ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,141
- 950
Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa NEMC,Dk Robert Ntakamulenga (aliyesimama katika picha) amefariki dunia leo. Habari za kuaminika toka kwa ndugu jamaa na marafiki zimebainisha hili.
Dr. Ntakamulenga alikuwa miongoni mwa watumishi wachahce sana katika Serikali hii ambao walidhubutu kusimamia kwa dhati Sheria ya Mazingira Na. 20 ya 2004 akiwa na wadhifa wa Ukurugenzi.
Miongoni mwa kazi ambazo zitakumbukwa kuzisimamiwa ni pamoja na:
1. Bomboa bomoa ya nyumba za kifahari za vigogo zilizojengwa kando ya Mito ya Mbezi Beach, Mndumbwe na eneo la Hifadhi ya Mikoko, Dar es Salaam ikwiemo hekalu lililodaiwa kumilikiwa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mchungaji Dk. Getrude Rwakatare
2.Kuwadhibiti wamiliki wa Viwanda ikiwemo kiwanda cha Karibu Textile cha Mbagala jijini Dar es salaam ili kuhakikisha wanafunga mitambo maalum yakusafisha maji taka yatokanayo na bidhaa wanazozitengeneza hasa zinazotumia rangi kabla ya kuyamwaga katika mifumo ya maji machafu ili kupunguza athari za uharibu wa mazingira.
3.Kufunga kiwanda cha nguo cha 21st Century kilichopo Kihonda Morogoro kwa kukiuka sharia ya Mazingira;
MWENYE ENZI MUNGU AMPE PUMZIKO LA MILELE..AMINA!!.
Dr. Ntakamulenga alikuwa miongoni mwa watumishi wachahce sana katika Serikali hii ambao walidhubutu kusimamia kwa dhati Sheria ya Mazingira Na. 20 ya 2004 akiwa na wadhifa wa Ukurugenzi.
Miongoni mwa kazi ambazo zitakumbukwa kuzisimamiwa ni pamoja na:
1. Bomboa bomoa ya nyumba za kifahari za vigogo zilizojengwa kando ya Mito ya Mbezi Beach, Mndumbwe na eneo la Hifadhi ya Mikoko, Dar es Salaam ikwiemo hekalu lililodaiwa kumilikiwa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mchungaji Dk. Getrude Rwakatare
2.Kuwadhibiti wamiliki wa Viwanda ikiwemo kiwanda cha Karibu Textile cha Mbagala jijini Dar es salaam ili kuhakikisha wanafunga mitambo maalum yakusafisha maji taka yatokanayo na bidhaa wanazozitengeneza hasa zinazotumia rangi kabla ya kuyamwaga katika mifumo ya maji machafu ili kupunguza athari za uharibu wa mazingira.
3.Kufunga kiwanda cha nguo cha 21st Century kilichopo Kihonda Morogoro kwa kukiuka sharia ya Mazingira;
MWENYE ENZI MUNGU AMPE PUMZIKO LA MILELE..AMINA!!.