EMINEM na STAN wake

Keyboard_Warrior

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2015
Posts
6,107
Reaction score
10,473
Kwanza niweke wazi kabisa, EMINEM ndiye mwanamuziki wa HIP HOP ninayemkubali kuliko mwanamuziki mwingine yeyote wa HIP HOP, yaani ninamkubali kiasi kwamba nikiona "list" yoyote inayohusu wanamuziki watatu (3) bora tangu muziki wa HIPHOP upate kuanzishwa, kwangu mimi hiyo "list" inakuwa ni batili kama jina la mkali EMINEM halipo katika hiyo "list". Naam kwangu mimi EMINEM ndio msanii bora kuwahi kutokea kwenye "game" ya HIP HOP (Mnisamehe sana mashabiki wa TUPAC na BIG, maana ni wazi kuwa nitakuwa nimewakera mno).


Haya, niwarudishe kwenye lengo la "thread". Leo nikiwa natazama video mbalimbali za muziki nikakutana na video ya STAN kutoka kwa mkali wangu EMINEM akimshirikisha mwanamama DIDO kutoka Uingereza. Wimbo huu unamzungumzia mshikaji mmoja anayefahamika kama STAN (Stanley), huyo jamaa anamkubali vibaya mno msanii EMINEN, anamkubali EMINEM kiasi kwamba ilifikia hatua akawa anagombana na mke wake, jamaa alifikia hadi kubadilisha muonekano wake ili aweze kufanana na EMINEM.
Sehemu ya Video inaonesha STAN akimuandikia barua EMINEM kulalamika jinsi alivyokua akimpuuzia, STAN alikuwa anajitahidi kuhudhuria show za EMINEM ili EMINEM atambue jinsi anavyomkubali, juhudi za STAN ziligonga mwamba,kwasababu EMINEM hakuonesha kujali kabisa.
Baada ya kumaliza kuandika barua hiyo STAN anaamua kumchukua mke wake ambae alikua mjamzito na kumuingiza kwenye buti ya gari, kisha anaendesha gari mpaka darajani kisha analiingiza gari kwenye mto, hivyo kutokana kutoonesha kujali kwa EMINEM, STAN anaamua kujiua yeye pamoja na mke wake mjamzito, inashangaza eeenhe?
Kwangu mimi hii ndio video bora kuliko zote kutoka kwa mkali EMINEM.

Kutokana na huu wimbo neno "Stan" limeingizwa kwenye kamusi za lugha ya KIINGERZA likiwa na maana kama "USHABIKI ULIOPITILIZA KWA MTU MASHUHURI/MAARUFU"


Kwa wale mnaomkubali EMINEM kama mimi, taja wimbo unaokubamba kutoka kwa mkali huyu.
 
Kifupi ni STAN alimkubali sana EMINEM na kumfanya role model wake...
Hakujua tu kwamba Eminem anaemkubali na kumjua kupitia nyimbo ni tofauti na Eminem wa maisha Halisi,
So Stan alikua Violent kwa jamii na familia yake Hadi kufikia kumuua mke wake mwishoni ...
Akaiga Hadi Ugomvi wa Eminem na mke wake Kim ...akaupeleka kwenye maisha yake Halisi

Stan inafundisha sana Ni my best Song ever ,
Eminem kajigeuza geuza humo,ana rap sehemu ya Eminem na Ana rap sehemu ya Stan (majibizano) Kali Sana hii na Toy Soldier zilichukua best lyrics written Songs awards kibao.

Another kwangu Ni
Slim Shady kwenye LP
Sing for the moment
When am Gone
Mockingbird
Cleaning out my closet
Headlights
Spacebound
Not afraid
Love the way you lie
Aisee Ni kama zote tu za Eminem
2005 shule waliniita aka STAN Hadi leo limenikaa
 
Asante sana chief,alafu nilikua sijui kama ugomvi wa Stan na mke wake ilikua pia ni sehemu ya Stan kumuiga Eminem..!
Hakika Stan alikua mwehu..!
Ila mkongwe,mashabiki aina ya Stan wapo kweli..?
 
Asante sana chief,alafu nilikua sijui kama ugomvi wa Stan na mke wake ilikua pia ni sehemu ya Stan kumuiga Eminem..!
Hakika Stan alikua mwehu..!
Ila mkongwe,mashabiki aina ya Stan wapo kweli..?
Hahaha STAN aliumwa kumkubali Eminem,Kuna sehemu Eminem anamjibu Stan anamwambia I think you need some counseling or something to help ur ass from bouncing off the walls when you get down some,
Stan alimuita Hadi mtoto wake wakike Bonnie,akimaanisha mwembamba from Slim Shady

Eminem pia akamchana
 
Asante sana chief,alafu nilikua sijui kama ugomvi wa Stan na mke wake ilikua pia ni sehemu ya Stan kumuiga Eminem..!
Hakika Stan alikua mwehu..!
Ila mkongwe,mashabiki aina ya Stan wapo kweli..?
Mashabiki aina ya Stan wapo sana mkuu,hata hapa Bongo Kuna mtu anatamani afanye kama Amber Rutty nae akiki,au watoto ambao wapo insta wakimuona wema au nani nao wanajua Yale ndio maisha halisi nao wanatamani kuwa vile
 
Safi sana

Eminem is My Best rapper, Ila mimi sio stan

Stan alizingua

Kwenye Bad Guy, wimbo wa kwanza katka album ya Marshal Mathers Lp2

Mdogo wake Stan Mathew anakuja kumuibukia Eminem na kutaka kulipiza kisasi kwa Eminem kwa kitendo cha yeye Eminem kumpuuzia Stan had kusababisha Stan kujiua.

Bonge la wimbo pia
 
Kajiue na ww beba family yako mkajiue
 
Ahahaaaah...
Stan nyoko sana...
Mimi huwa nacheka sana pale wimbo unaanza Stan yupo chooni anabadilisha rangi ya nywele zake ili afanane na Eminem...
Mke wake anamwita "Stanley, Stanley..."
Stan anamjibu kwa ukali sana "Don't call me that, don't call me that"
Yaani jamaa alikua halitaki hata jina lake..!
 
Ahahaaaah...
Hata mimi pamoja na kumkubali kwangu kote Eminem siwezi kuwa Stan aisee..!
Jamaa alizidisha mahaba..!
Video ya Bad Guy sijapata kuionaga, hivi ipo kweli..?
 
Ahahaaaah...
Hata mimi pamoja na kumkubali kwangu kote Eminem siwezi kuwa Stan aisee..!
Jamaa alizidisha mahaba..!
Video ya Bad Guy sijapata kuionaga, hivi ipo kweli..?
No haipo

Kwenye Marshall mathers lp2 nyimbo zenye video ni chache sana nadhan ni Headlights tu na nyingine mbili
 
Rap god inaingia kwenye karne hii ya sasa.
1. Rap god
2. Not Afraid
3. The Ringer
4. Killshot
5. Lucky you
6. Stepping stone
7.
8.
9.
10.
Malizia hapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…