Dr Slaa sasa ni Mzalendo

Dr Slaa sasa ni Mzalendo

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,255
Reaction score
8,027
Katika hii nchi kuna vituko sana mpaka mtu unajiuliza mambo mengi sana! Leo Kuna kundi linampamba Dr Slaa na kumwita Mzalendo, mpiganaji, upinzani wa kweli, mpinga ufisadi! Lakini kabla ya Lowassa Kuhamia Chadema hawa hawa watu walikua wanamwita Padri,kiongozi wa kanisa,Babu,Fisadi anayejikopesa pesa ndani ya Chama,walimwita ni mtu aliyetumwa toka vatkani na Ujerumani! Alipewa majina ya kila aina!

Leo Dr Slaa anasifiwa kinafki na watu wale wale wanamwita Mzalendo wa kweli, mpiganaji! Hawa watu wanashindwa kuelewa kwamba Dr Slaa ni Kichwa kingine anawasoma tu wanavyohangaika na mwisho wa siku aibu yao.

Ni mtu ambaye ambaye anazifahamu fika shida za watanzania, ameshaketi na wenzake mezani kuumiza vichwa ili kuhakikisha wanapata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi October na wakaona silaha pekee ni ile iliyoachwa na wapinzani wao wakuu!

Hawa hawa watu wanaelewa kua kukaribishwa Lowassa CHADEMA ni baada ya vikao vingi vya kamati kuu na kuridhia suala hilo maana Mwenyekiti hawezi kua na sauti peke yake bila ya watendaji wenzake.

Badala ya kupeana mikakati ya namna ya kupambana na nguvu inayokuja kutoka UKAWA wanabaki kummezea Dr Slaa mate huku yeye akiwachora huku yuko bize kuandaa mikakati zaidi ya ushindi mwezi October. Sawa na ile hadithi ya Fisi kumfuatilia binadamu kwa nyuma huku akusubiri mkono uanguke ili aufaidi kumbe binadamu anasonga mbele, kitu ambacho hakiwezekani.

Nionavyo mimi hata kama Lowassa asingekuja UKAWA bado nguvu ingekua kubwa kwa sababu tu kitendo chao cha kihistoria kuungana na kua wamoja mpaka wanafikia kumtoa mgombea urais mmoja,mbunge mmoja kwa kila jimbo na madiwani kwa kila kata ilikua ni ushindi tu.Sasa Lowassa ameongezea nguvu ambayo ni kubwa kwanini watu wasichanganyikiwe? Kwanini watu wasikose usingizi?

Tuwe wakweli tu kwa hili jambo!
 
* Magamba yamechanganyikiwa, mtaa wa lumumba pamebana, wanatafuta kasoro za UKAWA hazina mashiko...wanaona wakomae na Dr...unajua siku ya kufa nyani miti yote huteleza...
 
Kama CHADEMA sio tena chama cha sera na maadili, basi huu ndio wakati wa Dr. Slaa kukihama CHADEMA ili apokelewe kwa mwbembwe na CCM na kupewa ulaji. CCM nao watajiona kuwa wameirudi CDM na kubeba wale wachache ambao wanamuunga mkono Dr. Slaa, kama vile Mzee Mwanakijiji n.k., bila hivyo huu ndio utakuwa mwisho wa Slaa kisiasa.
 
Mbona lowassa alikuwa fisadi sasa amekuwa Kamanda? Unashangaa nini?
 
Kama CHADEMA sio tena chama cha sera na maadili, basi huu ndio wakati wa Dr. Slaa kukihama CHADEMA ili apokelewe kwa mwbembwe na CCM na kupewa ulaji. CCM nao watajiona kuwa wameirudi CDM na kubeba wale wachache ambao wanamuunga mkono Dr. Slaa, kama vile Mzee Mwanakijiji n.k., bila hivyo huu ndio utakuwa mwisho wa Slaa kisiasa.

Wewe kweli ni Kubwajinga unadhani Dr slaa atatoka chadema kwa propaganda zenu mfu hizo, hivi mnadhani ilikuwa kazi ndogo kumleta Lowasa Chadema tumechoka upuuzi wenu
 
Last edited by a moderator:
Kamanda ndiyo siasa zilivyo leo hii Lowassa ni dhahabu Chadema mwezi uliopita alikuwa fisadi wacha watu wajiachie na Slaa.
 
bado ni mapema mno kusema lolote ila ukitaka kushinda vita vya adui wako lazima umpate kibaraka wa mwisho wa upande wa madui zako, huyu ndiye Lowass the most controversial politician in our Tz.
 
slaa na phd yake ya kanisani tunamsubili mwembeyanga tena ,
 
bado ni mapema mno kusema lolote ila ukitaka kushinda vita vya adui wako lazima umpate kibaraka wa mwisho wa upande wa madui zako, huyu ndiye Lowass the most controversial politician in our Tz.

usiwaze wamejipanga wanamalizana nae vizuri tu na wamesema mbinu zilizotumiwa na nyerere kumkalisha chini ,wembe ni uleule,
 
Dr. Slaa usilewe sifa za hao maccm nia yao nikutaka uiache chadema usikubali mkuu
 
MAHANJU

nguvu ya lowasa iko wapi mbona mlisema ni dhaifu ccm wakimpitisha,
 
Last edited by a moderator:
Dr. Slaa usilewe sifa za hao maccm nia yao nikutaka uiache chadema usikubali mkuu

ccm ni chama kongwe akitengemei mtu kutoka kyenye saccoss hila nafsi yake ya unafiki na uzandiki wake zidi ya watanzania kama padre msitaafu afanye maamuzi mwenyewe,lakini bora kuachana na siasa kwa heshima,
 
Tangu lini who mahasimu waitakie mema chadema?
 
Kama CHADEMA sio tena chama cha sera na maadili, basi huu ndio wakati wa Dr. Slaa kukihama CHADEMA ili apokelewe kwa mwbembwe na CCM na kupewa ulaji. CCM nao watajiona kuwa wameirudi CDM na kubeba wale wachache ambao wanamuunga mkono Dr. Slaa, kama vile Mzee Mwanakijiji n.k., bila hivyo huu ndio utakuwa mwisho wa Slaa kisiasa.
Ndiyo nini sasa, mwisho wa Slaa/CCM?
 
hizi ni nyakati za mashaka na kukosa imani ni raisi kwa wale wasiojua nini maana ya kutaka mabadiliko the difference between a rebel and a patriot depends upon who is in power at the moment huu ni wakati wa kutulia na kuonyesha ukomavu wetu kumbukeni hawa ni mabigwa wa kuanzisha hash tag za kuhuzi walianza na # ya udini dhidi ya cuf wakaja na # ya ukabila dhidi ya chadema now wamekuja na # ya dr slaa kutoka chadema bt tunaojua nini maana ya mabadiliko we are not buy cheap politics
 
Back
Top Bottom