Dr. Slaa na Prof. Ibrahim Lipumba na hatma ya UKAWA

Dr. Slaa na Prof. Ibrahim Lipumba na hatma ya UKAWA

Hivi UKAWA kama watampitisha dr. Slaa na kweli wakafanikiwa kushinda uchaguzi katika uundwaji wa baraza la mawaziri kwa mujibu wa katiba ya sasa mawaziri lazima watoke chama alichotoka rais sasa je UKAWA inatambulika kama chama? Na kama haitambuliki kama chama itakuaje katika muundo wa serikali yao ? Vyama vingine vinavyounda ukawa vitashirikishwaje katika serikali ijayo kwa mwenye kujua naomba anijuze.

..mawaziri siyo lazima watoke chama alichotoka Raisi.

..katiba yetu inaruhusu hata waziri mkuu na raisi kutoka vyama tofauti.

..waziri mkuu ni lazima awe mbunge toka chama chenye wabunge wengi ktk bunge la muungano.

..kwa hiyo ikitokea chama kilichotoa Raisi hakina wabunge wengi bungeni, basi raisi na waziri mkuu watatoka vyama tofauti.

..sasa hivi tunaye waziri wa fedha, Mama Saada Mkuya, ambaye aliteuliwa toka serikalini. mpaka sasa hivi hakuna anayejua waziri wa fedha ni mwanachama wa chama kipi cha siasa.

..pia kuna wabunge 10 wa kuteuliwa na raisi. sasa katiba hailazimishi Raisi kuteua wanachama wa chama chake.
 
KABLA YA YOTE KUMBUKA UKAWA NI KIMBILIO LACDM BAADA YA MVURUGANO NA ZITO
HIYO KWENYE
RED NDO UKWELI WENYEWE KWANI KATIKA KATA NINAYOKAA MIMI TUMEKOSA MITAA MITATU KWA UBISHI WA VIONGOZI WA CDM PIA SEHEMU AMBAYO CUF HAWAKUWA NA NGUVU HAWAKUTHUBUTU KUWEKA WAGOMBEA LAKINI CDM WALIFOSI MFANO NI KATIKA MITAA YA KATA ZA BUGURUNI NA VINGUNGUTI LAKINI CUF WALIIBUKA KIDEDEA

NA HIYO KWENYE BLUE YA KWAKO NDO HAINA MASHIKO
CUF NDO ILIKUWA INAONGOZA KUWA NA VIJIJI NA MITAA MINGI BAADA YA CCM KWA HIYO CDM NDO WANUFAIKA WAKUBWA NA UKAWA

Mwishokuna watu wengi nimewasikia wakishauri
NLD itumike kama chama cha dharura kuokoa umoja huu kwa kupewa nafasi ya urais kama KENYA , MWAI KIBAKI alitokea katika chama kidogo na vyama vikubwa vikamsapoti,wapo watu kutoka CCM wanataka kuipa kura ukawa wanashindwa kutokana na UCDM na UCUF


Chadema haiwezi kukimbilia ukawa kwa kigezo cha kukorofishana na Zitto. Politically, Zitto is dead! Na amebaki historia. Ukawa ni umoja ulioundwa kwa misingi ya "umoja ni nguvu" na "Pamoja tunaweza". Hayo mengine ni bla bla Tu!
 
Makaid sialisha maliza jana? Au hamkumsikia kuwa rais atatoka UKAWA na uteuz ushakamilika bado kutangazwa tu. Mbatia atakwenda vunjo na lipumba alisha waambia akitokea mtu mkali zaid yake atamwachia. So uchambuz huu niwakizush tu kuturudisha nyuma umekula midagaa yako umevimbewa unatuchafua tuu. UKAWA ndio dawa yenu labda mumpitishe huyo mkulima wa upande wa wasalit alosa million ya fom. Ccm hoiiiiii hoyeeee
 
Nadhani mjadala huu sio wa maana sana kwani kadri iwavyo atapatikana muwakilishi wa ukawa. Tatizo au changamoto pekee ambayo naiona ni kwamba UKAWA haupo kisheria pia makubaliano yake. Shaka yangu ni kukanana baada ya ushindi au kushindwa... tunaachiana majombo pia nafasi kuu. What if mtu akishinda uraisi or kuzoa majimbo mengi na asishinde na akaamua kutotimiza malengo tunayowekeana? hatuoni vyama vingine tutakuwa tumetapeliwa na tumepotea kabisa?

Mahwelu, Nangu
 
Unajua hii UKAWA japo naiunga mkono lakini inanitatiza sana. Moja ya vigezo muhimu vya kupata ruzuku ya vyama ni ushiriki wa chama katika uchaguzi wa Urais. Wanaposimamisha mgombea mmoja vyama vingine vitapataje ruzuku? Au na ruzuku vitagawana? Vyama vya upinzani karibu vyote havina capacity ya kujiendesha bila ruzuku. Havina rasilimali wala miradi endelevu. Kwakweli natatizika. Anaejua atufafanulie tafadhali.
 
Hivi UKAWA kama watampitisha dr. Slaa na kweli wakafanikiwa kushinda uchaguzi katika uundwaji wa baraza la mawaziri kwa mujibu wa katiba ya sasa mawaziri lazima watoke chama alichotoka rais sasa je UKAWA inatambulika kama chama? Na kama haitambuliki kama chama itakuaje katika muundo wa serikali yao ? Vyama vingine vinavyounda ukawa vitashirikishwaje katika serikali ijayo kwa mwenye kujua naomba anijuze.

Tanzania ina umaskini wa akili katika kufikiri sio Vitu
 
Lini mgombea wa chadema alishinda?

Kumbuka Ndugu Wapiga Kura Wa Tanzania Wanaangalia Zaidi Chama Kuliko Ubora Wa Mgombea, Mara Zote Lipumba Alipogombea Alikua Ni Mgombea Bora Kuliko Wengi, Lakini Hakuwahi Kukaribia Ushindi, Bali Hata Kura Anazopata Zinazidi Kupungua.
 
Back
Top Bottom