Elimu ya bongo kigeugeu!

Msafiri Kasian

JF-Expert Member
Sep 9, 2011
2,133
659
Ni miaka 50 ya uhuru,nimetafakari nikaona elimu tunayoipata hapa Tanzania haikidhi haja za watanzania. Kwa vipi?
Serikali imejitahidi kujenga shule kibao za kata ikishirikiana na wananchi,lakini ukijaribu kuangalia,shule nyingi kati ya hizi hazitoi elimu iliyo kamilika. Shule hizi hazina maabara,library,walimu wakutosha na kadhalika.
Ukikuta shule zenye maabara na library,utaona kuwa hazina vifaa vya kutosha. Je,serikali inatazama vp kuhusu hli?
Pia nikatafakari kuhusu elimu inayotolewa katika shule zote hapa nchini kwa kuzingatia mitaala ya elimu,haimsaidii mhitmu wa kidato cha nne kujiajiri au hata kuajiriwa. Vijana wengi wasiofaulu vizuri katika matokeo ya kidato cha nne wanaoishilia mitaani na mara nyingine kujishughulisha na matendo mabaya kama wizi na kuvuta dawa za kulevya. Je,serikali inachukua hatua gani kuhusu hli?

Pia kwa wale wanaofaulu vizuri na hatimaye kufanikiwa kujiunga na elimu ya kidato cha tano na sita,serikali inadiriki kuwanyima haki yao ya msingi ya kujiendeleza kimasomo (elimu ya juu) kwa wale wanafaulu na kuwa na vigezo vya kupatiwa mikopo kutoka serikalini,badala yake wanaonufaika wengi wao ni wale wenye uwezo wa kusomeshwa na wazazi wao.(mniwie radhi kwa hili kama nimemgusa mtu).
Je,mitaala ya elimu hapa nchini Tanzania inawawezesha vipi vijana wa kitanzania kujiajiri?? Tutafakari kwa miaka hamsini(50) ya uhuru elimu imetukomboa vipi!
Na mwisho kabisa nawatakia mtihani mwema wanafunzi wote wa kidato cha nne mwaka 2011,msipanic,good selection of questions,speed and accuracy will save you! All the best.
Naomba kuwasilisha.
 
minavyo ona serikali kama serikali haithamini elimu kama nchi nyingine zinavyoithamini kwa mfano sera mbovu za elimu ambazo hazizingatii mahitaji ya jamii pia poor cordination kati ya curriculum developers na curriculum implimenters,ndo mambo yaliyopo TZ.
 
kawambo juzi katishia wanafunzi watakaogoma chuo na mimi ni mmoja kati ya wale watu watakaofukuzwa naapa mpaka kieleweke na kama ni kufa potelea mbali ****in kawambo mkweli kazi kucheza ngoma elimu kwenu ziro.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom