Dhana ya ‘Rais Mtarajiwa’

Richard

Platinum Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
16,630
Reaction score
25,586
Neno raisi mtarajiwa ni neno ambalo mara nyingi humaanisha mtu ambae kwa walo wengi wategemea yeye ndie awe raisi hivi karibuni, hata kama bado hajaapishwa au kuchukua majukumu ya kiofisi. Hiki si cheo rasmi lakini kisiasa au kiuandishi wa habari neno hili lina maana sana.

Baada ya uchaguzi mshindi wa kiti cha uraisi huwa ni raisi mteule ambae husubiria kuapishwa pamoja na mgombea mwenza wake.

Lakini katika siasa za Dunia na khasa katika nchi hizi za kwetu kumekuwepo na dhana ya raisi mtarajiwa ambae aweza kuwa ni yule aneonekana ndiye mrithi anefaa kukalia kiti hicho hata baada ya kuapishwa kwa raisi mwenyewe na khasa pale ambapo chama kinotawala kinapoona upo umuhimu huo na pia kama panakuwepo sintofahamu kubwa kufuatia matukio makubwa yanotikisha nchi.

Raisi mtarajiwa ni neno linobeba matarajio kwa mtu ambae aonekana ndiye mwenye nguvu zaidi na ushawishi hata kama upo utaratibu wa kikatiba kisheria wa kuapishwa kwa raisi aliepo.

Hapa Marekani, makamu wa raisi JD Vance ndiye anetarajiwa kumrithi raisi Donald Trumo endapo hali ya kiafya itakuwa si nzuri zaidi au akiamua mwenyewe kuachia madaraka. Vyombo vingi vya habari zimekuwa vikiripoti kwamba mara kadhaa raisi Trump amekuwa akipoteza malengo au kutotilia maanani masuala fulani yanokuwa yakijadiliwa kwenye vikao mbalimbali.

Masuala mengine yanomweka makamu wake DJ Vance katika nafasi ya kupokea kiti cha uraisi wa Marekani ni hali ya kisiasa khasa pale raisi Trump atoapo kauli nyingi tata na zinoonekana zimekosa mwongozo mzuri na wakati mwingine kupuuza ushauri wa wasaidizi khasa wale wanoshauri kuhusu namna ya kuwasilisha ujumbe.

Raisi mtarajiwa pia huweza kushika madaraka endapo raisi alieshinda kwenye uchaguzi atakuwa azidi kupoteza imani na kuzidi pia kutojiamini katika masuala khasa ya kujenga hoja dhidi ya wapinzani au wahasimu wake.

Nini maoni yenu?
 
Unaonekana kuchanganya concepts. Kuna tofauti kubwa kati ya Rais mtarajiwa na Rais mteule!
 
Anaitwa Rais Mteule (President Elect) sio Rais Mtarajiwa
Unaonekana kuchanganya concepts. Kuna tofauti kubwa kati ya Rais mtarajiwa na Rais mteule!
Lakini kama ukitumia mfano wa makamu wa Donald Trump bwana DJ Vance makamu si ataitwa mtarajiwa au "president in waiting"?

Nimerekebisha kidogo maneno kwenye mada ili ieleweke.
 
Richard najua unazungumzia Makamu wa rais kama rais mtarajiwa na sio rais mteule ambaye hajaapishwa, naona kama umewachanganya watu kidogo,
 
Unalenga nini? Kwamba unaona kama Bongo ikitokea TENA?
Hapana.

Marekani mwaka 1974 raisi Richard Nixon aliekuwa raisi wa 37 wa Marekani alijiuzulu baada ya kashfa kubwa iloitwa Watergate ikiwa ni baada ya majaribio mengi ya kuficha ushahidi na kuzuia uchunguzi.

Gerald Ford akateuliwa kuwa makamu wa raisi na baadae akawa raisi wa 38 wa Marekani. Huyu ndie raisi pekee wa Marekani ambae hakuchaguliwa kuwa raisi bali kupandishwa moja kwa moja kuwa raisi.

Mara baada ya kuwa raisi Ford akatoa msamaha wa raisi kwa Richard Nixon.

Kwa muktadha huo ndio, yaweza kutokea ukawa na raisi ambae hakuchaguliwa.

Lakini nadhani tuongelee hili la makamu wa raisi ambae amegombea pamoja na raisi na wakashinda uchaguzi na kuapishwa kisha zikaanza sarakasi.

Nadhani umenielewa.
 
Mbona nazungukia mbali sana, juzi tu hapa Tz Magufuli kafa Samia karithi.
 
Mbona nazungukia mbali sana, juzi tu hapa Tz Magufuli kafa Samia karithi.
Hapana, Samia alikuwa makamu wa hayati JPM na walichaguliwa wote na kuapishwa.

Gerald Ford ndiye mtu pekee ambae aliteuliwa (kutoka nje ya mfumo) kuwa makamu na baadae raisi wa Marekani baada ya Richard Nixon kujiuzulu bila kuchaguliwa kwa kupigiwa kura.
 
Yes why not, inaweza kutokea nani alitegemea Samia atakuwa rais.
Mkuu... kwa hali ya Bongo sasa hivi, uwezo wa kibibi chetu, na kitu baadhi ya watu wanahisi ni mpasuko tayari kati yake na makamu, hata mimi sipingi.
 
Unaonekana kuchanganya concepts. Kuna tofauti kubwa kati ya Rais mtarajiwa na Rais mteule!
Pamoja na hilo. Binafsi nashindwa kujuwa mkuu 'Richard' kalenga nini hasa kwa mada yake hii.

Badala yake kanikumbusha nimuulize ile kesi aliyopeleka kule ICC imefikia wapi; kuna mrejesho wowote hadi sasa?

Mkuu 'Richard' umejaribu sana kuijengea nguvu mada yako hii, lakini binafsi sioni mantiki yake.

Wote wanaoshikilia madaraka sasa hivi ni haramu. Itawezekana vipi huyo Makamu wa Rais haramu awe "President in waiting"? Tuanajaribu kuhalalisha jambo ambalo ni haramu?

Sasa tujiandae Makamu wa Rais Haramu kuchukuwa madaraka ya Rais Haramu, na tubariki mabadiliko hayo na kuyageuza yawe halali?
HAPANA.
 
Pamoja na hilo. Binafsi nashindwa kujuwa mkuu 'Richard' kalenga nini hasa kwa mada yake hii.

Badala yake kanikumbusha nimuulize ile kesi aliyopeleka kule ICC imefikia wapi; kuna mrejesho wowote hadi sasa?
Mkuu, kesi ya ICC ipo mezani kwao na wao wangojewa watoe neno maana hadi leo hawajatoa kauli rasmi.

Nikumbushie tu pia kwamba ile barua yangu ilikuwa ni moja ya barua kadhaa zilopelekwa kule "The Hague".

Yasemwa huenda wapo wazipitia zile barua na ushahidi.
 
Sasa!!?yule mgombea mwenza yaani makam wa Rais wa Richard nixon kwanini hakuapishwa kuwa Rais!!?kwani alijiuzulu na Rais wake ya huyo nixon!!?

Hebu nieleweshe vizuri hapo!
 
Ipo shida au Power Struggle.

Kuna mambo mtu mzima ukiambiwa waharibu yakupasa uketi ujitafakari na ujipange upya.

Ile "speech" ya jana ni mbaya sana.

Siamini kama mzee Tido kashiriki kuandaa ile.
Speech ilitoa ushahidi kwamba:-

1.Alitoa order ya kuua waandamanaji!

2.Aliingiza majeshi ya nchi jirani yafanye mauaji!

3.wauaji walivuka mstari na kuanza kuingia majumbani na kuua watu wasio waandamanaji!

4.majeruhi walikataza wasitibiwe bali wauawe huko mochwari!

5.upo uwezekano Kuna majeruhi walizikwa wazima wazima!

6.Risasi zilizotumika sio za nchi hii ni kinyume na taratibu za kawaida na Sheria za nchi husika!

Ushahidi wa Habil na kabil unaonekana kumaliza kabisa utata na hatua kuchukuliwa!!

Kwahiyo Emmanuel nchimbi atajiuzulu na Raise wake!!?

Halafu ateuliwe makam wa Raise mwingine Ili aapishwe awe Rais!!?

Hilo dodo litamuangukia nani!!?

Cha ajabu sasa wahuni na influence yao wamweke January makamba!!?Sidhani na sielewi au Majaliwa!!?au Bashiru kakurwa au!!?

Hayaeleweki nawaza!
 
Sasa!!?yule mgombea mwenza yaani makam wa Rais wa Richard nixon kwanini hakuapishwa kuwa Rais!!?kwani alijiuzulu na Rais wake ya huyo nixon!!?

Hebu nieleweshe vizuri hapo!
Makamu wa raisi wa Richard Nixon alikuwa Spiro Agnew alikuwa na asili ya Ugiriki. Huyu mjamaa akiwa makamu wa raisi alipokea rushwa zaidi ya dola laki moja na akashtakiwa mahakamani.

Pia akakiri kosa la kutotangaza mali zake na ndo akajiuzulu. Hivyo Agnew alikuwa makamu wa Nixon kati ya mwaka 1969 na 1973.

Agnew alipojiuzulu, ndo Nixon akapendezeza jina la Gerald Ford kuwa makamu wake na ndie aliekuja kuwa raisi baada ya Nixon kujiuzulu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…