Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo, ameishukuru Serikali kwa kutoa vivuko vinne vitakavyotoa huduma za usafiri kwa wananchi wa Buchosa
Kauli hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na wananchi wa kata nne zinazounda Kisiwa cha Kome, kilichopo katika Jimbo la Buchosa
Shigongo ametaja vivuko hivyo kuwa ni MV Sengerema, ambacho kitatoa huduma za usafiri kwenye visiwa vya Kasalazi, Gembale hadi Kisiwa cha Soswa
Vingine ni MV Mwanza, MV Kome II, na MV Kome III, ambavyo vyote vitatoa huduma za usafiri kati ya Nyakaliro na Kisiwa cha Kome, Jimbo la Buchosa
Mbunge Shigongo amesema wananchi wa Buchosa wanapaswa kutembea kifua mbele kwa kupata vivuko na miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika jimbo hilo