Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
MSIMAMIZI Msaidizi wa Jimbo la Kivule, Wilaya ya Ilala, Dk. Mussa Ally ameipongeza serikali kwa kuwaruhusu wafungwa kushiriki katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu kwa mara ya kwanza.
Akizungumza na Daily News Digital, Dk. Mussa amesema hatua hiyo ni miongoni mwa maboresho makubwa kuelekea uchaguzi huo, ikiwemo kuhakikisha kila Mtanzania anatimiza haki yake ya kikatiba.
“Tumefarijika kuona serikali imewaruhusu wafungwa kupiga kura, hii itakuwa mara ya kwanza,” alisema.
Kwa mujibu wa Dk. Mussa, uamuzi huo unaonyesha dhamira ya serikali kuhakikisha ushirikishwaji wa makundi yote katika mchakato wa kidemokrasia nchini.
Akizungumza na Daily News Digital, Dk. Mussa amesema hatua hiyo ni miongoni mwa maboresho makubwa kuelekea uchaguzi huo, ikiwemo kuhakikisha kila Mtanzania anatimiza haki yake ya kikatiba.
“Tumefarijika kuona serikali imewaruhusu wafungwa kupiga kura, hii itakuwa mara ya kwanza,” alisema.
Kwa mujibu wa Dk. Mussa, uamuzi huo unaonyesha dhamira ya serikali kuhakikisha ushirikishwaji wa makundi yote katika mchakato wa kidemokrasia nchini.