betting zitafutwa rasmi ndani ya wiki mbili zijazo.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani, hatua hiyo imefuatia operesheni kubwa ya utekelezaji wa sheria iliyohusisha idara ya ujasusi wa taifa, huduma za usalama wa kifedha na polisi wa shirikisho.
Operesheni hiyo ilisababisha kukamatwa kwa wamiliki kadhaa wa kampuni za betting za michezo pamoja na washirika wao, wakituhumiwa kuficha zaidi ya Birr milioni 100 (sawa na Shilingi milioni 83) za mapato na kodi ambazo hazikuripotiwa.
Ripoti ya Birr Metrics imesema msako huo unaashiria mabadiliko makubwa katika mkabala wa udhibiti wa ELS, kufuatia hatua za awali zilizochukuliwa mapema mwaka huu kuimarisha usimamizi wa shughuli za michezo ya kubahatisha na bahati nasibu. Mnamo Aprili 2025, ELS ilizindua mfumo wa kwanza wa bahati nasibu wa kidijitali nchini Ethiopia kama sehemu ya mpango wa kisasa wa kupanua upatikanaji na kuongeza uwazi katika huduma za michezo ya kubahatisha zinazosimamiwa na serikali.
======
Ethiopia has shut down its entire betting industry after the Lottery Service (ELS) ordered banks, payment operators, and financial intermediaries to stop processing all betting transactions.The directive takes effect immediately and applies to both currently operating firms and 22 companies whose betting licenses were suspended two weeks earlier.
ELS said the move stems from ongoing investigations and findings from a nationwide review of the betting and finance sector, which flagged widespread breaches of licence agreements and illicit financial transfers that pose a threat to national security.It warned that all betting activity, whether digital or otherwise, must stop immediately, and that deposit gateways and payment channels must cease services.ELS emphasised that destroying, altering or concealing evidence will attract criminal prosecution under Ethiopian law.
"Operators are obliged to securely retain server data, financial records and user information," said ELS.Financial institutions, payment instrument issuers and payment system operators have been notified that the licences of all betting companies will be formally revoked within the next two weeks.
According to local media, the revocations follow a sweeping enforcement operation involving the national intelligence, the financial security service and the federal police.The operation led to the arrest of several sports betting company owners and associates over the suspected concealment of more than 100 million Birr (Sh83 million) in unreported revenue and tax proceeds."The crackdown marks a dramatic shift in ELS’s regulatory approach following broader measures earlier in the year to tighten oversight of gaming and lottery operations. In April 2025, ELS launched Ethiopia’s first digital lottery platform as part of its modernisation drive, aimed at expanding access and enhancing transparency in state‑regulated gaming services," Birr Metrics reported.