Ni takribani zimepita siku tatu tangu kumalizika kwa kikao cha bunge la JMT kule Dodoma huku Taifa likiwa limeachwa kwenye sintofahamu ya.kushindwa kuujua ukweli wa nini hasa kilichojiri kwenye akaunti ya Escrow. Ili kuielewa sintofahamu hii nitatumia mfano wa tukio la kweli lililotolea mtaani kwetu jana.
Majira ya saa tatu za isiku tulisikia kelele za mwizi ambapo wengi wetu tuliokuwa majumbani tulitoka na kila aina ya silaha kwa lengo la kumtia adabu.huyo mwizi. Kulikuwa na vijana watatu wanakimbia. Nasi bila ya kuhoji tukaanza kuwapiga wale vijana japokuwa walikuwa wakijitetea kuwa hawakuiba. Tuliendelea kuwasulubu hadi walipoonekana kuwa wameiva kwa kichapo, kuna mzee wa makamu akatuasa kuacha kuwapiga na kuuliza ni nani aliyeibiwa na wameiba nini. Swali lile lilionekana kutushtua kwani ghafla kila mtu alijihisi kuwa na hatia na hivyo kwa lengo la kukwepa mkono wa sheria, tulianza kupotea eneo la tukio kabla mambo hayajaharibika.
Ni tukio hili ndo limenisukuma kukumbuka makandokando yaliyolizunguka sakata la Escrow.
Kama tukumbakavyo sakata hili liliibuliwa na David Kafulila ambapo alikwenda mbali.zaidi kwa kumuita AG Werema kuwa ni mwizi ambapo reaction ya werema ilikuwa ni kuibuka kwa matumizi mapya ya msamiati wa Tumbili.
Pia kutokana na kuibuka kwa sakata hilo, Bunge lilimuagiza CAG kufanya ukaguzi wa dharura kwenye akaunti ya Escrow na kiwasilisha taarifa hiyo. Sio jukumu langu kurudia tulioyasikia na kuyaona.
Lengo langu ni kuwashirikisha wanajf juu ya kile ninachohisi kuwa ni makandokando yaliyopo nyuma ya sakata hili kwa nia njema ya kutumia jicho la tatu.
Na haya ndio makandokando ya Sakata zima la ESCROW.
Kwa muda wote wa sakata hili, tuliaminishwa kuwa Werema, Muhongo, Maswi na Pinda ni miongoni mwa walionufaika na fedha za Escrow. Lakini kwa mujibu wa taatifa ya CAG hawajaoneshwa kuwa kuna miamala inayowahusu.
Upi ukweli kuwa waliiba au hawakuiba? Lakini jambo la kushangaza ni kuwa kwa mujibu wa Mwigulu Nchemba, suala zima la Escrow ni purely legal and technical issue na sio political.
Kwa mujibu ws maelezo ya wabunge na media, kuna mkanganyiko kuhusu fedha zilizodaiwa kuibwa ni takribani Bil 306, 321 na Bil 183. Lakini hadi Bunge limaweka maazimio kiasi halisi kilchokuwemo kwenye akaunti hiyo hakijulikani.
Ripoti ya CAG ilikuwa haijitoshelezi na badala ya kuagiza ukaguzi wa kina, PAC ilikurupuka kuwa DPCCB na mkurugenzi mkuu wa TRA watoe maelezo mbele ya Kamati ambao pia hawakuwa na majibu yanayojitosheleza kuwa fedha za Escrow ni umma au ni za IPTL Hapa inatoa mashaka kuwa taarifa ya CAG haikuwa conclusive ma hivyo kuhitaji corroborative evidence. Mtu kama DPCCB hakustahili kuitwa kwa kuwa hakuwa sehemu ya uchungiuzi.
Mjadala kugubikwa na jazba na kelele na vitisho. Kwa kawaida jambazi akitaka kuchukuwa kitu hutumia vitisho na nguvu. Na mwanasiasa yeyote akitaka jambo lake lipite hutumia pia vitisho na uibuaji wa kashfa na wakati wa kujadili hujitahidi kuonesha jinsi alivyoguswa na uovu anaoulalamikia. Hili lilijitokeza kwa kiwango cha juu kiasi cha kuanza kutuaminisha kuwa nyuma uzalendo kuna jambo lililojificha. Hili linathibitishwa na aina ya maazimio yaliyopendekezwa na PAC. Kama sio hivyo ni kwa nini mjadala haukuwa ma busara?
Kutokana na makandokando haya, itakuwa ni jambo la busara iwapo raisi haitaingia kwenye mkenge na badala yake awarudishie bumge suala hilo ili waagize ukaguzi wa kina kufanyika
Karibuni kwa mjadala.
Majira ya saa tatu za isiku tulisikia kelele za mwizi ambapo wengi wetu tuliokuwa majumbani tulitoka na kila aina ya silaha kwa lengo la kumtia adabu.huyo mwizi. Kulikuwa na vijana watatu wanakimbia. Nasi bila ya kuhoji tukaanza kuwapiga wale vijana japokuwa walikuwa wakijitetea kuwa hawakuiba. Tuliendelea kuwasulubu hadi walipoonekana kuwa wameiva kwa kichapo, kuna mzee wa makamu akatuasa kuacha kuwapiga na kuuliza ni nani aliyeibiwa na wameiba nini. Swali lile lilionekana kutushtua kwani ghafla kila mtu alijihisi kuwa na hatia na hivyo kwa lengo la kukwepa mkono wa sheria, tulianza kupotea eneo la tukio kabla mambo hayajaharibika.
Ni tukio hili ndo limenisukuma kukumbuka makandokando yaliyolizunguka sakata la Escrow.
Kama tukumbakavyo sakata hili liliibuliwa na David Kafulila ambapo alikwenda mbali.zaidi kwa kumuita AG Werema kuwa ni mwizi ambapo reaction ya werema ilikuwa ni kuibuka kwa matumizi mapya ya msamiati wa Tumbili.
Pia kutokana na kuibuka kwa sakata hilo, Bunge lilimuagiza CAG kufanya ukaguzi wa dharura kwenye akaunti ya Escrow na kiwasilisha taarifa hiyo. Sio jukumu langu kurudia tulioyasikia na kuyaona.
Lengo langu ni kuwashirikisha wanajf juu ya kile ninachohisi kuwa ni makandokando yaliyopo nyuma ya sakata hili kwa nia njema ya kutumia jicho la tatu.
Na haya ndio makandokando ya Sakata zima la ESCROW.
Kwa muda wote wa sakata hili, tuliaminishwa kuwa Werema, Muhongo, Maswi na Pinda ni miongoni mwa walionufaika na fedha za Escrow. Lakini kwa mujibu wa taatifa ya CAG hawajaoneshwa kuwa kuna miamala inayowahusu.
Upi ukweli kuwa waliiba au hawakuiba? Lakini jambo la kushangaza ni kuwa kwa mujibu wa Mwigulu Nchemba, suala zima la Escrow ni purely legal and technical issue na sio political.
Kwa mujibu ws maelezo ya wabunge na media, kuna mkanganyiko kuhusu fedha zilizodaiwa kuibwa ni takribani Bil 306, 321 na Bil 183. Lakini hadi Bunge limaweka maazimio kiasi halisi kilchokuwemo kwenye akaunti hiyo hakijulikani.
Ripoti ya CAG ilikuwa haijitoshelezi na badala ya kuagiza ukaguzi wa kina, PAC ilikurupuka kuwa DPCCB na mkurugenzi mkuu wa TRA watoe maelezo mbele ya Kamati ambao pia hawakuwa na majibu yanayojitosheleza kuwa fedha za Escrow ni umma au ni za IPTL Hapa inatoa mashaka kuwa taarifa ya CAG haikuwa conclusive ma hivyo kuhitaji corroborative evidence. Mtu kama DPCCB hakustahili kuitwa kwa kuwa hakuwa sehemu ya uchungiuzi.
Mjadala kugubikwa na jazba na kelele na vitisho. Kwa kawaida jambazi akitaka kuchukuwa kitu hutumia vitisho na nguvu. Na mwanasiasa yeyote akitaka jambo lake lipite hutumia pia vitisho na uibuaji wa kashfa na wakati wa kujadili hujitahidi kuonesha jinsi alivyoguswa na uovu anaoulalamikia. Hili lilijitokeza kwa kiwango cha juu kiasi cha kuanza kutuaminisha kuwa nyuma uzalendo kuna jambo lililojificha. Hili linathibitishwa na aina ya maazimio yaliyopendekezwa na PAC. Kama sio hivyo ni kwa nini mjadala haukuwa ma busara?
Kutokana na makandokando haya, itakuwa ni jambo la busara iwapo raisi haitaingia kwenye mkenge na badala yake awarudishie bumge suala hilo ili waagize ukaguzi wa kina kufanyika
Karibuni kwa mjadala.