BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,331
Dhambi ya fedha inatafuna siasa-Mzindakaya
Imeandikwa na Ikunda Erick, Dodoma; Tarehe: 15th July 2010 @ 23:00
MBUNGE wa Kwela, Crisant Mzindakaya (CCM), ameaga bungeni jana na kusema vyama vyote vya siasa, ikiwemo CCM, vimetumbukia kwenye uovu wa dhambi ya namna ya kupata viongozi.
Alitoa kauli hiyo bungeni jana baada ya Spika Samuel Sitta, kumpa dakika 15 badala ya 10 walizopewa kila mbunge kuzungumza wakati wa kuchangia muswada wa Sheria ya Ubia ya Serikali na Kampuni binafsi wa mwaka 2010.
Katika salamu, shukrani na ushauri wake, Mzindakaya alisema Bunge lijalo ambalo litakuwa la 10, ni lazima lifanywe la uchumi na sifa njema ya Taifa nje ya nchi ihamie kwenye masuala ya kukuza uchumi.
Rasilimali tulizo nazo zinatusuta, tunaposaidiwa na nchi kama Uholanzi ambao wamechota bahari wakapata ardhi ili walime, alisema Mzindakaya.
Alisema vitu vyote alivyotoa Mungu, Tanzania inavyo na sio sahihi iwe kwenye hali ya uchumi iliyo nayo leo.
Alisisitiza kwamba ni lazima nchi itumie sheria kati ya matajiri na masikini, kwani utajiri wa nchi uko mikononi mwa watu 10 ambao alishawasema bungeni.
Rudini kwa watu wanyonge, saidieni watu wadogo, hawa wenye pesa achaneni nao, ujamaa utakaokuja baadaye utakuwa wa kuumizana kwa wenye pesa na wale masikini, alisema Mzindakaya.
Aliongeza kuwa watoto wanaosomeshwa sasa kwa baadaye wanakuwa hawana kazi kwa kuwa uchumi umemezwa na watu wachache, na kwamba serikali itaondolewa madarakani na hao watoto wanaosomeshwa sasa.
Tunawasomesha hawa watoto lakini baadaye hawana kazi ya kufanya kwa kuwa uchumi uko mikononi mwa watu wachache, sasa watakuwa mwiba na wataangusha chama tawala, alisema Mzindakaya.
Alisema baada ya miaka 15 watakaowaondoa CCM madarakani ni hao wanaosomeshwa leo, kwa kuwa watakuwa hawana cha kufanya.
Alisisitiza serikali lazima ijenge uchumi wa kati na wa watu wa chini ili kuwa na uwiano wa uchumi, kwani hali itakuwa mbaya ikiwa watu wachache wataendelea kumiliki uchumi.
Alisema siasa za leo ni fedha, wenye fedha ndio wanaopata ubunge wasio nazo hawana lao na kusisitiza kwamba ni lazima vyama vyote vibadilike viache siasa za fedha.
Mimi naondoka bungeni sio kwa uzee, naondoka kwa kujivunia nina akili timamu na bado jimboni watu wananipenda, ninachoomba vyama vyenu vijifunze nidhamu, alisisitiza Mzindakaya.
Alisema wakati akiwa kijana na Mwalimu Nyerere alishaapa kamwe hatakubali ubunge kwa kutoa fedha.
Nilishaapa nikiwa na Nyerere, sitaki ubunge wa fedha na nilisimamia hilo hadi leo, alisema.
Baada ya Mzindakaya kumaliza kutoa shukrani zake, Spika Sitta alimshukuru kwa nasaha zake na kusema, Nashukuru wewe sio mnafiki, ni mkweli tutaendelea kukukumbuka na maneno yako yatadumu kwa kuwa yanahifadhiwa, alimalizia Spika huku wabunge walimshangilia kwa makofi.
Imeandikwa na Ikunda Erick, Dodoma; Tarehe: 15th July 2010 @ 23:00
MBUNGE wa Kwela, Crisant Mzindakaya (CCM), ameaga bungeni jana na kusema vyama vyote vya siasa, ikiwemo CCM, vimetumbukia kwenye uovu wa dhambi ya namna ya kupata viongozi.
Alitoa kauli hiyo bungeni jana baada ya Spika Samuel Sitta, kumpa dakika 15 badala ya 10 walizopewa kila mbunge kuzungumza wakati wa kuchangia muswada wa Sheria ya Ubia ya Serikali na Kampuni binafsi wa mwaka 2010.
Katika salamu, shukrani na ushauri wake, Mzindakaya alisema Bunge lijalo ambalo litakuwa la 10, ni lazima lifanywe la uchumi na sifa njema ya Taifa nje ya nchi ihamie kwenye masuala ya kukuza uchumi.
Rasilimali tulizo nazo zinatusuta, tunaposaidiwa na nchi kama Uholanzi ambao wamechota bahari wakapata ardhi ili walime, alisema Mzindakaya.
Alisema vitu vyote alivyotoa Mungu, Tanzania inavyo na sio sahihi iwe kwenye hali ya uchumi iliyo nayo leo.
Alisisitiza kwamba ni lazima nchi itumie sheria kati ya matajiri na masikini, kwani utajiri wa nchi uko mikononi mwa watu 10 ambao alishawasema bungeni.
Rudini kwa watu wanyonge, saidieni watu wadogo, hawa wenye pesa achaneni nao, ujamaa utakaokuja baadaye utakuwa wa kuumizana kwa wenye pesa na wale masikini, alisema Mzindakaya.
Aliongeza kuwa watoto wanaosomeshwa sasa kwa baadaye wanakuwa hawana kazi kwa kuwa uchumi umemezwa na watu wachache, na kwamba serikali itaondolewa madarakani na hao watoto wanaosomeshwa sasa.
Tunawasomesha hawa watoto lakini baadaye hawana kazi ya kufanya kwa kuwa uchumi uko mikononi mwa watu wachache, sasa watakuwa mwiba na wataangusha chama tawala, alisema Mzindakaya.
Alisema baada ya miaka 15 watakaowaondoa CCM madarakani ni hao wanaosomeshwa leo, kwa kuwa watakuwa hawana cha kufanya.
Alisisitiza serikali lazima ijenge uchumi wa kati na wa watu wa chini ili kuwa na uwiano wa uchumi, kwani hali itakuwa mbaya ikiwa watu wachache wataendelea kumiliki uchumi.
Alisema siasa za leo ni fedha, wenye fedha ndio wanaopata ubunge wasio nazo hawana lao na kusisitiza kwamba ni lazima vyama vyote vibadilike viache siasa za fedha.
Mimi naondoka bungeni sio kwa uzee, naondoka kwa kujivunia nina akili timamu na bado jimboni watu wananipenda, ninachoomba vyama vyenu vijifunze nidhamu, alisisitiza Mzindakaya.
Alisema wakati akiwa kijana na Mwalimu Nyerere alishaapa kamwe hatakubali ubunge kwa kutoa fedha.
Nilishaapa nikiwa na Nyerere, sitaki ubunge wa fedha na nilisimamia hilo hadi leo, alisema.
Baada ya Mzindakaya kumaliza kutoa shukrani zake, Spika Sitta alimshukuru kwa nasaha zake na kusema, Nashukuru wewe sio mnafiki, ni mkweli tutaendelea kukukumbuka na maneno yako yatadumu kwa kuwa yanahifadhiwa, alimalizia Spika huku wabunge walimshangilia kwa makofi.