Keyboard_Warrior
JF-Expert Member
- Oct 10, 2015
- 6,107
- 10,473
Kwanza niweke wazi kabisa, EMINEM ndiye mwanamuziki wa HIP HOP ninayemkubali kuliko mwanamuziki mwingine yeyote wa HIP HOP, yaani ninamkubali kiasi kwamba nikiona "list" yoyote inayohusu wanamuziki watatu (3) bora tangu muziki wa HIPHOP upate kuanzishwa, kwangu mimi hiyo "list" inakuwa ni batili kama jina la mkali EMINEM halipo katika hiyo "list". Naam kwangu mimi EMINEM ndio msanii bora kuwahi kutokea kwenye "game" ya HIP HOP (Mnisamehe sana mashabiki wa TUPAC na BIG, maana ni wazi kuwa nitakuwa nimewakera mno).
Haya, niwarudishe kwenye lengo la "thread". Leo nikiwa natazama video mbalimbali za muziki nikakutana na video ya STAN kutoka kwa mkali wangu EMINEM akimshirikisha mwanamama DIDO kutoka Uingereza. Wimbo huu unamzungumzia mshikaji mmoja anayefahamika kama STAN (Stanley), huyo jamaa anamkubali vibaya mno msanii EMINEN, anamkubali EMINEM kiasi kwamba ilifikia hatua akawa anagombana na mke wake, jamaa alifikia hadi kubadilisha muonekano wake ili aweze kufanana na EMINEM.
Sehemu ya Video inaonesha STAN akimuandikia barua EMINEM kulalamika jinsi alivyokua akimpuuzia, STAN alikuwa anajitahidi kuhudhuria show za EMINEM ili EMINEM atambue jinsi anavyomkubali, juhudi za STAN ziligonga mwamba,kwasababu EMINEM hakuonesha kujali kabisa.
Baada ya kumaliza kuandika barua hiyo STAN anaamua kumchukua mke wake ambae alikua mjamzito na kumuingiza kwenye buti ya gari, kisha anaendesha gari mpaka darajani kisha analiingiza gari kwenye mto, hivyo kutokana kutoonesha kujali kwa EMINEM, STAN anaamua kujiua yeye pamoja na mke wake mjamzito, inashangaza eeenhe?
Kwangu mimi hii ndio video bora kuliko zote kutoka kwa mkali EMINEM.
Kutokana na huu wimbo neno "Stan" limeingizwa kwenye kamusi za lugha ya KIINGERZA likiwa na maana kama "USHABIKI ULIOPITILIZA KWA MTU MASHUHURI/MAARUFU"
Kwa wale mnaomkubali EMINEM kama mimi, taja wimbo unaokubamba kutoka kwa mkali huyu.
Haya, niwarudishe kwenye lengo la "thread". Leo nikiwa natazama video mbalimbali za muziki nikakutana na video ya STAN kutoka kwa mkali wangu EMINEM akimshirikisha mwanamama DIDO kutoka Uingereza. Wimbo huu unamzungumzia mshikaji mmoja anayefahamika kama STAN (Stanley), huyo jamaa anamkubali vibaya mno msanii EMINEN, anamkubali EMINEM kiasi kwamba ilifikia hatua akawa anagombana na mke wake, jamaa alifikia hadi kubadilisha muonekano wake ili aweze kufanana na EMINEM.
Sehemu ya Video inaonesha STAN akimuandikia barua EMINEM kulalamika jinsi alivyokua akimpuuzia, STAN alikuwa anajitahidi kuhudhuria show za EMINEM ili EMINEM atambue jinsi anavyomkubali, juhudi za STAN ziligonga mwamba,kwasababu EMINEM hakuonesha kujali kabisa.
Baada ya kumaliza kuandika barua hiyo STAN anaamua kumchukua mke wake ambae alikua mjamzito na kumuingiza kwenye buti ya gari, kisha anaendesha gari mpaka darajani kisha analiingiza gari kwenye mto, hivyo kutokana kutoonesha kujali kwa EMINEM, STAN anaamua kujiua yeye pamoja na mke wake mjamzito, inashangaza eeenhe?
Kwangu mimi hii ndio video bora kuliko zote kutoka kwa mkali EMINEM.
Kutokana na huu wimbo neno "Stan" limeingizwa kwenye kamusi za lugha ya KIINGERZA likiwa na maana kama "USHABIKI ULIOPITILIZA KWA MTU MASHUHURI/MAARUFU"
Kwa wale mnaomkubali EMINEM kama mimi, taja wimbo unaokubamba kutoka kwa mkali huyu.