GE2025 Dk. Mussa Ally Apongeza Uamuzi wa Serikali Kuwaruhusu Wafungwa Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba

GE2025 Dk. Mussa Ally Apongeza Uamuzi wa Serikali Kuwaruhusu Wafungwa Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,436
Reaction score
5,234
MSIMAMIZI Msaidizi wa Jimbo la Kivule, Wilaya ya Ilala, Dk. Mussa Ally ameipongeza serikali kwa kuwaruhusu wafungwa kushiriki katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu kwa mara ya kwanza.

Akizungumza na Daily News Digital, Dk. Mussa amesema hatua hiyo ni miongoni mwa maboresho makubwa kuelekea uchaguzi huo, ikiwemo kuhakikisha kila Mtanzania anatimiza haki yake ya kikatiba.

“Tumefarijika kuona serikali imewaruhusu wafungwa kupiga kura, hii itakuwa mara ya kwanza,” alisema.

Kwa mujibu wa Dk. Mussa, uamuzi huo unaonyesha dhamira ya serikali kuhakikisha ushirikishwaji wa makundi yote katika mchakato wa kidemokrasia nchini.

 
Back
Top Bottom