JingalaFalsafa, post: 19618571, member: 81123"]Unenayo ni sahihi kabisa, na ndivyo ilivyopaswa kuwa. Lakini pia ni vyema kujiuliza, kama 40 yrs ilishindwa kutupatia mpango, aje miezi 12 na sisi walewale?
Nipo katika rekodi nikisema kuhamia si jambo baya in fact it's long coming.
Uthubutu wa kuhamia ndicho kilichotakiwa
Uthubutu si kuamka na kusema tunakwenda.
Ni dhamira ya kwamba sasa tunakwenda
Swali muhimu baada ya kuthibitisha uthubutu ni , je, tunakwenda kwa mpango na utaratibu gani? Nani atusaidie katika kuandaa mpango mzima na utekelezaji wake?
Hapa ndipo tatizo lililpoanzia
JE TUNA NAFASI YA KUTOKURUPUKA? Ni lini tulijipanga kutokurupuka leo? Hatujawahi. NI LAZIMA TUPANGE LEO ILI TUSIKURUPUKE NA KESHO. Leo kilicho cha thamani kabisa na mtaji pekee tulionao ni DHATI katika maamuzi yetu, ni wazi hatuna hakika ya matokeo yake kesho, yaweza kuwa shimoni, lakini ni wazi hatuna nafasi hiyo
Dhati tunayo lakini je,is that the right way to do the right thing?
Kwenda shimoni kwasababu tu tunataka uthubutu ni kutenda kwa njia mbaya
Nafasi ya kufanya vizuri tunayo, tulichokosa ni watu wa kutuongoza kufanya vema
Jiulize pia ni lini ulimuundaa yule aliyekuwa katika nafasi ya maamuzi? Kama kilichomfikisha alipo ni jitihada zake binafsi, wewe utamfunga na nini? Hapo ndipo tunapobaki na tumaini moja tu, DHATI YAKE YULE KATIKA MAAMUZI, NA HAKIKA NDIO MTAJI PEKEE KWA SASA HIVI. KUTHUBUTU NI KUTENDA hata pasi na mpangilio, ni kutenda tu.
Kuishi kwa dhati ya mtu na si watu nalo ni tatizo.
Sikubaliani kuwa kuthubutu ni kutenda tu.
Unaingia katika pori kwa kutenda bila kujali dhahma ndani ya msitu.
Ni ili watu wabaki katika majamvi wakiomboleza, alithubutu.
Hapana tuna fursa hatuitumii vema. Tuna kila kila hatujui kupanga.
Tumebaki kuwa kiosk na siyo super market. Tunachukua dakika 45 kutafuta chupa ya maziwa ndani ya kiosk, hatujui kuwa kule mall na super market unaiona kwa dakika moja.
Super market walithubutu kuwekeza, uthubutu uliongozwa na weledi na
maarifa
Tumaini pekee kwetu kwa waendao Dodoma ni kwamba hawatarudi Dar, wanaishije, shida wapatazo, ni gharama ya uzembe wako na wangu, hatuwezi kukwepa, labda tusubiri miaka 40 mingine... walau tumethubutu.Anaita sasa
Tumeridhia askari wakafie vitani kwasababu huko ndiko makazi yao yalipo.
Hatuna sayansi ya kisasa kuwa kushinda vita si kupiga mabomu ni kuhakikisha askari waliokwenda wanabaki salama ili wajao wakute makazi yenye furaha.
Tunajivuna askari hawarudi, hatuangalii gharama itokanayo.
Tumeshindwa kupanga, tunawezaje kuthubutu?
Tusemezane