Eeeh Mungu wangu, Hapa nilipofika...

Eeeh Mungu wangu, Hapa nilipofika...

Guru Master

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2017
Posts
232
Reaction score
619
Mungu niokoe, maji yamenizidi. Yamefika mpaka nafsini mwangu.
Nimezama Baba katika matope
Yasiyowezekana kusimama.

Ewe Mungu angalia wanaokungojea, wasiaibishwe, kwa ajili yangu Ewe Bwana wa Majeshi.
Wanaokutafuta, wasiaibishwe kwa ajili yangu Ewe Bwana wa Majeshi.

Nimefika mpaka maji ya Vilindi Baba, Mkondo wa maji umenigharikisha.
Nimechoka sana na kulia lia,
Koo langu limekauka sana Eeh Mungu.

Mimi maombi yangu yote nakuomba Wewe Bwana.

Kwa maombi yangu,nakuomba wewe,
Kwa Fadhili zako, Bwana Unijibu,
Kwa Rehema zako, Bwana Uniponye
Kwa Neema zako, Bwana Uniokoe
Kwa Upole wako ,Bwana unisikie

😭😭😭😭
 
Pole boss Kama unapitia mapito,
Lau Kama umetushirikisha neno Asante mno
 
⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪⛪
 
Bwana Yesu akuguse kwa mkono wake uliyojaa wingi wa fadhili, hakuna aliyemkimbilia akapata haya! Yupo kukusaidia.

Neno lake linasema Tazama ninasimama mlangoni na kubisha hodi, anisikiaye na kufungua mlango nitaingia kwake....
20210209_220129.jpg
 
Mitihani ya maisha ni yetu sote binadamu
Kila mtu hujaribiwa kwa namna yake kadri Mungu alivyo panga

Jipe moyo
ni kuwa na sabr/subra ktk nyakati hizo
Alhamdullilah alaa kulli haal
Shukrani kwa Mungu ndie aliepanga yote kwa sababu zake.,
 
Huu ni wimbo ulionisaidia kupita kwenye kipindi kibaya cha giza ktk maisha yangu, jaribu labda itakusaidia wewe pia.





MAOMBOLEZO 3


1Mimi ni mtu aliyeona mateso
Kwa fimbo ya ghadhabu yake.
2Ameniongoza na kunipeleka katika giza
Wala si katika nuru.
3Hakika juu yangu augeuza mkono wake
Mara kwa mara mchana wote.

4Amechakaza ngozi yangu na nyama yangu;
Ameivunja mifupa yangu.
5Amejenga boma juu yangu,
Na kunizungusha uchungu na uchovu.
6 Amenikalisha penye giza,
Kama watu waliokufa zamani.

7Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka;
Amenifunga kwa mnyororo mzito.
8 Naam, nikilia na kuomba msaada,
Huyapinga maombi yangu.
9Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa;
Ameyapotosha mapito yangu.

10 Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye,
Kama simba aliye mafichoni.
11 Amezigeuza njia zangu, na kuniraruararua;
Amenifanya ukiwa.
12 Ameupinda upinde wake,
Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.

13Amenichoma viuno
Kwa mishale ya podo lake.
14 Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;
Wimbo wao mchana kutwa.
15 Amenijaza uchungu,
Amenikinaisha kwa pakanga.

16 Amenivunja meno kwa changarawe;
Amenifunika majivu.
17Umeniweka nafsi yangu mbali na amani;
Nikasahau kufanikiwa.
18 Nikasema, Nguvu zangu zimepotea,
Na tumaini langu kwa BWANA.

19Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu,
Pakanga na nyongo.
20Nafsi yangu ingali ikiyakumbuka hayo,
Nayo imeinama ndani yangu.
21Najikumbusha neno hili,
Kwa hiyo nina matumaini.

22 Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii,
Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
23 Ni mpya kila siku asubuhi;
Uaminifu wako ni mkuu.
24 BWANA ndiye fungu langu, husema nafsi yangu,
Kwa hiyo nitamtumaini yeye.

25 BWANA ni mwema kwa hao wamngojeao,
Kwa hiyo nafsi imtafutayo.
26 Ni vema mtu autarajie wokovu wa BWANA
Na kumngojea kwa utulivu.
27 Ni vema mwanadamu aichukue nira
Wakati wa ujana wake.

28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya;
Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake.
29 Na atie kinywa chake mavumbini;
Ikiwa yamkini liko tumaini.
30 Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake;
Ashibishwe mashutumu.

31 Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu
Hata milele.
32Maana ajapomhuzunisha atamrehemu,
Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.
33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu.
Wala kuwahuzunisha.

34Wafungwa wote wa duniani
Kupondwa chini kwa miguu,
35Kuipotosha hukumu ya mtu
Mbele zake Aliye Juu,
36 Na kumnyima mtu haki yake,
Hayo Bwana hayaridhii kabisa.

37 Ni nani asemaye neno nalo likafanyika,
Ikiwa Bwana hakuliagiza?
38 Je! Katika kinywa chake Aliye Juu
Hayatoki maovu na mema?
39 Mbona anung'unika mwanadamu aliye hai
Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?

40 Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu,
Na kumrudia BWANA tena.
41 Na tumwinulie Mungu aliye mbinguni
Mioyo yetu na mikono.
42 Sisi tumekosa na kuasi;
Wewe hukusamehe.

43Umetufunika kwa hasira na kutufuatia;
Umeua, wala hukuona huruma.
44Umejifunika nafsi yako kwa wingu,
Maombi yetu yasipite.
45 Umetufanya kuwa takataka, na vifusi
Katikati ya mataifa.

46Juu yetu adui zetu wote
Wametupanulia vinywa vyao.
47Hofu imetujilia na shimo,
Ukiwa na uharibifu.
48Jicho langu lachuruzika mito ya machozi
Kwa sababu ya kuharibiwa kwa binti zangu.

49Jicho langu latoka machozi lisikome,
Wala haliachi;
50 Hata BWANA atakapoangalia
Na kutazama toka mbinguni.
51Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu,
Kwa ajili ya kuangamizwa kwa binti wa watu wangu.

52 Walio adui zangu bila sababu
Wameniwinda sana kama ndege;
53 Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani,
Na kutupa jiwe juu yangu.
54 Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu,
Nikasema, Nimekatiliwa mbali.
55 Nililiitia jina lako, BWANA, kutoka lile shimo
Liendalo chini kabisa.
56 Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lako
Ili usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu.
57 Ulinikaribia siku ile nilipokulilia;
Ukasema, Usiogope.

58 Ee BWANA umenitetea katika kisa cha nafsi yangu;
Umeukomboa uhai wangu.
59Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee BWANA;
Unihukumie neno langu.
60 Umekiona kisasi chao chote,
Na mashauri yao yote juu yangu.

61Ee BWANA, umeyasikia matukano yao,
Na mashauri yao yote juu yangu;
62Midomo yao walioinuka juu yangu
Na maazimio yao juu yangu mchana kutwa.
63 Uangalie kuketi kwao, na kuinuka kwao;
Wimbo wao ndio mimi.

64 Utawalipa malipo, Ee BWANA,
Sawasawa na kazi ya mikono yao.
65 Utawapa ushup
avu wa moyo;

Laana yako juu yao.
66 Utawafuatia kwa hasira, na kuwaangamiza

Wasiwe tena chini ya mbingu za BWANA
 
huyu hana changamoto yeyote,anazingua tu hapa.naona watu mnampa pole za nn sasa.dogo acha utani ,naona unajichulia yatakapo kufika kiukwelikweli utatia adabu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom