Hivi kuwa na tawi la siasa ulaya faida yake nini hasa kwa mwananchi mlalahoi Tanzania?hivi wakuu haiwaumi nyinyi mnatumiwa dola 250,000 huko ulaya eti kwa ajili ya kuimarisha chama,wakati huku nyumbani huduma muhimu za kijamii kibao zimekwama na hizi pesa ni nyingi na zingeweza kusaidia sana kama zingepelekwa huko?Wewe uliyeleta thread haikuumi ukiona picha kwa michuzi kinamama wamelazwa chini baada ya kujifungua,halafu wewe unafurahia kuimarisha chama huko ulaya?
Halafu Mh Rais anasema Tanzania haina pesa ndiyo maana haiendelei,hivi kweli jamani wakati pesa zenyewe ndiyo hizi zinafujwa tuu hovyohovyo