Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,630
- 25,586
Neno raisi mtarajiwa ni neno ambalo mara nyingi humaanisha mtu ambae kwa walo wengi wategemea yeye ndie awe raisi hivi karibuni, hata kama bado hajaapishwa au kuchukua majukumu ya kiofisi. Hiki si cheo rasmi lakini kisiasa au kiuandishi wa habari neno hili lina maana sana.
Baada ya uchaguzi mshindi wa kiti cha uraisi huwa ni raisi mteule ambae husubiria kuapishwa pamoja na mgombea mwenza wake.
Lakini katika siasa za Dunia na khasa katika nchi hizi za kwetu kumekuwepo na dhana ya raisi mtarajiwa ambae aweza kuwa ni yule aneonekana ndiye mrithi anefaa kukalia kiti hicho hata baada ya kuapishwa kwa raisi mwenyewe na khasa pale ambapo chama kinotawala kinapoona upo umuhimu huo na pia kama panakuwepo sintofahamu kubwa kufuatia matukio makubwa yanotikisha nchi.
Raisi mtarajiwa ni neno linobeba matarajio kwa mtu ambae aonekana ndiye mwenye nguvu zaidi na ushawishi hata kama upo utaratibu wa kikatiba kisheria wa kuapishwa kwa raisi aliepo.
Hapa Marekani, makamu wa raisi JD Vance ndiye anetarajiwa kumrithi raisi Donald Trumo endapo hali ya kiafya itakuwa si nzuri zaidi au akiamua mwenyewe kuachia madaraka. Vyombo vingi vya habari zimekuwa vikiripoti kwamba mara kadhaa raisi Trump amekuwa akipoteza malengo au kutotilia maanani masuala fulani yanokuwa yakijadiliwa kwenye vikao mbalimbali.
Masuala mengine yanomweka makamu wake DJ Vance katika nafasi ya kupokea kiti cha uraisi wa Marekani ni hali ya kisiasa khasa pale raisi Trump atoapo kauli nyingi tata na zinoonekana zimekosa mwongozo mzuri na wakati mwingine kupuuza ushauri wa wasaidizi khasa wale wanoshauri kuhusu namna ya kuwasilisha ujumbe.
Raisi mtarajiwa pia huweza kushika madaraka endapo raisi alieshinda kwenye uchaguzi atakuwa azidi kupoteza imani na kuzidi pia kutojiamini katika masuala khasa ya kujenga hoja dhidi ya wapinzani au wahasimu wake.
Nini maoni yenu?
Baada ya uchaguzi mshindi wa kiti cha uraisi huwa ni raisi mteule ambae husubiria kuapishwa pamoja na mgombea mwenza wake.
Lakini katika siasa za Dunia na khasa katika nchi hizi za kwetu kumekuwepo na dhana ya raisi mtarajiwa ambae aweza kuwa ni yule aneonekana ndiye mrithi anefaa kukalia kiti hicho hata baada ya kuapishwa kwa raisi mwenyewe na khasa pale ambapo chama kinotawala kinapoona upo umuhimu huo na pia kama panakuwepo sintofahamu kubwa kufuatia matukio makubwa yanotikisha nchi.
Raisi mtarajiwa ni neno linobeba matarajio kwa mtu ambae aonekana ndiye mwenye nguvu zaidi na ushawishi hata kama upo utaratibu wa kikatiba kisheria wa kuapishwa kwa raisi aliepo.
Hapa Marekani, makamu wa raisi JD Vance ndiye anetarajiwa kumrithi raisi Donald Trumo endapo hali ya kiafya itakuwa si nzuri zaidi au akiamua mwenyewe kuachia madaraka. Vyombo vingi vya habari zimekuwa vikiripoti kwamba mara kadhaa raisi Trump amekuwa akipoteza malengo au kutotilia maanani masuala fulani yanokuwa yakijadiliwa kwenye vikao mbalimbali.
Masuala mengine yanomweka makamu wake DJ Vance katika nafasi ya kupokea kiti cha uraisi wa Marekani ni hali ya kisiasa khasa pale raisi Trump atoapo kauli nyingi tata na zinoonekana zimekosa mwongozo mzuri na wakati mwingine kupuuza ushauri wa wasaidizi khasa wale wanoshauri kuhusu namna ya kuwasilisha ujumbe.
Raisi mtarajiwa pia huweza kushika madaraka endapo raisi alieshinda kwenye uchaguzi atakuwa azidi kupoteza imani na kuzidi pia kutojiamini katika masuala khasa ya kujenga hoja dhidi ya wapinzani au wahasimu wake.
Nini maoni yenu?