Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
DUWASA YATEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI AWESO
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) imeanza uchimbaji wa kisima eneo la Kisasa-Mwangaza Jiji Dodoma baada ya maagizo ya Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb.) kwa DUWASA kutafuta suluhisho la changamoto ya maji katika maeneo ya Kisasa Bwawani, Kisasa East, Nyumba 300 na Mwangaza.
Zoezi la uchimbaji wa kisima hicho umeanza Oktoba 11 na utakamilika Oktoba 12, 2024 huku hatua inayofuata ni upimaji wa wingi wa maji na ubora wa maji kabla ya kuanza uendelezaji wa kisima hicho.
Uchimbaji kisima eneo la Kisasa - Mwangaza ni hatua ya utatuzi wa changamoto ya ukosefu wahuduma ya maji kwa wananchi wa maeneo ya Kisasa Bwawani, Kisasa East, Nyumba 300 na Mwangaza.
Baadhi ya Wananchi na Viongozi wa Serikali ya Mtaa Nyumba 300 na Mwangaza wameishukuru serikali kwa kusikia kilio chao katika kuwapatia huduma ya maji.
KERO - √ - Kero ya maji safi jijini Dodoma, Waziri Aweso ingilia kati
Waziri Aweso: DUWASA hakikisha mnatafuta suluhisho la muda mfupi maeneo yenye changamoto ya upatikanaji wa maji, hasa ya pembezoni mwa Mji wa Dodoma
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) imeanza uchimbaji wa kisima eneo la Kisasa-Mwangaza Jiji Dodoma baada ya maagizo ya Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb.) kwa DUWASA kutafuta suluhisho la changamoto ya maji katika maeneo ya Kisasa Bwawani, Kisasa East, Nyumba 300 na Mwangaza.
Zoezi la uchimbaji wa kisima hicho umeanza Oktoba 11 na utakamilika Oktoba 12, 2024 huku hatua inayofuata ni upimaji wa wingi wa maji na ubora wa maji kabla ya kuanza uendelezaji wa kisima hicho.
Uchimbaji kisima eneo la Kisasa - Mwangaza ni hatua ya utatuzi wa changamoto ya ukosefu wahuduma ya maji kwa wananchi wa maeneo ya Kisasa Bwawani, Kisasa East, Nyumba 300 na Mwangaza.
Baadhi ya Wananchi na Viongozi wa Serikali ya Mtaa Nyumba 300 na Mwangaza wameishukuru serikali kwa kusikia kilio chao katika kuwapatia huduma ya maji.
KERO - √ - Kero ya maji safi jijini Dodoma, Waziri Aweso ingilia kati
Waziri Aweso: DUWASA hakikisha mnatafuta suluhisho la muda mfupi maeneo yenye changamoto ya upatikanaji wa maji, hasa ya pembezoni mwa Mji wa Dodoma