Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,626
Makamu wa Rais Dk Philip Mpango ametilia shaka uaminifu na maadili kwa vijana wa Kitanzania, huku akisema hatma ya Taifa hili ipo mikoni mwa sasa na si kesho.
Dk Mpango ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Agost 7, 2023 wakati akifungua kongamano la vijana 3, 500 wa Mkoa wa Dodoma linalolenga kujadiri fursa zinazowazunguka.
Dk Mpango amesema ni neno lenye ukakasi kulitamka analazimika kufanya hivyo kwa sababu hali si nzuri kwa baadhi ya vijana.
Lengo la kongamano hilo ni kuwafanya vijana watambue fursa zinazowazunguka na kuzichangamkia ili kujiajiri na kuondokana na hali ya kulalamika kuhusu kazi.
“Ni neno lenye ukakasi kulisema lakini ngoja niseme tu, kwamba vijana wengi wa nchi yetu maadili yao yameporomoka, wengi hawana uzalendo na Taifa lao, hawana uadilifu, wavivu na wamejawa na tamaa ya kupata fedha kwa haraka,” amesema Dk Mpango.
Dk Mpango amesema kukosekana kwa uaminifu kwa vijana kunawafanya washindwe kuijenga Tanzania ya sasa na kesho wakati wanategemewa pindi wazee watakapokuwa wamechoka.
Mwananchi