Donors syndrome

Dua

JF-Expert Member
Nov 14, 2006
3,229
662
Fund Your Budget, Donors Tell Tanzania.


Its high time for the government to refuse foreign aid in our budget. We can't seriously depend on them to fund our budget and be free to choose what we want. Enough is enough and we should put our house in order.
 
wewe ota tu!

Shalom, sawa hii inaonekana kama ndoto... lakini ukweli wa mambo ni kuwa tukikomaa inawezekana kujitegemea. Mfano mzuri ndugu yangu ni Kenya...tusife moyo, tuwakomalie viongozi wetu, hata kwa kuandika tu hapa na kujadili mambo...

SteveD.
 
Shalom, sawa hii inaonekana kama ndoto... lakini ukweli wa mambo ni kuwa tukikomaa inawezekana kujitegemea. Mfano mzuri ndugu yangu ni Kenya...tusife moyo, tuwakomalie viongozi wetu, hata kwa kuandika tu hapa na kujadili mambo...

SteveD.

..we ulishaona wapi watu wanaopenda kuomba wakaacha kuomba?muulize matonya na nduguze watakueleza!

..kuomba kukishazoeleka kunakuwa kama utamaduni,wala watu hawaoni haya tena!

..mbaya zaidi unakuta mijibaba na mijimama mizima inaomba wakati ingeweza osha magari au pika mamantilie ikapata fedha tena nyingi!kumbuka uchumi tunao ila tunaukalia!

..kimsingi,ukiwa ombaomba hutoacha kuwa masikini siku zote za maisha yako!

..sasa,hali hiyo ndio aliyonayo tanzania!
 
inasikitisha sana mpaka leo hatuwezi kukusanya kodi zetu,sasa ikija kwenye kusimamia tulizozikusanya au kupewa msaada ndio tutaweza kweli,na hii teknoloji yote bado hatujaweza take advantage ili itusaidie,kazi ya serikali ni kukusanya kodi sasa kama hawawezi hiyo ni failure mbaya sana na tunazidi kuwa maskini tuu,wenzetu cheza na vingine lakini sio kodi yao mana utaishia jela au kukimbia nchi na usirudi tena
 
wewe ota tu!

BTW maneno hayo hapo juu ni ya donors wanakwambia hawawezi kuendelea kukupa dezo na wewe mpokeaji unawaambia waendelee kuota, I wonder nani anaota.

Tatizo lako kubwa binafsi na watu wengine kama wewe ni kutegemea misaada kwa mambo ambayo mnaweza kuyafanya wenyewe. Mimi sishangai kwa nini umeamua kwenda personal wakati unafahami fika kwamba katika viongozi wanafiki na wasiokuwa na aibu ni hili kundi ama genge ambalo tunalo hivi sasa wengi wao ni MAFISADI. Wanapokwenda mikutanoni na kuombaomba wakati uwezo tunao huwa hawaoni aibu? Hata siku moja huwezi ukaona wenzetu kama Wachina, Botswana au hata nchi ndogo kabisa kama Mauritius wakawapigia magoti mafirauni. Leo hii tunagawa mali asili yetu tena bure tu kwa sababu ya peremende, halafu tunapiga makofi kwamba tumesaidiwa.

Jiulize wewe mwenyewe binafsi unaweza kwenda pale kwenye makutano ya Nelson Mandela Road/Sam Nujoma na Morogoro Road na kungoja taa ziwake na kwenda kwa madereva na bakuli na kuomba chochote kwa madereva huku umemshika mwanao mkononi? Kama huwezi kufanya hivyo, Je, ni kwa nini Tanzania as a sovereign state ambayo inaweza kabisa kutumia nguvu ya dola na kukusanya kodi iende na bakuli kwa mafirauni. Huu ni umalaya na hatuwezi kuungalia kwa macho bila kuukemea. Hata watemi wetu hawakuweza kuuza utu wao; kumbuka historia ya Mkwawa, Mirambo na wengineo.

Sisi wengine hatukuzoea kuombaomba kama watoto waliozaliwa na ombaomba.

Serikali ingeweza kabisa kuchukua hatua hivi sasa (kwa mfano) ya kuweza kujenga nyumba za kisasa kwa wananchi na kuweza kusambaza gesi ambayo tunayo kwa wingi kwa matumizi ya nyumbani ili kuokoa matumizi makubwa ya umeme ambao ni ghali. Haya mambo yanawezekana ni kuwa na mipango madhubuti ya kuangalia jinsi tunavyoweza kufaidika na rasilimali zetu. Hatuwezi kila siku kusubiri maamuzi mabaya yanayofanywa na baadhi ya viongozi. (Vile vile gesi tutawauzia nchi zote majirani ambao hawana gesi.)

Mfano mwingine hivi sasa kuna uhaba wa cement serikali imechukua hatua gani kwa mfano kupunguza matumizi ya matofali ya cement (Blocks) kwa kuwa-encourage wajenzi kutumia matofali ya kuchoma? Fikiria ni ajira ya kiasi gani itapatikana kama hili likitokea? Kitu kinachotakiwa ni kuwa na standard ambayo itakubalika na TBS na funds kuwa available.

We can do a lot better kuliko kukaa na kutegemea akina Bill Clinton, Bill Gates, Bono etc. kuja kutujazia madola ambayo yanatafunwa na watu wachache na hata huko yanakoelekezwa yanafika kimkanda mkanda tu.
 
Tanzania ni nchi ambayo inauwezo kabisa wa kujitegemea ila inachohitaji ni kupata viongozi wenye sifa zifuatazo

1. Viongozi wawe na hofu na Mungu (wacha Mungu wa kweli) si ucha mungu wa kuhudhuria ibada hii itapelekea vitu kama ufisadi, rushwa, uzembe, uongo, ulevi, uasherati, nk kuwa ni hadithi tu

2. Wawe na uwezo wa ushawishi kwa wanachi na kutumia muda mwingi kuelezea jamii hasa kijijini nia yao ya dhati ktk yale waliyokusudia kiasi kwamba hata ukimwambia mwananchi kuwa tunafunga mikanda basi wamkubali

3. Elimu yao irandane na kazi au wajibu anaotekeleza na pia uzoefu wa kazi hiyo ou wajibu huo. Kama ni doctor awepo hospitalini na wala si ukuu wa wilaya au mkurugenzi wa jiji. Kama ni engeener awe ktk field yake na siyo kuwa mkuu wa chuo cha siasa kivukoni.
4. viongozi wawe na uwezo wa kubaini vipau mbele na hasa suala la kilimo na waweke limit ya muda wa kuwa ktk kilimo mathalan 2015 tuwe tumeachana na kilimu cha jembe la mkono na kuingia ktk klimo cha kutumia matrekta na by 2030 viwanda vya kusindika mazao ktk kata viwepo.

5. Wawe na uwezo wa kubaini ni elimu ipi inafaa kwa wakati unaofaa. Kama ni tech. school zinafaa wakati huu sawa na kama ni vyuo vikuu sawa wawe na huo uwezo.

6. Wawe na uwezo wa kubaini namna gani jeshi letu la wananchi linaweza kusaidia kuleta maendeleo mbali na kulinda nchi yetu; kuna la ziada jeshi letu pengine linaweza kusaidia

7. wawe na uwezo wa kuleta nidhamu ktk jamii hasa nidhamu ya matumizi ya mali tulizonazo na pesa kidogo tunazopata ni vitu gani tuanze navyo family wise. Familia zetu zinahitaji shule kutoka kwa viongozi wetu tunaowaamini juu ya matumizi yetu na future ya nchi yetu.

8. Namna ya kutumia vyombo vyetu vya habari vichache tulivyonavyo ktk kelimisha watu ktk masuala ya uchumi na kuwapa courage wananchi kuhusu future ya nchi yetu.

hizi ni baadhi tu ya sifa za viongozi wetu ambao wanaweza kutupelekea Tanzania yetu kuwa huru kutokana na misaada hii.Wanachi wako tayari ila wamekosa viongozi hao.
 
wewe ota tu!

Watu wengine bwana,!!!

Anyway, back to the topic. Ukisoma kwa makini hiyo habari unaweza kubaini mambo yafuatayo kwa haraka haraka:
1. Nchi ina rasilimali za kutosha lakini haiwezi kukusanya kodi
2.Pamoja na ukweli kuwa misaada (budget support, whatever) imeendelea kumiminika kwa takribani miaka 40, misaada hii inaonekana kudhoofisha nguvu ya serikali katika kukusanya kodi
3.Pamoja na ukweli kuwa misaada imeendelea kumiminika kwa takribani miaka 40, ukweli ni kuwa impact ya hiyo misaada haionekani kwa wananchi wa kawaida. Ndio maana wanalinganisha hali ya manultrition kwa nchi inayojisifia kuwa na amani na nchi zilizozotoka kwenye migogoro ya kivita kama Angola.

Sasa mwenzetu shalom unaposema "wewe endelea kuota" sijui unamaanisha nini hasa???

Nadhani tatizo kubwa ni kuwa imefika mahali hawa wafadhali wameona kuwa misaada yao haisaidii kuwajenga watanzania katika kukusanya kodi. Kwa hivi, serikali inabidi ichukue hizi comments za donors kama compliment rather than criticism.

 
Hilo kapu linavuja- kwa miaka 50 sasa- misaada ikisitishwa tutaendelea na kupata akili!
So je misaada for how long? now 50? what is time frame? Are we not becoming more dependent?
Hii misaada inamsaidia nani?
 
I dont believe on aid/handouts as a pre-requisite to develoment!

Nakubaliana na wewe 100% Ukiona jirani yako anatoa msaada wa chakula kwenye familia yako, kuvisha nguo wanao, na hela ya matumizi mengine ujue kuna kasoro hapo. Usishangae utakapopima DNA ukagundua kuwa hao watoto si wako. Sasa logic ndogo kama hii, viongozi wetu wanashindwa kabisa kung'amua??? Yaani wamefika mahala wanaona kama ndio utaratibu wa maisha vile!!! Disgusting!!!
 
Hilo kapu linavuja- kwa miaka 50 sasa- misaada ikisitishwa tutaendelea na kupata akili!
So je misaada for how long? now 50? what is time frame? Are we not becoming more dependent?
Hii misaada inamsaidia nani?

Hao wanaotia signature kwenye hayo makaratasi yanayobainisha kiwango cha pesa. Mtoaji na mpokeaji wote wanafaidika. Anayesahaulika ni "mlengwa" au mwananchi wa kawaida. Kwanza sina hakika hata kama huyo "mlengwa" huwa ni "mlengwa sahihi"
 
Kufa kufaana. Kipindi Cha njaa 2005/6 tuliomba misaada lakini ikaliwa vilevile. Umasisikini wa nchi yetu wanaosema wanaomba na wanakula. DHAMBI KUU KWA HAO WANAOKULA KWA MIGONGO YA MASIKINI
 

Misaada mingi tunayopata ni kuendeleza mitindo ya maisha ambayo kabla ya uhuru ilikuwa haipo. Rais wa nchi hafanyi kazi mpaka awe na ndege maalumu. Viongozi wetu wanajua hilo na wakikataa misaada ni wao watakoathrika na sio sisi.
 
Labda huu ni wakati mwanana wa kutembelea maelekezo ya "siasa za ujamaa na kujitegemea"...

Source link: Mwananchi.

SteveD.
 

Well hii ndio sifa kubwa aliyoipata Mkapa kwa hiyo leo mnashangaa kitu gani haswa?. tuliwambieni toka mwanzo sio swala la ukubwa wa fedha in millions bali ni kiasi gani cha asilimia ya fedha zinazokusanywa kulingana na vyanzo vilivyopo. Ndio hayo ya madini kuchangia asilimia 1.9 mfuko wa taifa imekuwa mshtuko mkubwa kwa baadhi ya watu waliokuwa wakisoma amount za mabillioni bila kufahamu kwamba kampuni ya bia ama sigara,kodi zetu za mishahara na pengine hata Bakhresa wote hawa kila mmoja wao huchangia mfuko wetu kwa aslimia kubwa kuliko madini. Hesabu za Nkapa ziliwapiga tobo wengi 2+2 = 22.
 
Hii naona itabakia kuwa ndoto. Ndoto za watu Weusi Amerika zimesikika kinamna yake, sijui kama sisi tutaweza. Hata hivyo mambo yote yanaongozwa kwa nia, hiari na malengo. Siku tutakapokuwa na hivi vitu tutaweza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…