Dk. Kigwangalla kumsomesha Getrude Clement kidato cha tano na cha sita kwenye shule za kisasa

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,502
3,483
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Kigwangalla, kumsomesha Getrude Clement kidato cha tano na cha sita kwenye shule za kisasa
03f3a865-a380-4040-b5dc-bc86baebbf73.jpg

"Huyu binti anaitwa Getrude Clement. Anatokea Jiji la Mwanza, nchini Tanzania. Alipata fursa ya kipekee kuongea kwenye Mkutano wa Umoja wa Mataifa, akikaribishwa na Mhe. Ban Ki Moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kama muwakilishi wa watoto na vijana wote duniani. Ana umri wa miaka kumi na sita.

Leo alikaribishwa kuongea kwenye kikao cha wabunge watetezi wa haki za watoto, alitoa hotuba iliyowatoa watu machozi. Baba yake ni kinyozi na mama yake ni mfanyabiashara mdogo mdogo wa nyanya na vitunguu, na yeye anasoma kidato cha tatu, shule ya sekondari Mnarani (shule ya sekondari ya kata).

Kwa kuthamini kipaji chake na mchango wake, na kutambua nafasi yangu kama Naibu Waziri kwenye Wizara inayosimamia mambo ya Watoto, na kama Mbunge na Mzazi wa mabinti, lakini zaidi kama mtu kutoka kwenye background ya maisha ya chini na ninayethamini mchango wa elimu kwenye maisha yangu, nimeamua kujitolea kumsomesha kidato cha tano na cha sita kwenye shule za kisasa.

Taasisi yangu ya misaada ya kijamii ya Hamisi Kigwangalla Development Foundation itamlipia ada za masomo yake ya high school."

Kujua Mtoto huyu aliongea nini UN, soma=>Mtoto Mtanzania wa miaka 16 alivyoongea kwa kujiamini mbele ya viongozi wa dunia umoja wa mataifa
 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Kigwangalla, kumsomesha Getrude Clement kidato cha tano na cha sita kwenye shule za kisasa
View attachment 344493
"Huyu binti anaitwa Getrude Clement. Anatokea Jiji la Mwanza, nchini Tanzania. Alipata fursa ya kipekee kuongea kwenye Mkutano wa Umoja wa Mataifa, akikaribishwa na Mhe. Ban Ki Moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kama muwakilishi wa watoto na vijana wote duniani. Ana umri wa miaka kumi na sita.

Leo alikaribishwa kuongea kwenye kikao cha wabunge watetezi wa haki za watoto, alitoa hotuba iliyowatoa watu machozi. Baba yake ni kinyozi na mama yake ni mfanyabiashara mdogo mdogo wa nyanya na vitunguu, na yeye anasoma kidato cha tatu, shule ya sekondari Mnarani (shule ya sekondari ya kata).

Kwa kuthamini kipaji chake na mchango wake, na kutambua nafasi yangu kama Naibu Waziri kwenye Wizara inayosimamia mambo ya Watoto, na kama Mbunge na Mzazi wa mabinti, lakini zaidi kama mtu kutoka kwenye background ya maisha ya chini na ninayethamini mchango wa elimu kwenye maisha yangu, nimeamua kujitolea kumsomesha kidato cha tano na cha sita kwenye shule za kisasa.

Taasisi yangu ya misaada ya kijamii ya Hamisi Kigwangalla Development Foundation itamlipia ada za masomo yake ya high school."
Ni vema lakini je wengine kwenye kata ? mmoja tu hatoshi! Hivi huyu binti aliongela kwa kiingereza?? na ilikuwa topic gani?
 
Naibu waziri nitamsomesha huyu mtoto kidato cha tano na sits katika SHULE YA KISASA anamaanisha nini?
 
Nampongeza sana....Dr Kigwangala kwa moyo wake huo wa kujitolea na kusaidia mtoto huyo kwa masomo ya juu! Moyo huo nimeupenda sana!!
 
Ni kweli huyo mtoto katoka familia ya kimasikin!? kwann misaada kama hyo wasipewe watoto wa masikini?

Misallocation of resources
 
Waweke SYSTEM, watu wote wasome kwenye shule nzuri,

CCM ni wasanii sana! Hapo KIGWANGALA anataka kujipatia utukufu binafsi!

Ina maana huyu KIGWANGALA anapingana na Bosi wake Bw.Magufuli kuwa shule za serikali zinatoa elimu bora?

Hizo shule za Kisasa ndio zipi?
 
Yaani binti kuhutubia yueni na jinsi tulivyoichukulia inaonyesha tunapenda sifa kupindukia.

Wasipoangalia ndio wameshaharibu maisha ya huyu binti, maana akili za darasani uraiani ni changamoto.
 
Ni vizuri kumsaidia, kama kweli anahitaji msaada

Ila ningependa kujua kutoka kwa bwana mh, jimboni kwake ashasaidia /anasaidia wangapi, au kwa sababu huyo binti ni maarufu so ndio anajitahidi kuongeza political influence kupitia humo

Siasa za kiafrica shida sana, that's why maendeleo endelevu ni ndoto
 
Je akifeli form four ni shule gani ya kisasa itampokea?

Kwa nini ufadhili usianze immediately kama kweli kaamua kumsaidia?
 
Simpongezi huyo Naibu Waziri. Huyo mtoto ni wazi anatoka katika familia inayomudu gharama za elimu. Ukimsikiliza alivyoongea kwa kujiamini, ni wazi anapata elimu bora. Ni wazi serikali inatakiwa kuwatia moyo watoto kama hawa lakini nadhani Kigwangalla anazungukwa na watoto wengi wasiomudi gharama za elimu. Angemsaidia hata mmoja tu akazitimiza ndoto zake kuliko kutumia kanuni ya mwenye nacho huongezewa.
 
Back
Top Bottom