specialist88
JF-Expert Member
- Aug 31, 2014
- 1,140
- 619
Naandika hapa jukwaani nikiwa na mshangao, maswali na huzuni.
Hivi unaweza ukafikiri au ukadhania kampuni kubwa mbili kama VODACOM Tanzania na Multichoice (DSTV) zinaweza kushindwa kutatua tatizo dogo kabisa ambalo hata mtu mjinga asiye na uelewa analitatua ndani ya dk 10.
Yaani kampuni zenye technology ya hali ya mawasiliano na habari level DSTV na VODACOM zinarushiana mzigo,zinakwepa kazi yao ya msingi kabisa- HUDUMA KWA MTEJA.
Kisa ni hiki, jana nimelipia kifurushi DSTV kupitia VODACOM na nikarejeshewa sms hii
'' DSTV subscription payment successful.
Smartcard/account 10441580320
TZS 19000.00
Trans ID 5IK01O9ZR6S
Reference 5IK01O9ZR6S
If the service is not restored (E16 error), SMS the word RESET with your smartcard number to 15727. For assistance call 0768 988 800''
Baada ya SMS hiyo hakuna kilichofanyika kwenye king' amuzi changu.
Nikawapigia kwanza DSTV, wakanijuza hawajapokea malipo kutoka VODACOM. Nikakaa kimya. Baada ya nusu saa tena nikawapigia VODACOM. Vodacom wao wakasema malipo yangu yamefanikiwa na ela imeshatumwa DSTV. Heeeeee!
Nikalazimika kuwapigia tena DSTV na wao wakanipa tena jibu kama la awali-HATUJAPOKEA MALIPO YAKO.
Nikacheka kwa huzuni, nikajaribu kujiuliza hivi ishu kama hii ikitokea nani wakumlaumu, nani wakuwajibishwa na kwanini hizi kampuni mbili haziwezi kufanya mawasiliano kuhakikisha kama kweli mteja amelipia na kama amelipia ila kumetokea technical error kwanini wasimsaidie mteja wao alafu wao wamalizane ukizingatia hizi ni kampuni kubwa tu na sio rahisi kurushana!
Jana ikapita, leo inapita... Hakuna jibu la maana ninalolipata toka pande zote mbili, DSTV wanasema niwaambie VODACOM wanirudishie pesa zangu na VODACOM wananiambia niwaambie DSTV wanipe huduma maana malipo yameshaenda. HAJABU HII. VICHAA wamepewa ofisi.... Hawawazi kusaidia mteja wao wala kutatua tatizo... wao ni kumrusha mteja huku na kule.
Narudia kusema tena, hapa TANZANIA tunahitaji sijui MUNGU ashuke kutoka wapi aje afundishe watu kuwajibika na kujali mteja..... HAWAJALI.
Nimeandika na bado nina mengi yakuandika ila mpaka sasa bado nina swali moja muhimu kichwani kwangu.. KAMA VODA NA DSTV kampuni kubwa kabisa zinashindwa ku-sort tatizo dogo kama hili kwa zaidi ya masaa 24 pamoja na kuwapigia simu kila mmoja wao kwa zaidi ya mara 3, sasa hizi kampuni ndogo ndogo zitaweza lipi?! Yaani kama DSTV wanashindwa kufanya mawasiliano na VODACOM kuulizia kama kweli mteja amelipia ili wamfungulie huduma, sasa hizi kampuni ndogo zitaweza lipi?!
Kama voda na DSTV zinakumbwa na uzembe wa kiwango hiki, ni wapi na kampuni ipi hapa Tanzania itakuwa na huduma bora kwa wateja?!
Kazi ipo TANZANIA YANGU.
Hivi unaweza ukafikiri au ukadhania kampuni kubwa mbili kama VODACOM Tanzania na Multichoice (DSTV) zinaweza kushindwa kutatua tatizo dogo kabisa ambalo hata mtu mjinga asiye na uelewa analitatua ndani ya dk 10.
Yaani kampuni zenye technology ya hali ya mawasiliano na habari level DSTV na VODACOM zinarushiana mzigo,zinakwepa kazi yao ya msingi kabisa- HUDUMA KWA MTEJA.
Kisa ni hiki, jana nimelipia kifurushi DSTV kupitia VODACOM na nikarejeshewa sms hii
'' DSTV subscription payment successful.
Smartcard/account 10441580320
TZS 19000.00
Trans ID 5IK01O9ZR6S
Reference 5IK01O9ZR6S
If the service is not restored (E16 error), SMS the word RESET with your smartcard number to 15727. For assistance call 0768 988 800''
Baada ya SMS hiyo hakuna kilichofanyika kwenye king' amuzi changu.
Nikawapigia kwanza DSTV, wakanijuza hawajapokea malipo kutoka VODACOM. Nikakaa kimya. Baada ya nusu saa tena nikawapigia VODACOM. Vodacom wao wakasema malipo yangu yamefanikiwa na ela imeshatumwa DSTV. Heeeeee!

Nikalazimika kuwapigia tena DSTV na wao wakanipa tena jibu kama la awali-HATUJAPOKEA MALIPO YAKO.
Nikacheka kwa huzuni, nikajaribu kujiuliza hivi ishu kama hii ikitokea nani wakumlaumu, nani wakuwajibishwa na kwanini hizi kampuni mbili haziwezi kufanya mawasiliano kuhakikisha kama kweli mteja amelipia na kama amelipia ila kumetokea technical error kwanini wasimsaidie mteja wao alafu wao wamalizane ukizingatia hizi ni kampuni kubwa tu na sio rahisi kurushana!
Jana ikapita, leo inapita... Hakuna jibu la maana ninalolipata toka pande zote mbili, DSTV wanasema niwaambie VODACOM wanirudishie pesa zangu na VODACOM wananiambia niwaambie DSTV wanipe huduma maana malipo yameshaenda. HAJABU HII. VICHAA wamepewa ofisi.... Hawawazi kusaidia mteja wao wala kutatua tatizo... wao ni kumrusha mteja huku na kule.
Narudia kusema tena, hapa TANZANIA tunahitaji sijui MUNGU ashuke kutoka wapi aje afundishe watu kuwajibika na kujali mteja..... HAWAJALI.
Nimeandika na bado nina mengi yakuandika ila mpaka sasa bado nina swali moja muhimu kichwani kwangu.. KAMA VODA NA DSTV kampuni kubwa kabisa zinashindwa ku-sort tatizo dogo kama hili kwa zaidi ya masaa 24 pamoja na kuwapigia simu kila mmoja wao kwa zaidi ya mara 3, sasa hizi kampuni ndogo ndogo zitaweza lipi?! Yaani kama DSTV wanashindwa kufanya mawasiliano na VODACOM kuulizia kama kweli mteja amelipia ili wamfungulie huduma, sasa hizi kampuni ndogo zitaweza lipi?!
Kama voda na DSTV zinakumbwa na uzembe wa kiwango hiki, ni wapi na kampuni ipi hapa Tanzania itakuwa na huduma bora kwa wateja?!
Kazi ipo TANZANIA YANGU.