Edwin Mtei asikitishwa na alaani kitendo cha Tundu Lissu kumtukana Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere

Status
Not open for further replies.
Well,

As much as I would love to see this as busara ya Mzee, Lakini ningeomba Mheshimiwa E.Mtei ukane aliyosema Tundu Lissu kwa hoja. Kwamba useme kuwa aliyosema amemsingizia Mwalimu!

Tuambie kuwa siyo Hayati Mwalimu aliyesema Wazanzibari wakiamua kwa hiyari yao kuuhoji Muungano, hatawalazimisha kuendelea nao. Tuambie siyo yeye aliyewasimamisha kazi Wawakilishi wa Zanzibar wakiwemo Aboud Jumbe kienyeji bila hata kujali haki zao kisheria, kwa kuwa walihoji uhalali wa Muungano! Tuambie kuwa siyo Hayati Mwalimu aliyeandika baadaye kuwa "waliwakatalia hoja yao kwa nia njema kabisa"... Na kisha tuambie kama alisema na alifanya hayo, kwa kiongozi wa hadhi yake, tumsemeje! Kwamba alikuwa Mtakatifu sana? Kwamba alichowafanyia Wawakilishi wa Wazanzibari ni haki? Kwamba hakukiuka haki za wenzake? Au kwamba ni utamaduni tunaotaka kujijengea wa mtu tunayemheshimu akifanya upuuzi tuendelee kumwabudu na kumsifia!

Mzee Mtei hii nchi inabadilika! Na pamoja na kupenda kwangu kuwaheshimu wazee lakini nashindwa kulifumbia macho swala la kupotoka kwa uadilifu katika taifa kulikoasisiwa na Waanzilishi wa Taifa, upotofu ambao umekuwa ukirithishwa kwa vizazi vilivyofuatia na kupelekea kufikia hali ya sasa ambapo haki katika Taifa imepotea kabisa na Wananchi wamekuwa watumwa ndani ya nchi yao wenyewe!

Napenda mtuelewe tunapopigania haki za wanyonge walio wengi. Ambao kwa muda mrefu wa utawala wa haohao unaodhani ni wa kuabudiwa umewafanya dhalili na wageni kwenye nchi yao wenyewe, huku wenye fedha na wenye majina makubwa wakiwa juu ya sheria na kupanga mwelekeo wa taifa letu, huku wakijipangia madaraka na majukumu kama vile hii nchi ni mali yao binafsi!. Napenda ufahamu siyo Tundu Lissu, ni Wapenda mabadiliko. Na wapenda mabadiliko wote watakubaliana nami kuwa ili tufanikiwe, ni lazima kwanza tujue tulipoangukia. Kwa sasa nadhani ni sawa kabisa, ili kupata mwelekeo sahihi, tukubali pale kulipo na ukweli hata kama ukweli huo unakera na unawahusu marehemu tunaowapenda!

Vinginevyo nasikitika kuwa kwa hali ilivyo, kinyume kabisa na unavyofikiria nchi hii inawahitaji kina Tundu Lissu wengi zaidi. Watu ambao watasimamia ukweli kama msingi wa haki kwa wote, katika jamii huru inayoamini katika usawa na utu! Na nasisitiza usiwaambie wanaosema wanyamaze eti kwa sababu nyie hamkusema wakati wenu! Mzee wetu mpendwa, "Kila zama na kitabu chake"
 
Edwin Mtei is a political liability to CHADEMA.He has been wrong on so many issues.Lissu was right on his views over Nyerere,Lissu was fighting a strategic war against CCM.He was trying to beat CCM to their own game by pitying them against the very same electorate they (CCM) used to win elections.Sadly,To my surprise,Mtei comes and help to get CCM out of this political trap Lissu and Jussa carefully designed.Lissu must be very disappointed right now following Mtei ignorance of political trap he ensnared CCM.
Well said Mkuu... Mzee Mtei ameruhusu emotions zimtawale bila kujua strategies za Mhe Lisu alizozitumia kuwabana CCM! Mbaya zaidi kwa nafasi yake kama muasisi wa CDM, amedhoofisha harakati bila ya yeye kujua! Labda uzee umemuingia ndiyo maana hisia zimemtawala bila ya kuangalia mwenendo wa mjadala ulivyokuwa unaendelea! Huyu Mzee lazima ajue kuwa kuwang'oa CCM iliyoko madarakani si rahisi bila hoja za nguvu zenye kuwajengea ujasiri wananchi kama afanyavyo Mhe Lisu ...Utamaduni wa reasoning najua hatuna na pengine kizazi cha kale hawakulelewa kuhoji! Kizazi hiki kina hoji kina kosoa regardless ni nani mtoa hoja !!! Bado kwangu Lisu ni mtu muhimu sana kwa Harakati hizi za kidemokrasia ktk nchi yetu ...
 
Yanini kupaka rangi makaburi na kuweka marumaru na hali ndani mifupa imeoza? J.K.Nyerere alikufa na huko aliko hajui lolote ajabu mnamwabudu kama mungu mtu,zaidi ya yote alikuwa binadamu wa kawaida tu tena hata Warioba alimzidi utashi na wengine wengi tu. Watanzania jaribuni kuondoa nidhamu ya uoga,kwasababu ya udikteta wake J.K.Nyerere ndiyo maana mpaka sasa baadhi ya wajinga wajinga wanaliogopa hata jina lake. Hivi wanajf mnaamini kuwa kuna watu wanaona ccm ni chama makini na chenye kuwajali watu wake? Ndiyo Tanzania yetu aibu tupu.
 
Mzee Mtei, kama ni wewe kweli uliyeandika hii kitu basi hujatumia hekima hata kidogo. Kwani hamna vikao vya chama?

Je, tunaweza kujua ni kitu au sehemu gani ya hotuba iliyokuudhi?

mzee mtei ameanza kujitambua sasa..amechelewa sababu saccos yake ya chadema imeshapoteza mvuto
 
Hiki chama ni mkusanyiko wa machizi tu, wao wanajua matusi tu

Majuzi niliifurahia hotuba yake alivyoanza kabla umeme haujakatika, kumbe mwishoni ni matusi matupu!

Ona sasa wamemkera hadi muasisi wao...

Nashauri, TUNDU, na MBOWE wafukuzwe mara moja.
Hakuna cha Mtei ni Usanii tu wa CCM subirini Mtei atakanusha.
 
Hiki chama ni mkusanyiko wa machizi tu, wao wanajua matusi tu

Majuzi niliifurahia hotuba yake alivyoanza kabla umeme haujakatika, kumbe mwishoni ni matusi matupu!

Ona sasa wamemkera hadi muasisi wao...

Nashauri, TUNDU, na MBOWE wafukuzwe mara moja.

Bado hamjamaliza mchezo Wenu wa kuigiza
 
Nimebaatika sijasikia hilo tusi, maana kusikia matusi sio baati, lakini ngoja kwanza nikatafute hilo tusi nikishalipata nilichunguze kama ni tusi au ni kejeli au ni dhihaka ndio nije kushusha maoni yangu.
 
kama ni kweli, muasisi wa CDM ndio kaandika hivyo! nahc akumtendea haki Tindu Lissu! haya ni mambo ambayo yanahitajika yajadiliwe kwenye vikao vya ndani vya chama.

Tundu Lissu alichokifanya ni kudadavua kile alichikifanyia utafiti, alichoamini kwamba kwa nafasi alioipata na kwa mambo anayoyafahamu itakuwa ni vema na haki watanzania kujua historia ya nchi, kwa mfano " nani alijua habari ya Jumbe na ya Sharrif Hamad na wengineo" kwa sababu tu! ya Muungano, hasa vijana wa sasa ambao ni washabiki wa siasa, kwa maoni yangu sioni kosa la Tundu Lissu, ametumia haki ya kikatiba kwamba kila mtanzania anayohaki ya kutoa au kupokea taarifa/habari.
 
Mzee Mtei, kama ni wewe kweli uliyeandika hii kitu basi hujatumia hekima hata kidogo. Kwani hamna vikao vya chama?

Je, tunaweza kujua ni kitu au sehemu gani ya hotuba iliyokuudhi?

Akikujibu basi labuda yu Dar es salaam,

Yaani hoyo kiumbe wa ajabu sana na ajijua u adabu wake ndo maana ama kama Panya...!
Kuendesha Chama huezi kuendesha pekeako lazima pana washauri.

Nakugeiya mfano Edwin Mtei
Hapo katika Chama ni sawa na vile ambavyo ulikuwa hujaoa, hivyo kila kitu ulikifanza pekeako lakini naamini wakati mwangine ulishirikisha wazazi au rafiki zako kama ulihitajia mafanikio na tena endelevu.

Lakini baada ya muda ulioa na watu walikuzidishia hishma baada ya kusikia /kuona kuwa umeoa na naamini ufanisi wako uliongezeka na pia mkeo/wakezo walipawa sifa nyingi mno.

Na kama ungeliharibu na naamini uloharibu na sasa unadhihirisha namna ulivyo na unavyo haribu mambo watu watakupuuza wewe na wale wanokushauri.

Hebu tafakari baadhi ya mambo kisha ndo uwe unafanza presentions zako.

Tafakari, chukua hatua.

NA ntarejea.
 
Last edited by a moderator:
Edwin Mtei fukuzia mbali huyu nguchiro, usikubali wahuni waendelee kuharibu chama chako!
Lissu ni zaidi ya JK!Simpendi Nyerere kwani ndiye aliye asisi Mfumo Kristo na Bakwata mpaka leo BAKWATA HAINA UNIVERSITY WALA HOSPITAL
 
Last edited by a moderator:
Hiki chama ni mkusanyiko wa machizi tu, wao wanajua matusi tu

Majuzi niliifurahia hotuba yake alivyoanza kabla umeme haujakatika, kumbe mwishoni ni matusi matupu!

Ona sasa wamemkera hadi muasisi wao...

Nashauri, TUNDU, na MBOWE wafukuzwe mara moja.

atafukuzwa baba yako ambaye ni mjumbe wa nyumba kumi
 
Ina maana hotuba ya Lissu haikupitiwa na 'vigogo' wa Chadema kabla hajaitoa bungeni?

hivi, ni vigezogani ambavyo vinatumika ili kumfanya mtu apelekwe kupimwa akili? tundu lisu hajatimiza vigezo hivyo? maana tunaweza kulaumu kumbe mwenzetu ana matatizo ya akili. nakumbuka kwenye miaka ya nyuma, alikuwepo rais mmoja wa marekani alishawahi kusema," mwalimu nyerere hakupaswa kuzalhwa kwenye nchi ya afrika. naamini aliyajua haya kuwa sisi waafrika hatujui thamani ya mambo hata tufanyiwe nini. kwamba ipo cku kama ilivyokuwa kwa lisu, nyerere angezalilishwa. wakati mzee mugabe anaazimisha siku yake ya kuzaliwa miezi iliyopita, alisema " bara la afrika bado halijampa mwalimu nyerere hadhi anayolingana nayo. leo lisu anasema malimu nyerere alizoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi! kwamba eti nyerere alikuwa msanii wa kisiasa? ama kweli tenda wema wende zako, usingoje shukrani. mwalimu hawa ndio vijana waliosoma bure enzi zako. wamekula wamesaza sasa wanakutuna. ndio wanasiasa wanaotaka kwenda ikulu hawa.
 
Mbona CCM wanamtukana WARIOBA? CCM wana nini hasa?
Kama jamaa kamtukana Mwl kiukweli siyo sahihi lakini tuangalie hao ccm watamuua Maw
mzee Warioba kwa stress
 
Hakuna cha Mtei ni Usanii tu wa CCM subirini Mtei atakanusha.

Na kuna watu wakaamini kweli pmzee mtei kaandika hii kitu na wanachangia. Lol. Id ina jina lake kwa nini heading iwe kama kaandika mtu mwingine. Alikuwa na haja gani kutumua "Nafsi ya tatu" kama ni yeye mwenyewe. Si angesema "Nimesikitishwa" Badala ya "Edwin Mtei asikitishwa". Mungu kawapiga upofu waongo. Tz nchi ya kuunga unga wananchi wake wa kuunga unga lol. Guys do not believe this. Is a scam
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom