Either....or... ya kiingereza na Aidha ya kiswahili.

Either....or... ya kiingereza na Aidha ya kiswahili.

Potatoes

Member
Joined
Aug 26, 2016
Posts
78
Reaction score
79
Ufahamu wangu wa wastani wa lugha ya kiingereza na kiswahili umenifanya nione matumizi yasiyo sahihi ya either...or ya kiingereza na neno 'aidha' la kiswahili.

Nimegundua kwamba baadhi ya wazungumzaji wa kiswahili hufikiri kwamba either ...or ya kiingereza kiswahili chake ni aidha. Kwa hiyo nimewasikia hao wazungumzaji wa kiswahili wakisema: Wanaohusika na uchafu wa mazingira aidha ni wananchi au halmashauri za wilaya.

Ninawaonea huruma sana hao waswahili kwa kosa kubwa sana la kudanganyika na matamshi ya kiingereza ya either....or.. na kudhani ni aidha...au..!
Nimeisikia mara nyingi sana hii.

Wazungumzaji wengi wa kiswahili wamesahau kwamba kuna muundo wa 'ama.......au.....' ambao ndio tafsiri ya 'either.....or...'

Hiyo 'aidha' wanayoikimbilia ina maana tofauti kabisa katika kiswahili.
'aidha'=1.zaidi ya hayo.........
2.pia vilevile..........
3.kwa kuongezea.......

Wadau, mwasemaje.Nipo kwenye mstari au nimepotoka?
 
Ufahamu wangu wa wastani wa lugha ya kiingereza na kiswahili umenifanya nione matumizi yasiyo sahihi ya either...or ya kiingereza na neno 'aidha' la kiswahili.

Nimegundua kwamba baadhi ya wazungumzaji wa kiswahili hufikiri kwamba either ...or ya kiingereza kiswahili chake ni aidha. Kwa hiyo nimewasikia hao wazungumzaji wa kiswahili wakisema: Wanaohusika na uchafu wa mazingira aidha ni wananchi au halmashauri za wilaya.

Ninawaonea huruma sana hao waswahili kwa kosa kubwa sana la kudanganyika na matamshi ya kiingereza ya either....or.. na kudhani ni aidha...au..!
Nimeisikia mara nyingi sana hii.

Wazungumzaji wengi wa kiswahili wamesahau kwamba kuna muundo wa 'ama.......au.....' ambao ndio tafsiri ya 'either.....or...'

Hiyo 'aidha' wanayoikimbilia ina maana tofauti kabisa katika kiswahili.
'aidha'=1.zaidi ya hayo.........
2.pia vilevile..........
3.kwa kuongezea.......

Wadau, mwasemaje.Nipo kwenye mstari au nimepotoka?


Wewe unafahamu lugha ipi kwa ufasaha? kwanza tuanzie hapo, yaani lugha yako ni ipi?
 
upo sahihi.. ingawa aidha inatumika kwa sababu ina matamshi sawa na either.. hata paka jina lake sio nyau ila tunamwita nyau kutokana na ule mlio wake wa "Mieow".. kwenye kamusi hakuna mnyama anayeitwa nyau.

kwa hio aidha ni mbadala wa ama, kama nyau ilivyo mbadala wa paka.
 
Wewe unafahamu lugha ipi kwa ufasaha? kwanza tuanzie hapo, yaani lugha yako ni ipi?
Pointi yako ni nini haswa? Nina ufahamu wa wastani wa kiingereza na kiswahili. Lugha yangu hasa niliyozaliwa nayo ni kipare ie my mother tongue is kipare.
 
Pointi yako ni nini haswa? Nina ufahamu wa wastani wa kiingereza na kiswahili. Lugha yangu hasa niliyozaliwa nayo ni kipare ie my mother tongue is kipare.


Kwa hiyo unajua zaidi kuandika na kuongea Kipare klk Kiswahili?
 
Naamini kabisa hakuna MTU yeyote tanzania anaweza kuongea lugha yake kwa ufasaha siyo kiswahili lugha ya taifa wala kingereza na zaidi Hata lugha yamana... Lugha ni kitu kingine jamani cha msingi hapa tuwelewane......maisha yaende
 
Umesahau kuwa moja ya sofa ya lugha huwa inakopa?????? Kiswahili kimekopa hapo neno either kuwa aidha
 
Uko sahihi, shukran kwa usahihisho.
 
Back
Top Bottom