Wadau hivi ni kwanini elimu ya juu Tanzania haimuwezeshi mhitimu kujiajiri pindi amalizapo masomo yake,matokeo yake anazunguka mtaani miaka na miaka na vyeti vyake anaishiwa kudhalilishwa na thamani yake kama msomi haionekani tena? Mfano muajiri anahitaji wafanyakazi 10 anaita watu 150 au 100 kwa usaili huu ni udhalilishaji na kucheza na akili za watu.Ni kweli kwamba tunasoma ili tuajiriwe with low pay maisha yetu yote? Na je course na mitaala iliyoko katika vyuo vyetu are they relevant kwa mazingira ya nchi yetu? And what is our specialization as a nation?Duniani,Africa au Africa mashariki na hata ndani ya Tanzania yenyewe tunasifika kwa kutoa wataalamu wa aina au fani gani? Im stand to be corrected endapo sipo sahihi lakini maoni yako ni muhimu zaidi