PostGE2025 Dkt. Tulia Ackson agawa Vifaa vya Shule kwa Wanafunzi 3,000 wenye Uhitaji Jimbo la Uyole

PostGE2025 Dkt. Tulia Ackson agawa Vifaa vya Shule kwa Wanafunzi 3,000 wenye Uhitaji Jimbo la Uyole

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

PAYE

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
354
Reaction score
395
Januari 10, 2026, Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Uyole, Spika Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU) Mhe. Dkt. Tulia Ackson amegawa vifaa vya shule kwa wanafunzi wenye uhitaji Jimbo la Uyole.

1768310515899.png
Dkt. Tulia anatoa msaada wa Sare za Shule na Daftari kwa Wanafunzi Elfu Tatu (3,000) wenye uhitaji zaidi kutoka kata 13 za Jimbo la Uyole ikiwa ni muendelezo wake wa kuwasaidia watoto wasio jiweza kipindi cha kufungua shule kwa kutoa msaada huo.

1768310597428.png
Aidha, Dkt. Tulia amewataka wazazi na walimu kuwa mstari wa mbele kuhakikisha na kusimamia watoto wanakwenda shule na wanapata Elimu bora kwani kufaulu kwa wanafunzi inategemea na walimu na wazazi kwa pamoja kutia bidii katika kuyatekeleza hayo.

Amemaliza Dkt. Tulia kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji wake katika sekta ya elimu haswa kwenye miundombinu, Serikali ya awamu ya sita imefanikiwa kujenga shule, madarasa na kuboresha miundombinu mingine mashuleni kitendo kitakachopelekea Elimu kukua kwa kasi zaidi na kushawishi wanafunzi kufanya vizuri zaidi.

1768310672717.png

1768310740933.png

1768310796303.png
 
Haisaidii chochote, Njia pekee ni kuweka mipango na sera za kuondoka umasikini
 
Ex JBL Katika ubora wake. Na yule njemba nae kafurushwa TPDC au
 
Januari 10, 2026, Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Uyole, Spika Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU) Mhe. Dkt. Tulia Ackson amegawa vifaa vya shule kwa wanafunzi wenye uhitaji Jimbo la Uyole.

Dkt. Tulia anatoa msaada wa Sare za Shule na Daftari kwa Wanafunzi Elfu Tatu (3,000) wenye uhitaji zaidi kutoka kata 13 za Jimbo la Uyole ikiwa ni muendelezo wake wa kuwasaidia watoto wasio jiweza kipindi cha kufungua shule kwa kutoa msaada huo.

Aidha, Dkt. Tulia amewataka wazazi na walimu kuwa mstari wa mbele kuhakikisha na kusimamia watoto wanakwenda shule na wanapata Elimu bora kwani kufaulu kwa wanafunzi inategemea na walimu na wazazi kwa pamoja kutia bidii katika kuyatekeleza hayo.

Amemaliza Dkt. Tulia kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji wake katika sekta ya elimu haswa kwenye miundombinu, Serikali ya awamu ya sita imefanikiwa kujenga shule, madarasa na kuboresha miundombinu mingine mashuleni kitendo kitakachopelekea Elimu kukua kwa kasi zaidi na kushawishi wanafunzi kufanya vizuri zaidi.

Ni vyema kurudisha shukrani kwa wapiga kura wake.
 
Sio mbunge huyo hakuchaguliwa .

Halafu hii ndio nchi tuliyoambiwa inaonewa wivu na US kutokana na wingi wa rasilimali??

Nchi ambayo watu hawawezi kumudu kununua sare za shule hadi wapewe msaada.
 
Back
Top Bottom