Ilongailunga
JF-Expert Member
- Jan 18, 2012
- 1,388
- 896
Wakati mchakato wa uteuzi wa nafasi ya mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM ukiendelea kushika kasi, joto la mchakato huo ndani ya vyama vinavyounda ukawa nalo linazidi kupanda, ni hivi majuzi tu zimesikika habari kuwa Menyekiti wa CUF Prof.Ibrahim Lipumba nae akitangaza kuwa na nia ya kupeprerusha bendera ya umoja huo. Kwangu mimi hapo ndipo tatizo linapoweza kuanzia, haiyumkini kuwa vyama vingine vinavyounda umoja huo hasa CHADEMA vikakubali kwamba CUF ipeperushe bendera ya umoja huo, na hii ni kwasababu mbili zilizowazi, mosi, inaelekea umoja huo umekubali kuwa CUF iwakilishe umoja huo visiwani Zanzibar, hapa ni vigumu kwa umoja huo kukubali CUF pia iuwakilishe Tanzania nzima.
Pili CHADEMA ina nguvu kubwa bara kuliko CUF hivyo itakuwa ni vigumu sana kwa chama hicho kukubali chama chochote kinachounda umoja huo kutoa mgombea wa UKAWA, mantiki ya kisiasa inakubaliana na hoja hii, kuwa CHADEMA tayari kina mtaji mkubwa wa wapiga kura kuliko chama kingine chochote ndani ya umoja huo hivyo kilipaswa chenyewe kiungwe mkono na wala sio kiunge mkono, kazi ambayo CDM ingepewa na umoja huo ni kutafuta na kuleta mgombea ambae anakubalika na makundi yote ndani na nje ya UKAWA.
CUF wakiongozwa na dhana ya kuwa sisi tuna mgombea bora kuliko vyama vingine itakuwa na taathira kubwa katika siasa za UKAWA ni maoni yangu kuwa CUF inaihitaji sana CHADEMA kushinda majimbo mengi ya ubunge bara kuliko CHADEMA inavyoihitaji CUF, Vivyo hivyo kura za wafuasi wa CHADEMA hata kwa uchache gani zitakuwa muhimu sana kuamua hatma ya Urais wa Zanzibar katika uchaguzi ujao, kwa ufupi CUF inaihitaji zaidi UKAWA kujiimarisha katika siasa za Tanzania bara.
Nimeongea na baadhi ya viongozi waandamizi na wanachama wa kawaida ndani ya CUF, wengi wao wamejaa na dhana kuwa CHADEMA iliwasaliti kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, hoja hii haina mashiko kwakuwa ukiangalia takwimu za chaguzi zilizopita za serikali ya mitaa CUF imepata viti vingi vya vijiji, vitongoji na mitaa kuliko chaguzi zilizotangulia,hii ni kusema kuwa CUF imeimarika zaidi ndani ya UKAWA kuliko ilivyokuwa nje ya UKAWA, hoja hii ni kweli kwa vyama vyote vinavyounda umoja huo. Hapa ninaunga mkono maneno yalisemwa bungeni wiki iliyopita na mbunge wa kilwa kusini(CUF) Selemani bungara maarufu kama "-----" kwa kauli yake kuwa viongozi wa UKAWA wakikubali umoja huo uvunjike watakuwa ni wanafiki kuliko CCM na ni wasaliti
Hapo ndipo ninapoiona dhima ya viongozi wawili wanaotajwa kuwania Urais kupitia umoja huo Dr. Slaa na Prof. Lipumba kuwa ni muhimu kuliko wakati wowote toka uanzishwe umoja huo, Lipumba itabidi awe na chaguo moja, kuwapuuza wahafidhina ndani ya chama chake hivyo kukiimarisha zaidi chama chake au kuwakubalia hivyo kukidhoofisha zaidi chama chake (kwa kuwa vyama vingine vitakataa CUF watoe wagombea Urais SMZ na SMT) hivyo kuvunjika rasmi kwa UKAWA, DR. Slaa atakuwa na kazi kubwa ya kuchagua ima akubali kujiweka pembeni hivyo kuwakatisha tamaa wafuasi wengi wa CDM na kumuunga mkono mgombea mwingine (kwa hili CHADEMA itadumaa) au au CDM iingie yenyewe katika uchaguzi mkuu (hili likitokea CDM itabaaki palepale, haitashinda Urais na idadi ya wabunge itapungua au kuongezeka kidogo mno)
Kwa kuhitimisha ni vizuri tukaitaja nafasi ya mwenyekiti wa NCCR Bw. James Mbatia, huyu ni mtu muhimu sana kwa vile anayajua mahitaji ya sasa ya kisiasa na mtu anayefuata political realities, ni mategemeo ya wapenda siasa za ushundani kuwa atakuwa ndio political stabilizer ndani ya UKAWA. Tanzania inahitaji ushindani mkubwa wa kisiasa kwa kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Pili CHADEMA ina nguvu kubwa bara kuliko CUF hivyo itakuwa ni vigumu sana kwa chama hicho kukubali chama chochote kinachounda umoja huo kutoa mgombea wa UKAWA, mantiki ya kisiasa inakubaliana na hoja hii, kuwa CHADEMA tayari kina mtaji mkubwa wa wapiga kura kuliko chama kingine chochote ndani ya umoja huo hivyo kilipaswa chenyewe kiungwe mkono na wala sio kiunge mkono, kazi ambayo CDM ingepewa na umoja huo ni kutafuta na kuleta mgombea ambae anakubalika na makundi yote ndani na nje ya UKAWA.
CUF wakiongozwa na dhana ya kuwa sisi tuna mgombea bora kuliko vyama vingine itakuwa na taathira kubwa katika siasa za UKAWA ni maoni yangu kuwa CUF inaihitaji sana CHADEMA kushinda majimbo mengi ya ubunge bara kuliko CHADEMA inavyoihitaji CUF, Vivyo hivyo kura za wafuasi wa CHADEMA hata kwa uchache gani zitakuwa muhimu sana kuamua hatma ya Urais wa Zanzibar katika uchaguzi ujao, kwa ufupi CUF inaihitaji zaidi UKAWA kujiimarisha katika siasa za Tanzania bara.
Nimeongea na baadhi ya viongozi waandamizi na wanachama wa kawaida ndani ya CUF, wengi wao wamejaa na dhana kuwa CHADEMA iliwasaliti kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, hoja hii haina mashiko kwakuwa ukiangalia takwimu za chaguzi zilizopita za serikali ya mitaa CUF imepata viti vingi vya vijiji, vitongoji na mitaa kuliko chaguzi zilizotangulia,hii ni kusema kuwa CUF imeimarika zaidi ndani ya UKAWA kuliko ilivyokuwa nje ya UKAWA, hoja hii ni kweli kwa vyama vyote vinavyounda umoja huo. Hapa ninaunga mkono maneno yalisemwa bungeni wiki iliyopita na mbunge wa kilwa kusini(CUF) Selemani bungara maarufu kama "-----" kwa kauli yake kuwa viongozi wa UKAWA wakikubali umoja huo uvunjike watakuwa ni wanafiki kuliko CCM na ni wasaliti
Hapo ndipo ninapoiona dhima ya viongozi wawili wanaotajwa kuwania Urais kupitia umoja huo Dr. Slaa na Prof. Lipumba kuwa ni muhimu kuliko wakati wowote toka uanzishwe umoja huo, Lipumba itabidi awe na chaguo moja, kuwapuuza wahafidhina ndani ya chama chake hivyo kukiimarisha zaidi chama chake au kuwakubalia hivyo kukidhoofisha zaidi chama chake (kwa kuwa vyama vingine vitakataa CUF watoe wagombea Urais SMZ na SMT) hivyo kuvunjika rasmi kwa UKAWA, DR. Slaa atakuwa na kazi kubwa ya kuchagua ima akubali kujiweka pembeni hivyo kuwakatisha tamaa wafuasi wengi wa CDM na kumuunga mkono mgombea mwingine (kwa hili CHADEMA itadumaa) au au CDM iingie yenyewe katika uchaguzi mkuu (hili likitokea CDM itabaaki palepale, haitashinda Urais na idadi ya wabunge itapungua au kuongezeka kidogo mno)
Kwa kuhitimisha ni vizuri tukaitaja nafasi ya mwenyekiti wa NCCR Bw. James Mbatia, huyu ni mtu muhimu sana kwa vile anayajua mahitaji ya sasa ya kisiasa na mtu anayefuata political realities, ni mategemeo ya wapenda siasa za ushundani kuwa atakuwa ndio political stabilizer ndani ya UKAWA. Tanzania inahitaji ushindani mkubwa wa kisiasa kwa kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii.