Nimeenda kwenye Duka Moja pale Mailimoja Kibaha kwa ajili ya kununua zawadi za watoto, baada kuchagua vitu nilivyokuwa nahitaji nakufanya malipo nimeshangaa kuona naomba RISITI na kunyimwa kibaya zaidi muuzaji ameanza kunitolea maneno makali akidai Serikali inawapigia kelele wakati TRA haiwapatii hizo EFD Machine ingawaje wanaziitaji.......kilichonishangaza zaidi ni pale muuzaji aliposema MKOA WA PWANI mzima hauna utaratibu wa kutoa RISITI.
TAFADHALI WAHUSIKA WA MAPATO BILASHAKA KUNA HAJA YA KUONGEZA KAZI KUANGALIA HUU MKOA[/QUOTE
Mkuu hilo tatizo tumelipigia kekele sana humu lakini naona wahusika ni kama wamelala au wanamakusudi fulani. Sasa hivi hata ukienda maduka unapewa za kawaida tu.