Hawa ni madj waliojizoelea umaarufu mkubwa ukanda huu wa Africa mashariki kutokana na umahiri wao wa kutafsiri muvi mbalimbali iwe za kihindi, kichina na za kimarekani na nyinginezo ni DJ MARK wa Tanzania na DJ Afro kutoka nchini kenya. Hebu tiririka mdau ni nani mkali wako kati ya hawa madj wawili. Mimi binafsi nawakubali wote kwa kila mmoja na nafasi yake, dj mark ni mkali kwa kutangaza movie za action ee bana ee huyu jamaa utamkubali mwenyewe yaani yuko vizuri kwenye action movie asikwambie mtu na dj Afro yeye namkubali kwa kutafsiri film za mapenzi kama za kihindi na nyinginezo na anavyojua tena kuwa manjonjo kwa kiswahili chake cha kikenya hapo ndo balaa. Kwa upande wako ni nani mkali?
Dj Afro mkali zote,tafuta the defender,deadly pray,missionary man,dragon bridge,once upon a tym in mexico,na za kavita ni hatari,utaskia mavietnamese,hakika mtapenda,afro kiboko
Acha kumfananisha DJ MARK na vitu za kijinga huo ni moto wa kuotea mbali
Hatahivyo Mark amejikita kwenye singo movies zaidi zisizo za kihindi na yupo serious na kinachofanyika huku Afro yeye namuona kwenye zote halafu yeye utoto mwingi kwahiyo kwa watoto na vijana wadogo wanamuelewa sana